Sugu aelezea sakata la ndege ya Rais wa China

Sugu aelezea sakata la ndege ya Rais wa China

batazoba

Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
58
Reaction score
29
Mchango wako wa leo umechangia kwa njia ya aina yake ktk suala la kuitetea nchi kwa ujumla lakini pia hukutupa au kwa lugha nyingine kutuacha vijana nguvu kazi ambao ni Taifa la leo hasa sisi wenye kipato cha chini

ambapo kila kukicha tunadharauliwa na kupewa majina ya kila aina lakini pamoja na yote hayo Mh Sugu bado unakazi sana kuendelea kututetea ili nasi tufanye biashara zetu za kujiajiri wenyewe ili tuwe kukidhi mahitaji ya kila siku.
 
· UCHUNGUZI WA KIMATAIFA UFANYIKE YAWEZEKANA RAIS WA CHINA HAJUI
· MTASIKIA WATU WAMENYONGWA CHINA SABABU SISI HATUCHUKUI HATUA

Mh. Joseph Mbilinyi "Sugu" ameitaka serikali kuchunguza kuhusu tuhuma zilizotolewa na Televisheni ya Al-Jazeera kuhusu sakata linalohusu tuhuma za kuwa ndege ya Rais wa China ilihusika kusafirisha pembe za ndovu kwa kushirikiana na maofisa wa Ikulu. Huku akisisitiza kuwa humu ndani mnasema kuna watu wanaichonganisha serikali na wananchi ila mchawi wa CCM ni CCM yenyewe kwa mambo yanayofanyika kila siku.

Watanzania wa sasa hivi sio wale, wa sasa hivi wanajua kinachoendelea wanaelewa inamaanisha nini wakiona Televisheni ya Al jazeera inapoonyesha kuwa ndege ya Rais wa China pamoja na maofisa wa Ikulu wameshiriki kusafirisha pembe za ndovu. Mbunge huyo amemtaka waziri wa mambo ya nje aache kukurupuka na kutolea majibu kuwa shutuma hizo ni uzushi badala yake wafanye uchunguzi sababu mtu amehojiwa bila kificho anaelezea kwa namna gani wanavyoshirikiana na Wachina katika kusafirisha pembe za ndovu na wanatoa ushahidi wa meno ya ndovu bila kificho.

Sugu akasisitiza kuwa Waziri anasema "Rais wa China kaja alifanya saa ngapi shopping", Mbunge Mbilinyi akahoji yaani inamaanisha Rais wa China aende vinyagoni Mwenge kufanya shopping? Wanasema ile ziara ndiyo imetumika yawezekana ukakuta Rais mwenyewe wa China ajui kuwa ndege yake ilihusika kusafirisha pembe za ndovu mkifanya uchunguzi mtasikia kuna watu wamenyongwa China, sababu sisi hatuwezi kuchukulia hatua watu wetu

kwa mfano mara ya kwanza tulisema kuhusu meli ya Kinana watu wakapiga kelele leo tunaambiwa ndege ya Rais wa China. Ripoti inasema uchunguzi ulifanyika kwa miaka kumi halafu waziri Membe anasimama na kusema kuwa wazungu wameleta uzushi, akasema "kwa nini wazungu wakisema Rais wetu ni kinara wa utawala bora Waziri Membe asemi ni uzushi?" alihoji.

Alitakiwa aje na kusema inatakiwa ufanyike uchunguzi wa Kimataifa tujue ukweli na kama tukigundua Ripoti ni ya uongo, Tanzania kama nchi tuchukue hatua kwa wale waliotuchafua haswa ikichukuliwa taarifa imetolewa na vyombo vikubwa vya habari kama BBC na AL JAZEERA, kufanya mambo ya maendeleo inabidi tushirikishe wananchi na wananchi wanavyokatishwa tamaa na taarifa kama hizi wanashushwa moyo wa kufanya shughuli za maendeleo.
 
Ameongea mambo ya maana sana Sugu, ila makosa hayako kwa ccm, ccm dhahiri imeonyesha imeshindwa na ni mzigo kwa taifa hili, makosa yako kwa watanzania wanaoiunga mkono, nao pia ukitafakari sana, ni kama hawana makosa ni kwa sababu tu ya upeo na elimu kuwa ndogo, taifa hili lina wajinga wengi
 
Nathamani siku moja aongelee habqri za maadili kwa vijana, tuone yeye atwjiweka kundi gani
 
Lakini juu ya hilo kasema jambo bora kabisa!!!
Uchunguzi, uchunguzi, uchunguzi!!!!!
 
Safi sana kamanda sugu! Inshu ya mapanki walisemaga hivyo hivyo badae ikaonekana,ni kweli
 
Nasubiri M4C tour inawezekana kwenye verse moja ya wimbo wa UKAWA tukakuta issue ya ndege iliyobeba pembe zetu.
 
SUGU hajui kitu zaidi ya kufunga suruali chini ya makalio na kuvaa hereni.

Ukosefu wa maadili unatuharibia mijadala. Kazi kutukana na kusema maneno yanayouzi.

Hivi wewe unaweza kumwambia hivyo baba yako anakazi yake ya kuinama?
 
SUGU hajui kitu zaidi ya kufunga suruali chini ya makalio na kuvaa hereni.
Msalani kweli umeshindwa kuona mantiki iliyo katika ujumbe wa Sugu?
Kuna kauliza humu kuwa Membe anajua kila kilichokuwa katika diplomatic bags za ujumbe wa China?
Kwa nini unajitoa fahamu kiasi hiki?
 
Back
Top Bottom