Mkuu hao watu ni janga la kitaifa.
Ni jumapili hii iliyopita muda wa saa 1 kasoro jioni nikiwa natoka City Centre kuelekea Kimara kulitokea kituko ambacho kilisababisha nimpe jibu moja baya sana askari wa traffic. Ilikuwa hivi:
Nilipofika pale nje ya Kiwanda cha Kibuku, jamaa wa Strabag wakiwa na lorry lao kubwa lenye matofali ya kuziba barabara, walikuwa wamepaki katikati ya barabara na mmoja wao akashuka akawa anaelekea madereva wote tupitie upande wa kulia (Ambao ndio unaopitisha magari yatokayo Kimara kwenda Mjini). Ikabidi tukubali na kuanza kubanana na magari yatokayo Kimara kwenye "road lane" moja.
Ghafla huku nyuma tena wale jamaa wa Strabag wakaifungua tena njia wakati huo sisi upande wakulia tumeshapigana pini, wa Kimara-Mjini hawaendi wala wa Mjini-Kimara hatuendi huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Akatokea Police Traffic mmoja akaanza kutukana madereva wanaotoka Mjini-Kimara na kudai wao ndiyo chanzo cha Msongamano huo.
Kwa kweli yale maneno aliyokuwa anatukanwa dereva aliyekuwa mbele yangu niliona yananihusu na mimi pia kwa kuwa tulikuwa wote zaidi ya magari 25. Ilibidi nifungue kioo ili kumuelimisha yule Polisi akawa mkali kama mbogo. Ilibidi na mimi nipandishe sauti kwa kumkosoa kikanuni na watu wengine wakaingilia kumsakama yule Polisi mpaka akasalimu amri.
Ndipo ikabidi asimamishe magari ya kutoka Kimara kwanza ili sisi wa kutoka mjini tugeuze tena kurudi nyuma mbele ya lango la kutokea UBT ili tuendelee na safari yetu kupitia njia ya kawaida pembezoni mwa kiwanda cha Kibuku. Yaani kutoka eneo la Kiwanda cha Kibuku mpaka nafika Ubungo mataa nilitumia muda usiopungua dakika 50.
Kwa kweli niliboreka sana na hiyo njia mpaka nikaapa kutoitumia tena mpaka hapo ujenzi utakapokamilika.