Strabag ni janga jingine

Strabag ni janga jingine

Jamani tusiwe wepesi wa kulaumu hii kampuni iko njema sana. Kumwaga zege hadi likauke sio kazi ya siku moja wala mbili na ukumbuke kabla ya kuweka hilo zege kuna Landscaping kubwa sana imefanyika.

Nakumbuka ujenzi wa Sam Nujoma ulilalamikiwa sana huku walalamikaji wakizisifia kampuni zilizokua zinajenga Shekilango na Kilwa roads. Leo hii nenda kajionee tofauti ya roads hizo.
Nadhani tuweni nasubiri sometimes

Naam nyie ndiyo watu mnaotakiwa Tz, siyo wabwabwajaji.
 
kwa wageni wa dsm hii ni kampuni inayotengeneza barabara ya morogoro kwa ajili ya magari yaendayo kasi. Kwa mtazamo wangu kampuni hii imeonyesha udhaifu sana katika kufanya kazi, kiasi kuna wakati najiuliza iliwezaje kupata hii kazi jamani. Fikiria, wamechimbachimba kwa ustadi mkubwa barabara toka kimara, ubungo, manzese hadi town center, sasa ishu ngumu ni kuijenga hiyo barabara! Wanajenga kwa mwendo wa konokono kiasi cha kuwapa shida sana watumiaji wa barabara.
hapo ubungo stend ndo balaa tupu hakuna utaratibu mzuri haielewi hata gari zinapitaje.binafsi nimeshashuhudia kuna makampuni yanafanya kazi katika eneo finyu mfano unakuta barabara upande mmoja ina shimo/bonde upande mwingine kuna mlima lakini wajomba wanapiga kazi inaenda vema na magari yanapita vizuri lakini hawa jamaa wamepewa sehemu kubwa ya kufanyia kazi lakini bure kabisa!!!!
mburula wewe
 
Jamani mwenye picha za maendeleo ya huo mradi atupie basi na mwenzenu nioshe macho,maana sijaja dar siku nyingi sana !!
 
Swali hivi kwenye makutano ya barabara itabidi hayo mabasi yapite kwanza ndo na sie wengine tupite? Kwanini wasingeyapitisha juu ili kuzuia msongamano?
 
kwa wageni wa dsm hii ni kampuni inayotengeneza barabara ya morogoro kwa ajili ya magari yaendayo kasi. Kwa mtazamo wangu kampuni hii imeonyesha udhaifu sana katika kufanya kazi, kiasi kuna wakati najiuliza iliwezaje kupata hii kazi jamani. Fikiria, wamechimbachimba kwa ustadi mkubwa barabara toka kimara, ubungo, manzese hadi town center, sasa ishu ngumu ni kuijenga hiyo barabara! Wanajenga kwa mwendo wa konokono kiasi cha kuwapa shida sana watumiaji wa barabara.
hapo ubungo stend ndo balaa tupu hakuna utaratibu mzuri haielewi hata gari zinapitaje.binafsi nimeshashuhudia kuna makampuni yanafanya kazi katika eneo finyu mfano unakuta barabara upande mmoja ina shimo/bonde upande mwingine kuna mlima lakini wajomba wanapiga kazi inaenda vema na magari yanapita vizuri lakini hawa jamaa wamepewa sehemu kubwa ya kufanyia kazi lakini bure kabisa!!!!

Mkuu tatizo siyo la mkandarasi Strabag , bali tatizo lilianzia hukohuko serikalini.

Msimamizi mkuu wa mradi huyo alikuwa anaitwa Ndg Takule, huyu jamaa ni mburula kwei kweli!
Hata waziri wa ujenzi Ndg Magufuli alilalamika mbele ya Rais. alipokuwa akifungua kituo cha mabasi Mbezi Luis, kuwa jamaa hafai, hafai kabisa!
Na kweli akaondolewa kutoka mradi huu wa mabasi yaendayo kasi na utayarishaji miundo mbinu yake.

Madhambi ambayo hayajaelezwa ni kwamba usanifu wa miundombinu haukukamilika, na huku tayari wameshaweka mkandarasi, kwa mantiki hiyo mkandarsi hana kazi ya kufanya bila kuwepo michoro ya kazi.

