Story behind your date of birth

Story behind your date of birth

Tarehe 01/08
TAREHE 01/08 NI NYOTA YAKO NI
[TABLE="class: ecxyiv1670654587contentpaneopen"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]

NYOTA YA SIMBA (LEO)


  • Hii ni nyota ya tano katika mlolongo wa nyota kumi na mbili.
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21Julai na 21 Agosti.
  • Sayari yao ni Jua (Sun).
  • Siku yao ya bahati ni Jumapili.
  • Namba yao ya bahati ni 1 na 4.
  • Rangi yao ya bahati ni Njano au rangi ya Dhahabu.
  • Asili ya nyota yao ni moto.

KIPAJI CHA SIMBA (INSPIRED):

Wenye nyota hii wana kipaji cha ufunuo wa kiungu , wana uwezo wa kuvumbua mambo ambayo yanaweza kuwaletea fedha pamoja na kwamba hazikai.
Wanauwezo vilevile wa kuponya kwa kutumia mikono yao kuponya watu na wanakipaji cha asili cha uongozi.

TABIA ZA SIMBA:

Watu wenye nyota hii ya Simba ni watu wanaopenda ufahari mkubwa na kutukuzwa. Ni watu wanaopenda kutumia na wanataka waonekane na wanuwezo wa kuvumbua mambo amabyo watu wengine hawajui na wanapenda sana heshima.
ni wakarimu lakini ni wajeuri na wanapenda kuonea watu. Wana hisia kali, ni wakali na wanakiburi.

TABIA YA SIMBA KATIKA MAPENZI:

Tabia ya Simba ni kujitanua, Ukarimu na ulezi ikichanganyika na ujeuri na kujionyesha, huwaharibu wale wanao wapenda.
Furaha haina mpaka katika mapenzi ya simba, mioyo yao mikubwa na hisia zao nzito hutokeza dhahiri wanapompenda mtu.
Baada ya hapo ndipo sura kamili ya Simba hujitokeza. Wao wanathamini sana mapenzi na juu ya jambo lolote, na wanaweza kuwa waaminifu sana na wakati mwingine huwaabudu wapenzi wao.
Wanapenda kujishughulisha sana na mambao ya mapenzi lakini mambo yakiharibika basi inakua vigumu sana kuyatengeneza.
Tatizo lao kubwa ni wao kujisahau kwamba ni upande mmoja wa penzi na wanajifanya wao ndio viongozi.
Kwa nje wanaonekana ni wenye kujiamini katika mapenzi lakini kwa ndani wanaweza kuwa wanaumia lakini hawawezi kukubali. Hata hivyo mara nyingi hutegemea kupata hisia kama walizonazo wao kutoka kwa wapenzi wao.

MATATIZO YA KIAFYA:

Nyota hii inatawala moyo, sehemu ya juu ya mgongo na bandama.
Vilevile inatawala uti wa mgongo na mshipa mkubwa wa damu.
Matatizo yao makubwa kiafya yanahusiana na maradhi ya kuumwa sehemu ya juu ya mgongo.
Maradhi yanayotokana na damu kama shinikizo la damu la juu na chini na maradhi ya moyo.
Vilevile wanaugua maradhi ya homa ya uti wa mgongo.
{mospagebreak}

KAZI ZA WENYE NYOTA YA SIMBA:

Wenye nyota hii wanatakiwa wafanye kazi zifuatazo; kazi za usimamizi, kama katika kampuni yake binafsi au katika mashirika au biashara, kazi za michezo au uongozi wa michezo.
Wanatakiwa wafanye kazi za usonara au kazi za kuuza au kutengeneza mavazi ya mitindo.
Vilevile wanatakiwa wafanye kazi za uigizaji au uendeshaji sinema au kazi zozote zinazohusika na masuala ya vijana.
Kazi yao nyingine ni ya ualimu katika taasisi, shule au vyuo vya ualimu.

FAMILIA ZA SIMBA:

Kwa asili Simba ni Mfalme na mamlaka yake yamezungukwa na hisia za kifalme. Wazazi wa simba huwa wana mila ya kuwapangia watoto wao namna watakavyoishi kwa sababu wanajivunia sana familia zao.
Wazazi wa Simba wanajiona kwamba wana nafasi kubwa katika dunia ambayo inawataka wajionyeshe kwa watu ubora. Pamoja na kwamba wenye nyota hii hupenda kuzunguka na watoto wao (na wao wenyewe wakati mwingine wana tabia ya utoto) hawakubali kupoteza heshima zao wakati wanafanya hivyo.
Wenye nyota hii ni wachangamfu, wenye moyo wa kupenda na wanapenda raha, pamoja na ukali wao wanaweza kuwa wepesi kwa watoto wao.
Watu wa simba kwa uhakika wanaona raha kuwa wazazi lakini wanatakiwa wawe makini kutowaharibu watoto wao kwa zawadi nyingi na maisha ya raha.
Simba wana uhakika na nafasi yao katika jamii kwamba wao ni viongozi hivyo watoto wao huwa wanapenda kujionyesha na wanategemea wawe wanaonekana kwa watu muda wote.

