Eleza kwanini culture zinatofautiana tuanzie hapo
Mbona rahisi Sana hiyo.
Binadamu tupo tofauti ndio maana culture ni tofauti; tunatofautiana mambo makuu Yafuatayo;
1. Rangi
Wapo weupe, wekundu, wanjano, na Weusi.
Nywele za kijivu, nyeusi, ugoro n.k
Macho meusi, ugoro, samawati, kijivu n.k
2. Maumbile.
Wapo wenye Nywele Kama Sufi, nywele Kama kamba, kipilipili n.k.
Warefu, wafupi, wawastani.
3. Tofauti za kijiografia hapa tuna vipengele vifuatavyo;
3.1 Tabia ya nchi, Ujangwa, utropika Savannah, uikweta, umediterania n.k
3.2 Maumbile ya Ardhi Kama milima, mabonde, tambarare n.k
Usitegemee watu wanaoishi ikweta waishi Kama watu wanaoishi Jangwani,
Usitegemee Mtu mwenye rangi nyeupe na nywele ndefu aishi Kama mtu mwenye nywele fupi na Rangi nyeusi.
Culture za kila sehemu zinazingatia maumbile ya Wanajamii husika na hapo ndipo majukumu yanapotokea,
Mwanaume anaakili yake, mtazamo wake, umbile lake hivyo hupewa majukumu na jamii yake kulingana na jinsi alivyo.
Halikadhalika na Mwanamke.
Sasa inashangaza jitu linashindwa kuelewa mambo madogo Kama hayo.
Zingatia; kuna mambo ya ku-share watu wote dunia nzima, na yaku-share na jinsia zote lakini yapo mambo ambayo kila jamii inafanya kivyake halikadhalika na jinsia