Kuna sehemu hata makubaliano ya kufidia watu walio katika sehemu ambazo njia au barabara ya mabasi itapita wala haija fanyika.

Wakati mwingine ni lazima watu wanyongwe ili wafanye kazi kwa ufanisi!!!
 
Ni uzoefu wa watanzania kulalamika katika kila jambo ingawa baadae litakuwa na manufaa kwa kila mmoja wetu: kuna baadhi ya mambo ya kujiuliza je ingelikuwa kwamba hii barabara ujenzi wake haujaanza mpaka leo na kubaki kama ahadi si tungelalama na kusema serikali haitekelezi kabisa ahadi na miradi iliyopo?barabara kiukweli kwa leo imekuwa tabu kupitika kwa sababu ambazo kama wewe unakaa Dar Es Salaam utakuwa umeshuhudia mwenyewe jinsi mvua zilivyokuwa zinanyesha kwa muda mrefu kwa hiyo ndugu mdau kuwa na subira kwani kila maendeleo huja na changamoto zake
Wewe tatizo lako ni exposure! Wewe ni kati ya wale watu wanaofikiri hakuna godoro zuri kuliko analolalia baba yake.. just because hawajatembea na kuona. Ni kweli katika ujengaji wa barabara kuna karaha, lakini karaha anayozungumzia mwanzisha thread ni zaidi ya karaha... ni uzembe ni uongozi mbaya ni kila aina ya ushetani. Nimetembea na kuishi sehemu nyingine za dunia lakini sijawahi kuona ujenzi usiojali watumia barabara kama huu. Naona wajenzi wanakwepa kuingia gharama zinazoendana na kupangilia mambo yaende smoothly. Na haya madodoki yetu ya ccm kama kawaida yanafukuzana kuibia wanyongo na hayaoni kadhia yoyote!
 
Hawa jamaa hata mitaro hawajaweka!
Matokeo yake wanapeleka mafuriko katika nyumba zilizo jirani na barabara!
Kuna duka moja la nafaka limefirisika kutokana na ujinga wa hao jamaa.
Kweli kabisa Strabag ni choo kingine cha kike.
 
Kuna kitu kinaitwa capacity and level of service(los) kama barabara ilikuwa na njia mbili na sasa ni moja unategemea nn.pili kwenye makutano pakoje?mazigira ya mradi ndio yalivyo
 
Ni muda muafaka kujitoa humu jamii forum kuna watu wanaolalamika wavivu wajinga.....nisije nikaingia katika kundi hili hawa ni wajinga toka darasani ....foools

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Ni muda muafaka kujitoa humu jamii forum kuna watu wanaolalamika wavivu wajinga.....nisije nikaingia katika kundi hili hawa ni wajinga toka darasani ....foools

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

jamii forums haiboi.mkuu nimecheka mpaka basi.!
 
kiukweli pamoja na kusema kazi ya barabara ina itifaki zake lakini nina taarifa za jikoni kabisa kwamba jamaa amechelewesha kazi na WB wameshaliona hilo

  1. Alikwenda likizo December kinyume na mkataba
  2. alitakiwa afanye kazi usiku na mchana lakini wahandisi wamegoma wakaendekeze pombe na mademu ni karibuni tu baada ya review ndio kuna maeneo amenaza usiku
  3. Hiyo 2015 ni kwa phase zote mbili, hii ya Morogoro ni phase 1 tu
Nakubaliana na ukweli kwamba speed si kipimo lakini tizama aina ya mifereji anayoweka na tizama kule ambako ameshaweka lami, tayari mahandaki yameanza .................
 
mkuu mimi bado ninaimani na utendaji kazi wa kampuni ya STRABAG.naomba tutulie wapige kazi.sina mashaka na kampunii hii,labda ubabaishaji wauanzie hapa Tanzania.nilikua nafatilia report flani hiv,katika kampuni za ujenzi bora duniani,STRABAG ni kampuni ya 6 kati ya 10 kwa ubora wa kiutendaji dunian.
 