MADINI YA SIMBA:

(AMBER); Jiwe hili lenye rangi ya njano iliyochanganyika na kahawia linasemekana lina uwezo wa kumpa ukakamavu na ari ya uongozi kwa anayelivaa, vilevile linamwepusha mvaaji na maradhi ya kichwa.

UHUSIANO WA KIMAPENZI

(SIMBA NA NDOO):
Tabia ya Simba ya kutopenda kudhibitiwa au kudhibiti watu inakuwa ni faraja kubwa kwa wenye nyota ya ndoo ambao wanapenda uhuru na kufanya mambo yao bila kuingiliwa.


VYAKULA VYA SIMBA:

Wenye nyota ya simba wanatakiwa wale vyakula au matunda yafuatayo ambayo yanatawaliwa na nyota yao.
Vyakula hivyo ni machungwa, maboga, vitu vichachu kama ndimu au malimao na wapende sana kula nyama za ng'ombe, mbuzi na kondoo.


NCHI ZA SIMBA:

Watu wa nyota ya simba wanatakiwa wakaishi au watembelee nchi zifuatazo ambazo zinatawaliwa na nyota yao.
Nchi hizo ni Italia na Morocco na miji ni Bombay (India) na Roma (Italia)


RANGI ZA SIMBA:

Watu wote wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake nyumba zao au magari yao rangi zilizochangamka na zenye kuonyesha utajiri
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Ukiwa na Swali au Tatizo lolote usikose kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 
TAREHE 01/08 NI NYOTA YAKO NI
[TABLE="class: ecxyiv1670654587contentpaneopen"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]

NYOTA YA SIMBA (LEO)


  • Hii ni nyota ya tano katika mlolongo wa nyota kumi na mbili.
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21Julai na 21 Agosti.
  • Sayari yao ni Jua (Sun).
  • Siku yao ya bahati ni Jumapili.
  • Namba yao ya bahati ni 1 na 4.
  • Rangi yao ya bahati ni Njano au rangi ya Dhahabu.
  • Asili ya nyota yao ni moto.

KIPAJI CHA SIMBA (INSPIRED):

Wenye nyota hii wana kipaji cha ufunuo wa kiungu , wana uwezo wa kuvumbua mambo ambayo yanaweza kuwaletea fedha pamoja na kwamba hazikai.
Wanauwezo vilevile wa kuponya kwa kutumia mikono yao kuponya watu na wanakipaji cha asili cha uongozi.

TABIA ZA SIMBA:

Watu wenye nyota hii ya Simba ni watu wanaopenda ufahari mkubwa na kutukuzwa. Ni watu wanaopenda kutumia na wanataka waonekane na wanuwezo wa kuvumbua mambo amabyo watu wengine hawajui na wanapenda sana heshima.
ni wakarimu lakini ni wajeuri na wanapenda kuonea watu. Wana hisia kali, ni wakali na wanakiburi.

TABIA YA SIMBA KATIKA MAPENZI:

Tabia ya Simba ni kujitanua, Ukarimu na ulezi ikichanganyika na ujeuri na kujionyesha, huwaharibu wale wanao wapenda.
Furaha haina mpaka katika mapenzi ya simba, mioyo yao mikubwa na hisia zao nzito hutokeza dhahiri wanapompenda mtu.
Baada ya hapo ndipo sura kamili ya Simba hujitokeza. Wao wanathamini sana mapenzi na juu ya jambo lolote, na wanaweza kuwa waaminifu sana na wakati mwingine huwaabudu wapenzi wao.
Wanapenda kujishughulisha sana na mambao ya mapenzi lakini mambo yakiharibika basi inakua vigumu sana kuyatengeneza.
Tatizo lao kubwa ni wao kujisahau kwamba ni upande mmoja wa penzi na wanajifanya wao ndio viongozi.
Kwa nje wanaonekana ni wenye kujiamini katika mapenzi lakini kwa ndani wanaweza kuwa wanaumia lakini hawawezi kukubali. Hata hivyo mara nyingi hutegemea kupata hisia kama walizonazo wao kutoka kwa wapenzi wao.

MATATIZO YA KIAFYA:

Nyota hii inatawala moyo, sehemu ya juu ya mgongo na bandama.
Vilevile inatawala uti wa mgongo na mshipa mkubwa wa damu.
Matatizo yao makubwa kiafya yanahusiana na maradhi ya kuumwa sehemu ya juu ya mgongo.
Maradhi yanayotokana na damu kama shinikizo la damu la juu na chini na maradhi ya moyo.
Vilevile wanaugua maradhi ya homa ya uti wa mgongo.
{mospagebreak}

KAZI ZA WENYE NYOTA YA SIMBA:

Wenye nyota hii wanatakiwa wafanye kazi zifuatazo; kazi za usimamizi, kama katika kampuni yake binafsi au katika mashirika au biashara, kazi za michezo au uongozi wa michezo.
Wanatakiwa wafanye kazi za usonara au kazi za kuuza au kutengeneza mavazi ya mitindo.
Vilevile wanatakiwa wafanye kazi za uigizaji au uendeshaji sinema au kazi zozote zinazohusika na masuala ya vijana.
Kazi yao nyingine ni ya ualimu katika taasisi, shule au vyuo vya ualimu.

