STUNTER: Breezy Swagger Boy Wa Facebook

Aminia. Ila kwa watoto wa mjini kucheza mapicha kama hayo ndo zao. Mi nakumbuka moja nilicheza nipo kwenye train ya Tazara. Kitu Dar - Mbeya. Mwanao nimekata tiketi kajamba nani halafu ni mchongoma wa kutosha. Kajambanani hapakaliki.....full misele 2nd class na 1st class. Si ndo nikakutana na bonge la toto mitaa ya 1st class, halafu likanishobokea tu. Story 2tatu akaniuliza uko behewa gani.....kama kawa, sikutaka kujishusha. Nikamwambia nipo 2nd class. Hahahaaaa....picha linaanza demu anasema ''twende room kwako''. Duh!
 
Aminia. Ila kwa watoto wa mjini kucheza mapicha kama hayo ndo zao. Mi nakumbuka moja nilicheza nipo kwenye train ya Tazara. Kitu Dar - Mbeya. Mwanao nimekata tiketi kajamba nani halafu ni mchongoma wa kutosha. Kajambanani hapakaliki.....full misele 2nd class na 1st class. Si ndo nikakutana na bonge la toto mitaa ya 1st class, halafu likanishobokea tu. Story 2tatu akaniuliza uko behewa gani.....kama kawa, sikutaka kujishusha. Nikamwambia nipo 2nd class. Hahahaaaa....picha linaanza demu anasema ''twende room kwako''. Duh!
Hahahahah.... Hapo lazima utumie akili za kuzaliwa manake hamna tuitions za kufundisha kuescape misala kama hiyo
 
TUENDELEE NA KALE KASTORY KETU NILIVYOENDA KUMIT NA MREMBO WA FB RAHMA
MLIMAN CITY
Ilipoishia
Nilifika pale nikawasalimia Rahma na rafiki yake na
mimi nikakaa nikawa nashangaa tu na wenyewe
wakawa wananishangaa

Endelea...

Sikuelewa nianze vipi kuongea na Rahma sababu nilikuwa nimemdanganya kila kitu picha za
facebook hazikuwa zangu niliweka picha za rafiki
yangu handsome boy mwenye swaga wakati mimi
wakawaida tu sina swaga zozote sio handsome
nna lichogo kama ndizi, nilimdanganya mimi
wakishua naishi Masaki wakati nilikuwa mchoma mahindi naishi Manzese ila tu status zangu za
mashauzi za kujifia na zile picha zangu ndio maana
Rahma aliniamini fasta
,
Rahma alivyoona nimekaa pale siongei chochote
akaniuliza "we mkaka vipi mbona hatukuelewi
kuna mtu una shida naye hapa??? Nikajing'atang'ata pale nikamjibu "Ndio bby Rahma
mimi ndo BREEZY SWAGER BOY mpenzi wako
tuliyekutana facebook"
Kusikia vile Rahma na rafiki yake wote walistuka
akaniambia "We mkaka koma tena ishia hapo hapo
mimi Breezy wangu namjua hawezi kuwa mchafu mshamba kama wewe Breezy wangu mimi
handsome sana ana swaga kama mmarekani hebu
toka hapa wewe utakuwa umetumwa"
Nikainama chini kwa aibu nikajua mambo tayari
yameshaharibika nikamwambia "Naombeni
mnisikilize kwa makini jamani samahanini lakini mimi ndo yule BREEZY SWAGER BOY niliyekutongoza
facebook jina langu halisi naitwa ASWILE
MWAMPAGATWE zile picha nilizoweka facebook sio
zangu ni za rafiki yangu mimi naogopa kuweka
picha zangu sababu niliwahigi kuziweka mwanzo
nikawa kila msichana nikimtongoza anasema mimi sura ngumu nna chogo baya wakawa
wananiponda mimi sina swaga mshamba ndo
maana nikabadili jina nikatoa picha zangu
nikaweka za rafiki yangu na kiukweli mimi sikai
Masaki naishi Manzese niliamua tu kukudanganya
ili unikubali haraka mimi sio mtoto wakishua mimi nachoma Mahindi Manzese sokoni naomba
nisamehe kwa kukudanganya nilijua nikiongea
ukweli mrembo mzuri kama wewe lazima
ungenikataa hata usingekubali kuonana na mimi"
Rahma na rafiki yake walinisikiliza kwa makini
nilivyomaliza kuongea akaniambia "yani mimi siku zote hizo napoteza mda wangu kuchat nanunua
vocha nakupigia tunaongea mda mwingi napiga
picha nzuri natuma kumbe mtu mwenyewe ndo
wewe sasa kwanini uliamua kunidanganya
kwanini usiniambie ukweli niyajue maisha yako
halisi? sasa sikia we mpumbavu hebu ondoka hapa tayari umeshaniharibia siku mimi nimetoroka chuo
nimenunua mazawadi kibao najua naenda
kuonana na boyfriend wangu kumbe ndo nakuja
kuonana na wewe kituko hebu ondoka hapa nisije
nikakumwagia juice tena sasa hivi nitakuitia mwizi
na sitaki tena unipigie simu wala kunitumia message na facebook nakublock naenda
kukutangaza pumbavu mkubwa wewe unajifanya
fb una swaga misifa mingi kumbe picha sio zako
lione kule"
Nikaona Rahma ameanza kupiga makelele pale
hadi watu wengine wakaanza kusogea pale kujua nini kimetokea.
Nikasimama kwa aibu nikaanza kuondoka Rahma
na mwenzake wakaendelea kunicheka huku
wananitukana,
roho iliniuma sana
Nilipanda dala dala njia nzima nawaza hadi gari
likanipitiliza badala nishukie Manzese nikajikuta nipo magomeni nikaanza kurudi kwa mguu hadi
nyumbani nilijifungia chumbani nikaanza kujuta
bora tu ningemuambia ukweli Rahma kuliko
nilivyoongea uongo nikaumbuka bure
Nilichukua Tecno yangu nikaingia fb nikakuta
Rahma kaniblock kwa matusi aliyonitukana pale Mlimani nikawa naogopa hadi kupiga simu
nikaamua kuifunga account kabisa ili kukwepa
aibu iliyonikuta

Jamani kuweni wakweli masela wenzangu isije
ikawakuta aibu kama iliyonikuta mimi
 
Back
Top Bottom