Mshazoea wachina wangekua washamaliza kisha baada ya miezi sita mnakoma kuringa
kumbuka jamaa hawajengi barabara tu.wanatengeneza pia miundombinu ya mifereji kupitisja majitaka ndani kwa ndani.bila kusahau wanaboresha line za mawasiliano.
Na juzi nimepita kuelekea Mikoa ya Kaskazini wamefumua njia kuanzia korogwe mpaka Mwanga,Na shughuli wanayofanya ni ya uhakika sana.Jamaa wako vizuri sana
 
Madai ya mleta thread ni sahihi kwa upande fulani hasa ukizingatia kazi ya ujenzi wa barabara ni kazi ya wazi kwa maana inafanywa wakati watu wanapita na kuona kinachofanyika.

Kiukweli kinachoonekana kwenye barabara iliyozungumizwa ni jamaa kukosa mpangilio mzuri wa jinsi ya kufanya kazi yao. Wamekuwa wanachimba sehemu moja na kuhamia sehemu nyingine kabla hawajarekebisha sehemu waliyochimba awali. Wanasahau kama barabara bado inatumika.
 
watanzania kwa kulalamika hatuwezekani.....Sishangai ndivyo tulivyo.Ila kazi ni nzuri na wala speed yao si mbaya ni taratibu za ujenzi tu zinafuatwa.
 
Mkuu hao watu ni janga la kitaifa.

Ni jumapili hii iliyopita muda wa saa 1 kasoro jioni nikiwa natoka City Centre kuelekea Kimara kulitokea kituko ambacho kilisababisha nimpe jibu moja baya sana askari wa traffic. Ilikuwa hivi:

Nilipofika pale nje ya Kiwanda cha Kibuku, jamaa wa Strabag wakiwa na lorry lao kubwa lenye matofali ya kuziba barabara, walikuwa wamepaki katikati ya barabara na mmoja wao akashuka akawa anaelekea madereva wote tupitie upande wa kulia (Ambao ndio unaopitisha magari yatokayo Kimara kwenda Mjini). Ikabidi tukubali na kuanza kubanana na magari yatokayo Kimara kwenye "road lane" moja.

Ghafla huku nyuma tena wale jamaa wa Strabag wakaifungua tena njia wakati huo sisi upande wakulia tumeshapigana pini, wa Kimara-Mjini hawaendi wala wa Mjini-Kimara hatuendi huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Akatokea Police Traffic mmoja akaanza kutukana madereva wanaotoka Mjini-Kimara na kudai wao ndiyo chanzo cha Msongamano huo.

Kwa kweli yale maneno aliyokuwa anatukanwa dereva aliyekuwa mbele yangu niliona yananihusu na mimi pia kwa kuwa tulikuwa wote zaidi ya magari 25. Ilibidi nifungue kioo ili kumuelimisha yule Polisi akawa mkali kama mbogo. Ilibidi na mimi nipandishe sauti kwa kumkosoa kikanuni na watu wengine wakaingilia kumsakama yule Polisi mpaka akasalimu amri.

Ndipo ikabidi asimamishe magari ya kutoka Kimara kwanza ili sisi wa kutoka mjini tugeuze tena kurudi nyuma mbele ya lango la kutokea UBT ili tuendelee na safari yetu kupitia njia ya kawaida pembezoni mwa kiwanda cha Kibuku. Yaani kutoka eneo la Kiwanda cha Kibuku mpaka nafika Ubungo mataa nilitumia muda usiopungua dakika 50.

Kwa kweli niliboreka sana na hiyo njia mpaka nikaapa kutoitumia tena mpaka hapo ujenzi utakapokamilika.
 
mkuu mimi bado ninaimani na utendaji kazi wa kampuni ya STRABAG.naomba tutulie wapige kazi.sina mashaka na kampunii hii,labda ubabaishaji wauanzie hapa Tanzania.nilikua nafatilia report flani hiv,katika kampuni za ujenzi bora duniani,STRABAG ni kampuni ya 6 kati ya 10 kwa ubora wa kiutendaji dunian.
Kwani mbona wachina wanaosifika kwa utengenezaji wa bidhaa bora kabisa za kiteknolojia kwenye soko la Ulaya, ndiyo wanaoongoza kwa uingizaji wa bidhaa dhaifu Afrika hususani Tanzania?
 