FAMILIA ZA SIMBA:

Kwa asili Simba ni Mfalme na mamlaka yake yamezungukwa na hisia za kifalme. Wazazi wa simba huwa wana mila ya kuwapangia watoto wao namna watakavyoishi kwa sababu wanajivunia sana familia zao.
Wazazi wa Simba wanajiona kwamba wana nafasi kubwa katika dunia ambayo inawataka wajionyeshe kwa watu ubora. Pamoja na kwamba wenye nyota hii hupenda kuzunguka na watoto wao (na wao wenyewe wakati mwingine wana tabia ya utoto) hawakubali kupoteza heshima zao wakati wanafanya hivyo.
Wenye nyota hii ni wachangamfu, wenye moyo wa kupenda na wanapenda raha, pamoja na ukali wao wanaweza kuwa wepesi kwa watoto wao.
Watu wa simba kwa uhakika wanaona raha kuwa wazazi lakini wanatakiwa wawe makini kutowaharibu watoto wao kwa zawadi nyingi na maisha ya raha.
Simba wana uhakika na nafasi yao katika jamii kwamba wao ni viongozi hivyo watoto wao huwa wanapenda kujionyesha na wanategemea wawe wanaonekana kwa watu muda wote.

MADINI YA SIMBA:

(AMBER); Jiwe hili lenye rangi ya njano iliyochanganyika na kahawia linasemekana lina uwezo wa kumpa ukakamavu na ari ya uongozi kwa anayelivaa, vilevile linamwepusha mvaaji na maradhi ya kichwa.

UHUSIANO WA KIMAPENZI

(SIMBA NA NDOO):
Tabia ya Simba ya kutopenda kudhibitiwa au kudhibiti watu inakuwa ni faraja kubwa kwa wenye nyota ya ndoo ambao wanapenda uhuru na kufanya mambo yao bila kuingiliwa.


VYAKULA VYA SIMBA:

Wenye nyota ya simba wanatakiwa wale vyakula au matunda yafuatayo ambayo yanatawaliwa na nyota yao.
Vyakula hivyo ni machungwa, maboga, vitu vichachu kama ndimu au malimao na wapende sana kula nyama za ng'ombe, mbuzi na kondoo.


NCHI ZA SIMBA:

Watu wa nyota ya simba wanatakiwa wakaishi au watembelee nchi zifuatazo ambazo zinatawaliwa na nyota yao.
Nchi hizo ni Italia na Morocco na miji ni Bombay (India) na Roma (Italia)


RANGI ZA SIMBA:

Watu wote wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake nyumba zao au magari yao rangi zilizochangamka na zenye kuonyesha utajiri
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Ukiwa na Swali au Tatizo lolote usikose kunitafuta kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
Shukrani mkuu, kwa ufumbuzi huu. Ila kuna kitu kinaninipa ukakasi kidogo hapa katika tafiti yangu ndogo, hivi katita haya mawe ya nyota yanatakiwa yawe ya aina ngapi. Maana we umeniambia ni Amber lakini pia nimeona na Rubby pia linahusika je ni lipi linafaa zaidi au ni bora zaidi, na kwa nini?
 
Shukrani mkuu, kwa ufumbuzi huu. Ila kuna kitu kinaninipa ukakasi kidogo hapa katika tafiti yangu ndogo, hivi katita haya mawe ya nyota yanatakiwa yawe ya aina ngapi. Maana we umeniambia ni Amber lakini pia nimeona na Rubby pia linahusika je ni lipi linafaa zaidi au ni bora zaidi, na kwa nini?
Unaweza kuwa na pete 2 tofauti moja ikiwa na jiwe la Ambar na moja ikiwana jiwe la ruby huruhusiwi kuvaa hizo pete mpaka nizfanyie mimi Dua na maombi maalumu . ukiwa ni mwanamke unaweza kuw aan pete ya dhahabu ukaweka jiwe la Amber au unaweza kuw ana pete ya fedha ukaweka jiwe la Ruby ndio hivyo. Mkuu denoo49
 
Last edited by a moderator:
Unaweza kuwa na pete 2 tofauti moja ikiwa na jiwe la Ambar na moja ikiwana jiwe la ruby huruhusiwi kuvaa hizo pete mpaka nizfanyie mimi Dua na maombi maalumu . ukiwa ni mwanamke unaweza kuw aan pete ya dhahabu ukaweka jiwe la Amber au unaweza kuw ana pete ya fedha ukaweka jiwe la Ruby ndio hivyo. Mkuu denoo49
Eeeh, mkuu kumbe mpaka maombi!!?
Na haiwezikanj Pete hiyo hiyo moja ikawa na mawe yote.?

