Sugu ashinda kesi dhidi ya Faiza kuhusu malezi ya mtoto, Faiza aomba nafasi ya kujirekebisha

Status
Not open for further replies.

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
918
1,994
View attachment 262836

Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu amemshtaki aliyewahi kuwa mchumba wake Faiza Ally na aliyezaa naye mtoto kwa madai kuwa mwanamke huyo hana maadili na anahofia atamharibu mtoto wao. Sugu anataka kumchukua mtoto huyo na aishi naye (child custody).

Faiza ameiambia Bongo5 kuwa baada ya siku chache zilizopita kupandishwa kizimbani na kujibu shtaka hilo, alisema yeye hawezi kukubali kumuachia Sugu mtoto huyo kwa kuwa yupo chini ya umri.

"Kweli Sugu amenipeleka mahakamani kumtaka mtoto," amesema Faiza. "Mimi naona ni mtu anayekwepa majukumu kwa sababu chanzo cha yote nilikuwa namkata atulipie kodi ya nyumba, kwa sababu toka tuachane hajawahi kulipa kodi ya nyumba na siyo baba ambae anajali majukumu ya nyumbani kama inavyotakiwa."

"Kwahiyo nilivyoanza kumshauri kuhusu hilo akaniambia yeye anaweza kumchukua mtoto wake na mali zake anaweza kumlea mtoto wake. Sasa nilivyobishana naye kuhusu hilo wiki moja baadaye ndo likaja ili suala la KTMA ndio akalichukulia kama sababu ya kuweza kupeleka suala mahakamani kwa kudai sina maadili, kwahiyo nitammharibu mtoto. Kwahiyo kesho Jumanne ndio hakimu anatoa hukumu juu ya hili.

Lakini mtoto bado ni mdogo ana miaka miwili na kama miezi tisa bado mdogo anahitaji malezi yangu, pia hili suala nitalipeka ustawi wa jamii ili waangalie haki ya malezi ya mama kwa mtoto."


=======

Muendelezo:
Maamuzi ya Mahakama kuhusu kesi aliyoifungua Mbunge Joseph Mbilinyi ‘Sugu' dhidi ya mkewe wa zamani

Sugu-1.jpg

Ni habari ambayo imeandikwa na gazeti ya Mwananchi June 23 2015 ikitokea Mahakamani Manzese Dar es salaam kuhusu kesi iliyokua imefunguliwa na Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi kuhusu mke wake wa zamani.

Taarifa inasema Mahakama ya Manzese imeamuru Mbunge Joseph Mbilinyi akabidhiwe mtoto wao kutokana na kesi aliyoifungua dhidi ya mke wake huyu akidai anamuharibu mtoto.

Hii habari imekuja siku kadhaa tu baada ya TUZO ZA KILI 2015 ambapo mke huyu wa zamani aliingia kwenye headlines kutokana na vazi alilokuwa amevaa.

faizaaa.jpg

=======

Muendelezo: Alichosema mama wa mtoto wa mhe. Sugu baada ya maamuzi ya mahakama

faizamtoto.png


Mahakama ya Sinza Mori imetoa hukumu ya hatma ya mtoto wa Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi na mama wa mtoto wake Faiza kwa kuruhusu mtoto huyo kulelewa na baba yake kwa madai kuwa mama hana vigezo vya kumlea mtoto huyo kimaadili.

Uheard ilipata nafasi ya kuongea na Faiza baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo huku akiwa na huzuni kubwa alisema hajatendewa haki na kudai Mheshimiwa Sugu amekua si baba bora kwa mwanae kwani aliamua kuchukua uamuzi huo baada ya kuombwa kodi ya nyumba, mlevi sana pia amekua na safari nyingi hivyo hawezi kumuhudumia mtoto wao.

Ameongeza kuwa pamoja na lawama ambazo amepewa kuhusu mavazi yake amedai yuko tayari kujirekebisha lakini si kuchukuliwa kwa mtoto wake ambaye ana miaka miwili kwa kuwa amekua akimuhudumia na kumpa kila ambacho mtoto anastahili kupewa.


===========

Muendelezo: Baada ya Sugu Kushinda Kesi,Faiza Asema Bora Kufa Kuliko Kumuona Sasha Akilelewa na Mama Mwingine

sugufaiza.jpg

Baada ya Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Joseph Osmund Mbilinyi ‘Sugu' kushinda kesi mahakamani ya kutaka apewe amlee mtoto wake aitwaye Sasha,aliyekuwa mzazi mwanzake, Faiza Ally amefunguka kuwa ni bora kufa kuliko kumuona mtoto wake akilelewa na mama mwingine wakati yeye yupo hai.