Ni uzoefu wa watanzania kulalamika katika kila jambo ingawa baadae litakuwa na manufaa kwa kila mmoja wetu: kuna baadhi ya mambo ya kujiuliza je ingelikuwa kwamba hii barabara ujenzi wake haujaanza mpaka leo na kubaki kama ahadi si tungelalama na kusema serikali haitekelezi kabisa ahadi na miradi iliyopo?barabara kiukweli kwa leo imekuwa tabu kupitika kwa sababu ambazo kama wewe unakaa Dar Es Salaam utakuwa umeshuhudia mwenyewe jinsi mvua zilivyokuwa zinanyesha kwa muda mrefu kwa hiyo ndugu mdau kuwa na subira kwani kila maendeleo huja na changamoto zake

Kama STRABAG hawafai pendekeza kampuni unayoona inafaa ipewe kazi.

Ujenzi wa barabaara sio kama production line ya vyupa vya bia pale karume...ukiweka tu vinafika end point.

Jamani tusiwe wepesi wa kulaumu hii kampuni iko njema sana. Kumwaga zege hadi likauke sio kazi ya siku moja wala mbili na ukumbuke kabla ya kuweka hilo zege kuna Landscaping kubwa sana imefanyika.

Nakumbuka ujenzi wa Sam Nujoma ulilalamikiwa sana huku walalamikaji wakizisifia kampuni zilizokua zinajenga Shekilango na Kilwa roads. Leo hii nenda kajionee tofauti ya roads hizo.
Nadhani tuweni nasubiri sometimes

Unataka waripue fasta, halafu uanze tena kulalama

Strabag wanafanya kazi kwa juhudi sana, tena wanajitahid japo mazinngira ya kazi ni magumu, ujenzi wa mjin tena ni kuboresha barabara kwa kuijenga upya ni mradi mkubwa na unahitaji muda, tuwavumilie tu watamaliza ndan ya muda wa mkataba wao.


Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums

Mshazoea wachina wangekua washamaliza kisha baada ya miezi sita mnakoma kuringa
kumbuka jamaa hawajengi barabara tu.wanatengeneza pia miundombinu ya mifereji kupitisja majitaka ndani kwa ndani.bila kusahau wanaboresha line za mawasiliano.

Afadhali umenisaidia kumpa jibu linalo jitosheleza.Wa Tz tupunguze kupiga domo. Mnataka walipue kazi halafu mje na hoja ya kusema CCM wameiba hela kwa kutujengea barabara mbovu? Aaagh nchi hii labda aje YESU kututawala.

Mleta uzi kazoea kazi za wachina.Faster with low standard but full decorations.
Nadhani watu wengi humu ndani hatuchambui vizuri nini mleta mada ameleta hapa. Hakua mtu aliyehoji uwezo wa hawa jamaa bali uzembe katika utendaji kazi upo dhahiri.

Kwa mtu yeyote mwenye uelewa wa kandarasi za barabara, atakuwa anaelewa kwamba wakati wa ujenzi utatakiwa kuchonga njia ya muda ya watumiaji wengine au at least diversion yenye maelekezo yanayoonekana kutokea mbali wakati utakapokuwa unashughulikia kipande cha barabara fulani.

Kwa hawa jamaa hata sehemu wanapochimba ni sehemu chache sana utakuta alama za tahadhari, kila sehemu wamechimba bila sababu ya msingi. KERO MPAKA BASI
 
STRABAG ni wazuri kiufundi sana, ila nasikia wananyanyasa sana watumishi wa kitanzania. Mishahara ni kidogo sana na wanalipa mishahara kwa mikataba mifupi kuondokana na social security kwa watumishi wake. Nilitegemea kwa miezi 36 wanafanya kazi basi wangewapa baadhi hata ya watumishi mkataba wa kuweza kumplipa pension lakini wapi? Mshahara wao ni mdogo pia. Tu be frank wana zile tabia za Kijerumani za kudharau sana ngozi nyeusi kwa kila eneo.
 
Back
Top Bottom