Nanaomba msaada tena, wanaposema asili yao nyota hii ni moto wanakua wanamaanisha nini?
 
Last edited by a moderator:
Eeeh, mkuu kumbe mpaka maombi!!?
Na haiwezikanj Pete hiyo hiyo moja ikawa na mawe yote.?

Nanaomba msaada tena, wanaposema asili yao nyota hii ni moto wanakua wanamaanisha nini?
Unakwenda kwa sonara kutengeneza. Hizo Pete huwezi kuzipata kiurahisi Mkuu denoo49 Sio Pete za kawaida tu jaribu kwa Sonara kama utaweza kuzipata zilizokuwa teyari kisha uje unipe feedback.
 
Last edited by a moderator:
Unakwenda kwa sonara kutengeneza. Hizo Pete huwezi kuzipata kiurahisi Mkuu denoo49 Sio Pete za kawaida tu jaribu kwa Sonara kama utaweza kuzipata zilizokuwa teyari kisha uje unipe feedback.

Sawa mkuu, nimekuelewa. Nitakutafuta "chemba" kwa mengi zaidi. Ila maswali yangu haya ya mwisho naona kama umeyajibu kwa haraka au juu mno.
 
Last edited by a moderator:
Sawa mkuu, nimekuelewa. Nitakutafuta "chemba" kwa mengi zaidi. Ila maswali yangu haya ya mwisho naona kama umeyajibu kwa haraka au juu mno.
Hizo Pete sio pete za Mchezo au kila mtu anaweza kuwa nayo ni Pete za Spirit sio pete za kluzifanyia mchezo ndugu. Jaribu kwenda kwa Masonarakaulize kama utaweza kuzipata sio rahis kama unavyofikiria wewe@denoo49
 
KWA HIYO TAREHE ULIYOZALIWA UTAKUWA NA NYOTA YA NG'OMBE
(TAURUS)



Hii ni nyota ya pili katika mlolongo wa nyota 12.

Wenye nyota hii ni wale ambao wamezaliwa kati ya tarehe 21 April na May 20 ya mwaka wowote.

  • Sayari yao ni Venus (Zuhura).
  • Siku yao ya bahati ni Ijumaa.
  • Namba yao ya bahati ni 6.
  • Rangi yao ya bahati ni kijani.
  • Asili ya nyota yao ni Udongo.

KIPAJI CHA NG'OMBE

(BODY-CENTERED)
Wenye nyota hii wana kipaji kikubwa kilicho ndani ya mwili wao ambacho ni pamoja na kuelewa mambo kimbele, hesabu, kuponya kwa kutumia mikono na kwa kumwagia mtu maji.

TABIA YA NG'OMBE:

Wenye nyota hii ni watu wanaopenda kujishughulisha katika shughuli nyingi. Ni watu wakarimu na wanaopenda kusaidia watu, na wana tabia ya uvumilivu na subira katika jambo lolote wanalolifanya.
Ni watu wenye malengo na wenye msimamo thabiti, wasiopenda kupindishwa na wana tabia ya ubishi na ukaidi hasa katika jambo lao wanalolitaka.

TABIA YA NG'OMBE KATIKA MAPENZI:

Wenye nyota hii ni waaminifu sana katika mapenzi na wanaohitaji ulinzi katika mapenzi na njia au mwenendo unaoeleweka.
Pamoja na kwamba asili yao ni udongo, wanaweza kuwa ni wenye mahaba na mapenzi makubwa kwa wapenzi wao.
Uhakika wa mapenzi ndio jambo kubwa ambalo wenye nyota hii huangalia kwanza na baadae Penzi hilo liwe lenye hisia na mpangilio.
Pamoja na hisia kali walizonazo, wao ni watu imara na wasiobadilika hivyo kuwafanya watu wenye shauku kutovutiwa nao.
Uaminifu ni jambo la pili ambalo wenye nyota hii wanalo hivyo kuwafanya wao wawe watu wenye kuaminika na hiyo inasababisha wawe wenye wivu kupindukia.
Wanachotakiwa kufanya ni kujitahidi kuwapa nafasi wapenzi wao la sivyo watajikuta wako peke yao. Ndoa kwao ndio uamuzi mzuri kuliko kuishi na wapenzi. Tabia yao ni ya kudumisha jambo fulani wanaloliamini au walilolianzisha na hawapendi kubadilishwa.
{mospagebreak}

MATATIZO YA KIAFYA:

Nyota hii inatawala shingo, koo, koromeo, kidevu na sehemu ya chini ya taya.
Kwa asili wenye nyota hii ni watu wabishi na wenye kufanya mambo kwa upole na wagumu kubadilika.
Wanapenda sana vyakula vitamu na vyenye mafuta na huwezi kuwabadilisha katika hilo na wengi wao wanakuwa wanene kupita kiasi na inakuwa ni vigumu sana kuwashawishi kuamka na kufanya mazoezi ya mwili.
Tatizo lingine ni kufanya kazi kupita kiasi ambalo linawafanya wapate matatizo ya mvutano na misuli hasa katika sehemu zilizotajwa. wenye nyota hii wanatakiwa wajihadhari na mpangilio wao wa chakula na wafanye mazoezi kwa wingi.