Sugu alimfikisha mahamakani mzazi mwenziye kwa madai kuwa ameshindwa kumlea mtoto wao kwa kuwa mama huyo si mwadilifu.

Faiza ameandika hivi kupitia Akaunti ya Instagram:

"Sielewi joseph ameshindaje kesi - ushahidi wa picha peke yake sioni kama unatosha mimi kupokonya mtoto wangu- mtoto wangu ni mdogo sana ananihitaji sana – na sita rudi hata ikibidi kuuza kila nilicho nacho kwa ajili ya kusimamia hili- sijapewa nafasi nimepelekwa mahakamani ijumaa na leo jumanne nimepewa hukumu/ mwanangu achukuliwe….. hapana !

..Sitarudi nyuma na haitakua rahisi ninakata rufaa na kutafuta wakili wa kunisimamia hili- mwanangu anasoma vizuri anaishi vizuri na naamini kwenye mikono yangu yuko salama zaidi ya kokote/ yaani kuhusu kukosa kukaa na mwanangu ni bora kufa kuliko kuishi nikimuona sasha ana lelewa na mama mwingine ikiwa mimi mama yake niko hai na makini katika malezi ya mtoto wangu - nina ndoto na mwanangu nyingi sana – nahitaji kuishi nae yeye ndio kila kitu kwenye maisha yangu / nampenda sana mwanangu na sijashindwa kumlea - naona uchungu sana kupelekea mahakani na kupokonywa mtoto wangu bila sababu za msingi.

..Sitaogopa cheo chake cha ubunge kamwe - ntasimama kama mama mwenye haki kwa mtoto wake. Mungu naomba nielekeze, nisimamia na unihukumie huu ukatili ninaofanyiwa na baba Sasha".
 
mahakama imefanya uchunguzi kuthibitisha hilo au hicho kivazi tu ndiyo kimekuwa go ahead.... something haipo sawa

Kwa conduct ya Faiza kwa kipindi cha mwaka mmoja unaweza kuifananisha ya baba wa mtoto? Best interest mtt na welfare yake unadhani akiendelea kukaa na mama yake zitazingatiwa?
Faiza hajafanya hivyo kwa kivazi kimoja!!! Na katika kutoka huko zingatia anarudi saa ngapi anarudi na nani na mtoto anamuacha na nani? Mahakamani ni reasonability na weight of evidence ajipange upya kuthibitisha kuwa sugu hafai kukaa na mtoto ila yeye anafaa, apeleke evidence kuonyesha kuwa Sugu hafiiii. Kinachoonekana Evidence alizonazo Sugu kwa sasa zina uzito kuliko utetezi aliotoa Faiza
 
Tusiingilie mambo ya familia ambayo hatufahamu vizuri. Kwa sheria hizi basi wanamuziki na waigizaji wengi duniani wasingeweza kukuza watoto kwa wanavyo vaa au kuonyesha kwenye picha. Kuna vitu vingine sio vizuri kwa mtoto lakini tunaweza tusivione mfano je tunajua kama wazazi wanapigana, wazazi wanavuta sigara mbele ya mtoto, wazazi wanaongea matusi mbele ya mtoto, je kama kuna house girl yukoje, je kuna watu wangapi kwenye nyumba, je shule mtoto anayepelekwa ni nzuri. Hatuwezi kufanya uamuzi kutokana na picha za kwenye mitandao hasa kama mzazi ni muimbaji au muigizaji inabidi kuwe na uchunguzi wa kina
 
Kwa conduct ya Faiza kwa kipindi cha mwaka mmoja unaweza kuifananisha ya baba wa mtoto? Best interest mtt na welfare yake unadhani akiendelea kukaa na mama yake zitazingatiwa?
Faiza hajafanya hivyo kwa kivazi kimoja!!! Na katika kutoka huko zingatia anarudi saa ngapi anarudi na nani na mtoto anamuacha na nani? Mahakamani ni reasonability na weight of evidence ajipange upya kuthibitisha kuwa sugu hafai kukaa na mtoto ila yeye anafaa, apeleke evidence kuonyesha kuwa Sugu hafiiii. Kinachoonekana Evidence alizonazo Sugu kwa sasa zina uzito kuliko utetezi aliotoa Faiza
mimi niliona labda faiza ameshindwa kujenga hoja.. ni sawa tu
 
