Subaru Forester Vs Mazda CX5

Subaru Forester Vs Mazda CX5

Mkuu, iyo CX5 ya 2017 ya Diesel ina Ushuru tu wa Mil 19 hivi.

Nimeonana nazo kadhaa mjini aisee kali sana.
Ni kama hii mkuu au..
IMG-20260206-WA0135.jpeg
 
Mkuu, iyo CX5 ya 2017 ya Diesel ina Ushuru tu wa Mil 19 hivi.

Nimeonana nazo kadhaa mjini aisee kali sana.
Mwanzoni mwa mwezi huu nimepokea CX5 ya 2015 L Package. Nishapiga trip Dar Moshi. Inaridhisha design na performance. Sijui kwanini watu wanashobokea Toyota.
 
101 East juzi nilitaka kupost mada inayohusu hii gari Mazda CX-5 hasa baada ya jamaa yangu hapa kariakoo kununua hii gari...
Hii gari Kwa upande wa interior design iko juu zaidi ya harrier, Subaru forester, vanguard na nissan xtrail. Kama kwenye ishu ya design hii Mazda CX-5 walituliza vichwa mno hata design ya nje pia imekaa vizuri Sana kushinda hizo gari nimetaja pale juu.View attachment 2789230
Mimi nafikiri CX-9 na CX-7 ndiyo Mazda alituliza akili kuliko hata CX - 5
 
Mwanzoni mwa mwezi huu nimepokea CX5 ya 2015 L Package. Nishapiga trip Dar Moshi. Inaridhisha design na performance. Sijui kwanini watu wanashobokea Toyota.
L package ndio top package eeh. Mazda inafurahisha sana aisee.

Bado tuna uwoga wa “mafundi” na spea. Kwahiyo kila mtu anaamini Toyota ndio kimbilio.
 
Hakun
Hii ndio habari ya mjini Kwa wale wapenda magari mazuri

Hizi ni gari shindani kwa sababu zote zipo kundi moja la COMPACT SUV.

Zinafanana sifa katika utendaji kama vile:

1. Ukubwa wa umbo
2. Nafasi kubwa ndani
3. Ground clearance nzuri
4. Nguvu ya kutosha kustahimili
changamoto za barabara
ngumu

Baadhi ya Tofauti ambazo zinaweza kukusaidia kuchagua kati ya SUBARU FORESTER na MAZDA CX5 ni kama vile:
1. Muonekano, macho
yanatofautiana kila mtu ana
Upendeleo binafsi kati ya
Muonekano wa FORESTER na
MAZDA CX5

2. Matumizi ya mafuta, MAZDA
CX5 nyingi ni Diesel na
zinakwenda mpaka 18KM/L
wakati FORESTER ni Petrol na
zinakwenda 14KM/L. Kuhusu
utofauti wa injini ya Petrol na
Diesel unaweza kurejea somo
hilo lipo humu

3. Upatikanaji wa vifaa na
mafundi, Japo gari zote hazipo
kwa wingi sana, lakini subaru
ipo kwa wingi na hata vifaa ni
vingi na mafundi wapo wengi
pia kulinganisha na MAZDA
CX5

4. MAZDA CX5 zilizo nyingi ni
Non-Turbo lakini zinakuwa na
nguvu kubwa kuliko
FORESTER NON-TURBO (XS)
FORESTER XT inazalisha
nguvu kubwa zaidi kuliko
MAZDA NON-TURBO. Lakini
MAZDA CX5 TURBO inazalisha
nguvu kubwa kuizidi kidogo
FORESTER TURBO (XT)

5. Bajeti, MAZDA CX5 bajeti yake
ni kuanzia TSH 27M mpaka
TSH 30M wakati FORESTER
NEW MODEL zinaanzia TSH
25M mpaka TSH 28M lakini
pia FORESTER OLD MODEL
bajeti ni chini zaidi.

Bila shaka maelezo haya yanajitosheleza kukuwezesha kufanya Uchaguzi sahihi.