KAZI ZA WENYE NYOTA YA NG'OMBE:

Wenye nyota hii wana falsafa ifuatayo kulingana na kazi; "panda mbegu iote, mti uote halafu ule matunda". Ni watu ambao wanafuata mpangilio wa kikazi na wanaopenda kujituma na kujishughulisha. Wengi wenye nyota hii ni wafanyakazi wazuri na wanapenda wapewe muda kujenga vipaji na utaalamu wao wa kazi.
Kazi zao zinakuwa kazi za muziki, kazi zinazohusiana na chakula, hoteli, migahawa, kazi za ujenzi, kazi za mashamba, kazi za uhasibu, na kazi za sanaa hasa uchoraji au uchongaji vinyago.

FAMILIA ZA NG'OMBE:

Wazazi wa familia za Ng'ombe ni watu wenye msimamo, wakutegemewa na wanaothamini familia zao, na wako tayari kugombana na mtu yeyote kwa ajili ya watoto wao.
Ni wazazi wanaopenda kufuata mambo ya kizamani au ya asili hasa katika masuala ya nidhamu. wanapenda sana kuheshimiwa na watoto wao na huwashawishi au kuwashauri wawe huru.
Ni wazazi wanaotegemea watoto wao wafuate nyayo zao hasa katika biashara au kazi wanazozifanya, hivyo watoto wa wazazi Ng'ombe wanakuwa na muda mdogo wa kufikiria mambo mapya.
Ni wazazi ambao hufanya kazi kwa bidii kuhakikisha watoto wao hawakosi wanachokitaka na wanapenda watoto wao wawe na elimu nzuri. Hata hivyo ni wazazi ambao wanategemea watoto wao wafuate wanavyotaka wao vinginevyo inakuwa matatizo.

MADINI YA NG'OMBE:

Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinavyoitwa ALMASI au EMARALD.
Mawe haya yanawafanya wenye nyota ya ng'ombe wawe katika hali yao ya kike kike (Feminine) vili vile thamani ya mawe haya ni uthibitisho wa nyota hii katika fedha.

UHUSIANO WA KIMAPENZI:

(NG'OMBE NA N'GE):
Tabia ya uaminifu na ukweli waliokuwa nao wenye nyota ya ng'ombe inakuwa ni faraja kubwa kwa nyota ya Nge ambao wana tabia ya wivu kupita kiasi na kudhania maovu, kutuhumu na kushuku.

VYAKULA VYA NG'OMBE:

Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndivyo vinavyotawaliwa na nyota yao; Tofaa (apple), (oysters), viazi mbatata (potatoes), na dover sole.

NCHI ZA NG'OMBE:

Ili kupata mafanikio ya kinyota, kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao; baadhi ya nchi hizo ni USSR (Urusi), Ireland, St louis,na Lucerne (Switzerland).

RANGI ZA NGOMBE:

Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi za kijani au rangi za pinki au rangi ya bluu ambayo haijakoza katika nyumba zao au sehemu zao ya biashara ili kuleta mvuto wa kinyota.

UKITA UFANYE KITU GANI ILI UFANIKIWE KATIKA MAISHAYAKO UNAWEZA KUNITAFUTA KWA KUBONYEZA HAPA.
Mawasiliano

Mi tar 4/1 nipe future hapo
 
Mh. mimi 22nd feb. naomba future yangu tafadhar maana nimeona niko no4 lkn cjaelewa. mie ni ke. asante
 
Mi tar 4/1 nipe future hapo

6 January [Capricornian]

NYOTA YA MBUZI (CAPRICON)

  • Hii ni nyota ya kumi katika mlolongo wa nyota 12.
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 22 Dec na 19 Jan ya mwaka wowote.
  • Sayari yao ni SATURN (ZOHAL)
  • Siku yao ya bahati ni Jumamosi.
  • Namba yao ya bahati ni 8.
  • Rangi yao ya bahati ni rangi ya Kijivu au Nyeusi.
  • Asili yao ni Udongo.

KIPAJI CHA MBUZI(GRADUAL)

Wenye nyota hii wana kipaji cha kuchambua mambo kidogo kidogo au kufuatilia kitu bila watu kujua na kupata ufumbuzi wa uhakika mwishoni.

TABIA ZA MBUZI

Wale wote waliozaliwa katika nyota hii ni watu ambao wanapenda kuwajibika, ni wenye bidii ya kazi, katika kazi yeyote watakayofanya hata kama ikiwa ni ya kipuuzi.
Ni viumbe waaminifu sana na ni watu wastahamilivu na wenye kuweza kuvumilia matatizo yeyote.
Kwa upande mwingine ni watu wenye tamaa kubwa ya kimaisha na kimaendeleo, na kwa sababu ya kutekeleza malengo yao basi huwa wanakuwa wabinafsi na wenye uroho na uchu.


