Suala lenyewe liko hivi:1.Tanzania imekosea sana kujitumbukiza kijeshi migogoro ya maziwa makuu. Historically, yenyewe ndio ilikuwa kimbilio la hawa wengine wote. Soma hotuba ya Mwl. Nyerere kwenye mkutano mkuu wa CCM wakati wa mchakato uliompata Hon. Mkapa kama mgombea urais wa CCM. Kwamba tuna majirani 8 wanaotuzunguka na kwa hiyo inatakiwa rais mwenye busara ya hali ya juu jinsi ya kuishi nao. Hilo sasa tumelikosa na kwa miaka miwili iliyobaki litaendelea kutuandama.
2. Eac ina wanachama Burundi, Kenya, Rwanda,Tanzania na Uganda. Kura zikipigwa matokeo yatakuwa 4-1 (yaani wengine wote upande mmoja vs Tanzania upande mwingine. Ukumbuke pia kwamba Secretary General wa EAC ni kutoka Rwanda. 3. Kwa hiyo kwa sasa, sina hakika, inawezekana hawa wanne wakawa na kura ya kutosha kuwaingiza Somalia na Sudan kusini. Hii itafanya kura kuwa 6-1. Kwa hiyo watapitisha uamuzi wowote wautakao kwa wingi wa kura, na kwa maslahi. Kwa hiyo unapozungumzia demokrasia nk kama kigezo, utaanza kujiuliza nani kati ya hawa viongozi wa sasa aliyechaguliwa bila kuiba kura, utakuta ni wa Sudan kusini peke yake! Au nani hakutokea mazingira ya vita au kugandamiza wapinzani unaweza kokosa yoyote. Hilo ndilo tatizo lililopo mbele yetu kwa kukosea pointi namba 1 juu. Ni matumaini yangu kwamba, Rais Kikwete na Membe watafanya kila jitihada za kidiplomasia kurejesha mahusiano na Rwanda kwa faida ya Tanzania. 4.Ukweli ni kwamba, migogoro yote hii, mlengwa ni utajiri wa DRC na ndio uliowatoa roho Lumumba Patrice, Mobutu Seseseko na Kabila baba. Sitashangaa Joseph Kabila akifuata njia hiyohiyo-time will tell. Na watakaomtenda ni kati ya hawa wa hizi nchi sita on top of Usa,France,China,Israel, South Africa na Belgium. 5. Kenya peke yake ndio atafaidika na haya yote tena bila jasho wala jeshi lake maana mazingira yanakuja kutokana na makosa yetu. Siku zote tutambue hakuna Rwanda na Uganda na burundi-lao moja na watu wao na viongozi wao ni watu walewale. EAC sasa iko chini ya kundi hili na huo ndio ukweli. Tanzania ilitakiwa iwe macho tangu awali. Mwono wangu.