View attachment 2789002View attachment 2789003
Hakuna tofauti wala yenye afadhali. Yote makopo tu. Gari ni Toyota ya ulinganisho huo. Na ndio maana hata bei Toyota ya ulinganisho wa hizi mfano Harrier ni karibia mara 2 ya hayo makopo. Hata ugumu ni tofauti pia
 
Hakun

Hakuna tofauti wala yenye afadhali. Yote makopo tu. Gari ni Toyota ya ulinganisho huo. Na ndio maana hata bei Toyota ya ulinganisho wa hizi mfano Harrier ni karibia mara 2 ya hayo makopo. Hata ugumu ni tofauti pia
Makopo tenaaa???
Harrier ya 2014 ina utofauti gani wa body na Mazda CX-5 ya 2014?.
Sometimes kukaa kimya ni akili pia
 
Makopo tenaaa???
Harrier ya 2014 ina utofauti gani wa body na Mazda CX-5 ya 2014?.
Sometimes kukaa kimya ni akili pia
Pole kama unahusika nazo.

Hiyo Harrier ya 2014 na mazda jaribu tu hata kulinganisha bei. Ni vitu viwili tofauti. Hata ugumu.
Bahati nzuri nafahamu magari kitambo.
Kibongo bongo tunakimbilia Mazda au subaru au Nissan duas ni ksbb tu ziko chini bei kulinganisha na Toyota zinazolingana kwa muonekano.

Mazda,subaru,Nissan duas,usumbufu wake na uharibikaji wake huwezi kulinganisha na Toyota. Hizo nilizozitaja hapo juu inaweza ikakuharibikia tu ghafla uko safarini, inaweza ikawa kwenye engine au gear box au hata mounting kiasi cha kushindwa kuendelea na safari. Lakini upande wa Toyota yoyote uharibikaji wake lazima itakutaarifu muda kidogo kwamba kuna mahala hapako sawa,labda iwe wewe tu uwe mvivu wa kufuatilia unaposikia kuna utofauti mahala.

Kwa vijana waliongia kizazi cha kuingia kwa hizi subaru,mazida na Nissan akiingia kwenye kutumia hizo tu anaweza kudhani usumbufu anaopitia humo kwenye hizo gari labda hata kwingine ni hivyo hivyo. Toyota hazina usumbufu wa kijinga jinga kama zilivyo hizo gari hapo juu. Hivi karibuni kuna jamaa yangu amepack MAZDA CX5 mpya tu alitumia si zaidi ya mwezi toka aidokoe. Ikaua turbo. Usumbufu wa aina hizo kwenye Toyota haumo.
Kwenye hizi gari tunazotumia kwa wingi huku,ingia Toyota tu itakuvumia sana kuliko hizo zingine
 
Pole kama unahusika nazo.

Hiyo Harrier ya 2014 na mazda jaribu tu hata kulinganisha bei. Ni vitu viwili tofauti. Hata ugumu.
Bahati nzuri nafahamu magari kitambo.
Kibongo bongo tunakimbilia Mazda au subaru au Nissan duas ni ksbb tu ziko chini bei kulinganisha na Toyota zinazolingana kwa muonekano.

Mazda,subaru,Nissan duas,usumbufu wake na uharibikaji wake huwezi kulinganisha na Toyota. Hizo nilizozitaja hapo juu inaweza ikakuharibikia tu ghafla uko safarini, inaweza ikawa kwenye engine au gear box au hata mounting kiasi cha kushindwa kuendelea na safari. Lakini upande wa Toyota yoyote uharibikaji wake lazima itakutaarifu muda kidogo kwamba kuna mahala hapako sawa,labda iwe wewe tu uwe mvivu wa kufuatilia unaposikia kuna utofauti mahala.

Kwa vijana waliongia kizazi cha kuingia kwa hizi subaru,mazida na Nissan akiingia kwenye kutumia hizo tu anaweza kudhani usumbufu anaopitia humo kwenye hizo gari labda hata kwingine ni hivyo hivyo. Toyota hazina usumbufu wa kijinga jinga kama zilivyo hizo gari hapo juu. Hivi karibuni kuna jamaa yangu amepack MAZDA CX5 mpya tu alitumia si zaidi ya mwezi toka aidokoe. Ikaua turbo. Usumbufu wa aina hizo kwenye Toyota haumo.
Kwenye hizi gari tunazotumia kwa wingi huku,ingia Toyota tu itakuvumia sana kuliko hizo zingine
Kila MTU duniani anajua Hilo kuwa Toyota ndiyo gari zinazoaminika hakuna ubishi kwenye hili... wamiliki wa brand tofauti na Toyota tumetokea hukohuko kwenye Toyota.

Haiwezezekani wote tuendeshe Toyota Tu eti kwasababu ni imara
 
Back
Top Bottom