TABIA YA MBUZI KATIKA MAPENZI

Watu wenye nyota hii wanakuwa ni watu wenye aibu sana kwa wapenzi wao lakini aibu ikishawaondoka huwa ni wapenzi wa kutisha, kwa maana ya kwamba kwa vile wao ni waaminifu wanataka wapenzi wao wawaunge mkono katika hisia zao za kimapenzi.
Ni watu wanaoogopa sana kuachwa na wapenzi wao hivyo basi huwa wanakuwa waangalifu sana katika kuchagua wapenzi.
Jambo jingine ni kuwa huwa wao wenyewe hawajiamini kimapenzi, mara nyingi wanashindwa kuingia katika mapenzi kwa woga tu hivyo kukosa nafasi nzuri ya kupendwa.
Kwa ujumla ni wapenzi makini na huwa hawaoi mpaka wapate uhakika wa kutosha kutoka kwa wapenzi wao. Ni wapenzi makini, waaminifu na wanaoweza kuaminiwa. Lengo lao katika mapenzi ni usalama.

TABIA YA MBUZI KATIKA FEDHA

Kwa watu wenye nyota hii fedha ni kitu muhimu sana katika maisha.
Watu wa Mbuzi wanaamini kabisa kwamba fedha ndio zitawapa uwezo wa kuweza kupambana au kukabiliana na mazingira ya Dunia, hivyo basi suala lolote la fedha na mali wanalichukulia kwa uzito mkubwa sana.
Inawachukua muda mrefu kutekeleza malengo yao ya kifedha lakini wakishazipata basi huwa hawatetereki tena. Wana uwezo wa kuhifadhi walichonacho.
Ni watu wabahili sana na hata kama wakiwa na fedha nyingi utaona wanaishi maisha ya kawaida na wala huwezi kuwajua.
Fedha zao zinatoka kwa sababu maalum ya dharura na wala siyo katika starehe au vinginevyo na hiyo ni kwa sababu hupenda kukumbuka walikotoka katika hali ya umasikini au ufukara.
{mospagebreak}

MAVAZI YA MBUZI

Wenye nyota ya Mbuzi wanatakiwa wavae nguo za mitindo, zilizoshonwa kwa ustadi.
Nguo hizo ziwe za rangi ya kijivu au Kijani iliyoiva au hudhurungi nzito.
Kitambaa kiwe cha kitani (Linen) au cha ngozi.
Nguo ziwe ni suti na ziambatane na saa za mikononi.

MATATIZO YA KIAFYA

Nyota hii inatawala Mifupa, Magoti na Ngozi.
Matatizo yao makubwa ya kiafya huwa yanasababishwa na muda mrefu ambao wanafanya kazi au kujishughulisha.
Hii ni kwa sababu hawamwamini mtu mwingine afanye shughuli zao ambazo zina mipangilio ya muda mrefu, nguvu nyingi, na akili hutumika.
Shughuli zao nyingi za mizunguko na kufikiria huwaletea maradhi kama Baridi Yabisi (rheumatism).
Maradhi yao mengine makubwa ni ugonjwa wa ngozi, matatizo ya Magoti na maradhi ya mifupa.

KAZI ZA MBUZI

Wenye nyota ya Mbuzi kitu muhimu katika maisha yao ni kazi na maisha mazuri na yanayoeleweka ambayo yako katika mpangilio wanaoutaka wao.
Ni watu ambao wanazingatia sana muda wa maisha na wana mpangilio maalum kwamba katika umri fulani awe amepata nini au awe na fedha kiasi gani.
Ni wenye kupenda utekelezaji wa kazi wa hali ya juu na wao wanapoagizwa hufanya hivyo.
Kazi zao zinazowafaa ni zile za kutumia akili, Uhandisi, Usanifu Majengo, Saveya, kazi za Serikali, Siasa na Daktari wa Meno.

FAMILIA ZA MBUZI

Wazazi wenye nyota ya Mbuzi ni watu ambao wamepangilia kabisa mipango ya watoto wao kabla hawajazaa.
Ni wazazi ambao wanayachukulia kwa uzito mkubwa majukumu yao ya kulea na hawakubali kabisa watoto wao kufanya michezo michezo ya kipuuzi. Wanapenda kuwahimiza watoto wao kuwa na malengo ya maana.
Wanapenda sana nidhamu katika familia zao.
Mara nyingi wazazi wa kiume huwa hawapati muda kuwa na watoto wao kutokana na kazi nyingi walizonazo lakini kwa wazazi wa kike wanakuwa wanatumia akili ya hali ya juu katika kutatua matatizo au hisia za watoto wao.

MADINI YA MBUZI

Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinayoitwa Black Jet.
Jiwe hili inaaminiwa lina uwezo wa kuongeza ujasiri na kumletea mvaaji mafanikio ya kibishara.

UHUSIANO WA KIMAPENZI (MBUZI NA KAA)

Tabia ya Mbuzi ya ubahili na kutopenda anasa hulainishwa na tabia ya Kaa ya upendo, mapenzi na huruma.

VYAKULA VYA MBUZI

Wenye nyota ya Mbuzi wanashauriwa wapende kula vyakula au matunda yafuatayo. Ambayo ndio yanatawaliwa na nyota yao.
Wapende sana vyakula vya Nazi na Nyama yeyote.
Vile vile wapendelee kula Viazi Vitamu na Samaki Gamba (Shellfish).

NCHI ZA MBUZI

Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa watu wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee miji au nchi zifuatazo ambayo inatawaliwa na nyota ya Mbuzi.
Miji hiyo ni Brussels (Ubelgiji) na Oxford (Uingereza) au nchi za Mexico na India.

RANGI ZA MBUZI

Wenye nyota hii wanashauriwa wapake rangi zifuatazo kwenye nyumba zao, rangi ya Kahawia (Brown) Rangi ya Kijivu (Grey) au Nyeusi


  • UKITA UFANYE KITU GANI ILI UFANIKIWE KATIKA MAISHAYAKO UNAWEZA KUNITAFUTA KWA KUBONYEZA HAPA.Mawasiliano






 
Mh. mimi 22nd feb. naomba future yangu tafadhar maana nimeona niko no4 lkn cjaelewa. mie ni ke. asante

NYOTA YA SAMAKI (PISCES)

  • Hii ni nyota ya 12 katika mlolongo wa nyota 12
  • Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 19 February na tarehe 20 Machi.
  • Sayari yao ni JUPITER (MUSHTARA)
  • Siku yao ya Bahati ni Alhamisi.
  • Namba yao ya Bahati ni 8.
  • Rangi yao ya Bahati ni Zambarau au Kahawia iliyochangamka.
  • Asili ya nyota yao ni Maji.

VIPAJI VYA SAMAKI (VISIONARY)

Wenye nyota hii wana kipaji cha kufikiria jambo na kuliunda na likawa vile walivyotaka wao.

TABIA ZA SAMAKI

Watu wenye nyota ya Samaki ni wenye huruma, wapole na wenye moyo mzuri na hawawezi kukubali kumuona binaadamu mwingine akipata taabu au uchungu. Kwa hakika ni watu ambao wana hisia kati kwa wengine ni watu ambao hawajipendelei na wako tayari wakati wowote kujitoa mhanga ili watu wanufaike, mapenzi yao au huruma kwa binadamu wengine hayana masharti yeyote.
Nafsi zao zimegawanyika katika nafsi ndogo ndogo kama vile muathiriwa mwenye kujitoa mhanga, mwokozi, na mkombozi.
Hayo yote yaliyotajwa wanaweza kuyatekeleza inapohitajiwa na ikiwa mwenye nyota hii akishatumbukia katika moja ya mambo hayo huwezi kumtoa.
Kwa ujumla nafsi za wenye nyota ya Samaki siyo za kidunia, ni watu wabunifu na wenye ndoto za kufikiri mambo ya baadaye na katika maisha yao wanaona raha sana kuwa na mawazo ambayo yatawaepusha na ugumu wa maisha.
Ikiwa wamekwama katika jambo lolote basi wataitafuta faraja au watajituliza kwa ulimwengu wao wa mawazo.

TABIA YA SAMAKI KATIKA FEDHA

Ni vigumu sana kukadiria tabia za wenye nyota hii katika fedha kwa sababau wote waliozaliwa katika nyota huwa wanachanganyikiwa kwa sababu huwa wanashindwa kutafautisha kati ya matumizi na thamani ya fedha.
Hii ni kwa sababu wanashindwa au hawakubali vikwazo kati ya muda na nafasi au za kwako na zangu, kwao kila kitu ni sawa sawa.
Pamoja na kwamba wana uroho wa pesa, uwezo na matamanio lakini wanajichukulia mambo kadri yanavyokuja. Kwao wakiwa na fedha sawa wakiwa hawana sawa vile vile kwao uwezo wa kubuni au kutunga taswira ni muhimu kuliko fedha.
Mara nyingi huwa wanajishughulisha na masuala ya kutatua matatizo ya watu wengine kuliko masuala ya kifedha. Wakati wote wako tayari kupoteza fedha kuliko kuibiwa ndoto zao.

TABIA YA SAMAKI KATIKA MAPENZI

Wenye nyota ya Samaki ni wenye kukamilika na Mahaba mengi na wanapenda sana kujitumbukiza na kuzama kwenye dimbwi la mapenzi.
Kuwa katika mapenzi ni kitu wanachokipenda na kukifurahia sana. Ni waangalifu wazuri kwa wapenzi wao wana huruma nyingi.
Ni watu wenye hisia kali za kimapenzi na ni wepesi kuathirika.
Mara nyingi huwa waoga wa vitu vya kimapenzi kwa sababu ya kuogopa kuvurugika kwa mipango yao ya baadaye.
Ni watu wenye kuyachukulia mapenzi kama ua la waridi na wanawaona wapenzi wao kama binaadamu wasio wa kawaida.
Tatizo lao kubwa la kimapenzi ni kwamba wanawaamini sana wapenzi wao na wanakuwa na mawazo au firika za kimapenzi ambazohazipo katika dunia hii.
Kwa ujumla wenye nyota hii wanapokuwa katika mapenzi wanakuwa wamejawa na shauku na mifano ya kuvutia na wanapenda wapwnzi wao waishi kiroho. Mategemeo yao yanakuwa makubwa na yaispotimia huwa wanavunjika moyo.
{mospagebreak}

MAVAZI YA SAMAKI

Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wavae nguo za michezo kama vile fulana au za kiasili na zilizoongezwa madoido na vimbwanga vingi.
Nguo zao ziwe za rangi ya Zambarau au Kahawia iliyochangamka na rangi ya bluu.
Kitambaa kiwe cha sufu (tweed)
Wanawake wapendelee sana kuvaa sketi, ikiambatana na mikanda na viatu vyao viwe vya bati.

MATATIZO YA KIAFYA

Nyota hii inatawala nyayo na vidole vya miguu.
Matatizo yao ya kiafya yanakuja pale wanaposhindwa kutekeleza ndoto zao au mipangilio yao kimaisha au wanapokorofishana na wapenzi wao.
Wanapoathirika na hayo yaliyotajwa hukimbilia kwenye ulevi na utumiaji vidonge uliokithiri.
Tatizo lingine ni maradhi ya nyayo za miguu, uvimbe unaotokana na baridi kali hasa katika vidole vya miguu.

KAZI ZA SAMAKI

Kugunuda muelekeo wa kimaisha kwa wenye nyota hii wakati mwingine huwa ni matatizo.
Tabia yao ya kushughulikia sana binaadamu wengine huwafanya wasiwe na muelekeo.
Wenye nyota hii wanatakiwa wasifanye ubaguzi katika kazi.
Wanatakiwa wafanye kazi ambazo zinazohusiana na kusaidia watu. Kipaji cha kutafsiri mambo huwasaidia vile vile kufanya kazi za sanaa kama vile kupiga picha na kazi za muziki au maigizo.
Kazi zingine zinazowafaa ni za kuhudumia wagonjwa, kucheza shoo, uaskari wa majini (Navy) kazi za dini au kazi za kutoa ushauri nasaha (Counselling).

FAMILIA ZA SAMAKI

Wenye nyota hii ni wazazi wenye hisia, wanaopenda watoto wao na wanahuruma hasa watoto wanapowasikiliza.
Pamoja na hayo wazazi wa Samaki wana matatizo ya kukubali kwamba watoto wanaweza kuwa tofauti na wao, hata mwishowe wanapokubaliana na hilo huwa wanawachukulia watoto wao kama wageni kuliko ndugu.
Mtoto akiwa anapenda kusoma na mwenye kujituma au akiwa na tabia ya kutumia sana akili kuliko moyo huwa hapendwi na mzazi wa Samaki.
Wazazi wenye nyota hii wana mipangilio mibovu ya nidhamu na muelekeo, hivyo watoto wakorofi huwa wanatumia mwanya huo kufanya mambo yao.
Hiyo ina maana kwamba watoto wa wazazi wa Samaki wanaweza kuharibika au kutumiwa kutokana na udhaifu wa wazazi wao.
{mospagebreak}

(MADINI YA SAMAKI)

Wenye nyota hii wanashauriwa wavae madini yanayoitwa.
Madini haya yanasaidia kupunguza hisia na kumuepusha mvaaji na ulevi.

UHUSIANO WA KIMAPENZI

(SAMAKI NA MASHUKE)
Tabia ya Samaki ya kuwa na mbinu na mawazo ya mambo ya baadaye huenda sambamba na tabia ya Mashuke ya utekelezaji na kujishughulisha bila kuchoka.

VYAKULA VYA SAMAKI

Wenye nyota ya Samaki wanashauriwa wapenda kula matunda au vyakula vifuatavyo.
Matunda ya Kunazi, Nyama mwitu kama Swala,nyati na kadhalika.
Vile vile wapendelee kula maboga.

NCHI ZA SAMAKI

Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota yao.
Nchi hizo ni Tonga na Tanzania na miji ni Alexandria (Misri) na Seville (Ufaransa).

RANGI ZA SAMAKI

Wenye nyota ya Samaki wanatakiwa wapake nyumba zao au magari yao au sehemu zao za biashara rangi ambayo haijakoza ya Bluu au Kijani au Urujuani (violet).



    • UKITA UFANYE KITU GANI ILI UFANIKIWE KATIKA MAISHAYAKO UNAWEZA KUNITAFUTA KWA KUBONYEZA HAPA.Mawasiliano

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom