Amateur
Member
- Apr 18, 2011
- 34
- 5
Naomba kuuliza mnisaidie kumshauri rafiki yangu ambaye ni ofcmate wangu. Yeye ana mume na wana mtoto mdogo kwa sasa wa miaka miwili ( huyu ni mtoto wao wa tatu). Toka alipoconceive huyu mtoto wa tatu mpaka leo mume wake hataki kufanya nae tendo la ndoa. Hii mimba ya 3 mume ndio alidai sana kwamba anataka mtoto wa kike maana walikuwa na boys tu, na kweli akapata mtoto wa kike. Anadai ana stress nyingi. Mke anafanya ku beg mpka sasa anadai ameacha ku beg maa anaona kama anadhalilishwa. Siku nyingine akiomba mume anakuwa mkali na anamnunia for months. Anasema bado wanalala kitanda kimoja but no sex! She is very desperate na hajui afanyeje na mume hataki kabisa mazungumzo. Naombeni ushauri maana alivyonieleza nikamwambia ngoja nilifikirie pia najua hana muda wakusoma jamiiforums ndio maana nalileta kwenu mnisaidie.