Sip lazima uwe mwanasheria kigundua kuwa mwanamke anayevaa hayo mavaz hadharani hana maadili wala hawez kuwa mlezi wa mtoto mdogo wa miaka miwili..remember what that kid sees is wat she learns.!!
ukiongelea vazi tu mkuu naona hapana.... kuna watu wanavaa vizuri lakini hawana ulezi bora kwa watoto wao.... kwa kuangalia mavazi hukumu haijatenda haki... kuna kahali fulani cha kukomoana kipo
 
mimi niliona labda faiza ameshindwa kujenga hoja.. ni sawa tu

Best interest and welfare principle za makuzi na malezi ya mtoto ndizo zinazompiga chini Faiza. Ashauriwe.!! kwenda ustawi wa jamii anaongeza mzunguko. Ustawi wa jamii hawabadilishi maamuzi ya mahakama. Ajipange akate rufaa akiwa na sababu zilizoshiba. Maamuzi haya ya awali yaweze kupinduliwa na Mahakama ya juu. Otherwise atazunguka sana.
 
Tusiingilie mambo ya familia ambayo hatufahamu vizuri. Kwa sheria hizi basi wanamuziki na waigizaji wengi duniani wasingeweza kukuza watoto kwa wanavyo vaa au kuonyesha kwenye picha. Kuna vitu vingine sio vizuri kwa mtoto lakini tunaweza tusivione mfano je tunajua kama wazazi wanapigana, wazazi wanavuta sigara mbele ya mtoto, wazazi wanaongea matusi mbele ya mtoto, je kama kuna house girl yukoje, je kuna watu wangapi kwenye nyumba, je shule mtoto anayepelekwa ni nzuri. Hatuwezi kufanya uamuzi kutokana na picha za kwenye mitandao hasa kama mzazi ni muimbaji au muigizaji inabidi kuwe na uchunguzi wa kina
Mambo na tabia za wazungu msizilete Africa, tunategemea huyo mtoto awe president!!, kwa tabia za mama yake tutampata presida??
 
Tusiingilie mambo ya familia ambayo hatufahamu vizuri. Kwa sheria hizi basi wanamuziki na waigizaji wengi duniani wasingeweza kukuza watoto kwa wanavyo vaa au kuonyesha kwenye picha. Kuna vitu vingine sio vizuri kwa mtoto lakini tunaweza tusivione mfano je tunajua kama wazazi wanapigana, wazazi wanavuta sigara mbele ya mtoto, wazazi wanaongea matusi mbele ya mtoto, je kama kuna house girl yukoje, je kuna watu wangapi kwenye nyumba, je shule mtoto anayepelekwa ni nzuri. Hatuwezi kufanya uamuzi kutokana na picha za kwenye mitandao hasa kama mzazi ni muimbaji au muigizaji inabidi kuwe na uchunguzi wa kina

Hata hao waigizaji na wanamuziki huwa wanapelekana sana mahakamani kuhusu mambo ya custody.

Mfano mmoja tu wa haraka haraka ni Usher.

Usher alishinda kesi ya custody dhidi ya mkewe wa zamani.

Bofya hapo Usher Wins Custody Battle Against Tameka Foster
 
ukiongelea vazi tu mkuu naona hapana.... kuna watu wanavaa vizuri lakini hawana ulezi bora kwa watoto wao.... kwa kuangalia mavazi hukumu haijatenda haki... kuna kahali fulani cha kukomoana kipo

Mkuu achana na vivazi, unakumbuka ile story aliyoanza kusimulia few months back kuhusu maisha yake ya kimapenz na Sugu, had akaombwa kusitisha?? Ile inaprove kuwa huyu dada hakuba kitu. Me nisingesubiri Mahakama
 
ukiongelea vazi tu mkuu naona hapana.... kuna watu wanavaa vizuri lakini hawana ulezi bora kwa watoto wao.... kwa kuangalia mavazi hukumu haijatenda haki... kuna kahali fulani cha kukomoana kipo

* Ishu sio mavazi tu...grounds za Sugu zilikuwa nne:

* Kuvaa mavazi ya nusu utupu, kupiga picha za nusu uchi na kuyatupia mtandaoni...

* Kumpiga mtoto picha mbaya ya kuyatupia humohumo mtandaoni...

* Kusafiri mda mrefu na kuwa mbali na mtoto...

* Kutokuwa na kipato cha kuweza kumlea mtoto...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom