Sticker ya Fire Extinguisher Ndiyo Nini tena??

Sticker ya Fire Extinguisher Ndiyo Nini tena??

Cynic

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2009
Posts
5,144
Reaction score
1,658
Hawa watawala ni wazuri kweli katika kubuni kero. Unatoka na gari lenye sticker safi ya insurance na road licence (ambazo kila mtu anajua zinachangia ktk pato la taifa). Halafu unasimamishwa na traffic police kwamba huna sticker ya usalama barabarani (zinazofadhiliwa na kampuni la simu) na sticker ya fire extinguisher (fire extinguishers zinapatikana kwa wafanyabiashara fulani). Tutafika namna hii? Ukiwauliza watu, kila mtu anakushangaa. Ila hii Sticker ya Fire Extinguisher ni mpya kabisa (imebuniwa mwaka huu). Yote kwa yote, huku ni kusababisha usumbufu usio wa lazima na pia kutengeneza mianya mipya ya rushwa.
 
MoD saidia kupeleka hii kwenye threads za kero. Sorry!
 
Pigia mstari.
Hiyo bima yenyewe haisaidii saana,maana du! Nashindwa kumalizia
 
ni wanajitanua ktk kupata vyanzo vya pesa, maisha magumu kila kukicha watu wanabuni kitu kipya, nilifika mwanza kuna kikosi cha matrafic kama 20 wanakaa kwenye njia ya shinyanga - mwadui road kazi yao ni kukagua stika za fire, wangekua wa maana zaidi kama wangekua wanakagua mtungi wenyewe, kitendo cha kukimbilia stika ni dalili kwamba wako kimaslai zaidi kuliko usalama barabarani
 
Kuna jamaa anamradi wa fire extingusher, kwani sasa wanasema eti za maji hazifai inabidi kununua fire extinguisher za powder je huu ni ulaji wa mtu?
 
Pigia mstari.
Hiyo bima yenyewe haisaidii saana,maana du! Nashindwa kumalizia

Kweli Shaycas. Niliwahi kuwa na comprehensive ya NIC, ikatokea tatizo, nikadai, wakafanya evaluation na mambo yote, lakini nilifuatilia kwa miaka 6 wananizungusha, nikanawa. Nikakoma kukata comprehensive.
 
Kuna jamaa anamradi wa fire extingusher, kwani sasa wanasema eti za maji hazifai inabidi kununua fire extinguisher za powder je huu ni ulaji wa mtu?

Maajabu! Tumeishi miaka 50 ya uhuru (awamu tatu) bila stickers za fire extinguisher na hakuna kilichoharibika. Inawezekana pia ni huu ni moja ya miradi ya kukushanya hela wa mtandao.
 
Washaananza kukusanya hela za uchaguzi, kwani wewe hujui pattrns zao?
 
ni wanajitanua ktk kupata vyanzo vya pesa, maisha magumu kila kukicha watu wanabuni kitu kipya, nilifika mwanza kuna kikosi cha matrafic kama 20 wanakaa kwenye njia ya shinyanga - mwadui road kazi yao ni kukagua stika za fire, wangekua wa maana zaidi kama wangekua wanakagua mtungi wenyewe, kitendo cha kukimbilia stika ni dalili kwamba wako kimaslai zaidi kuliko usalama barabarani

Nakubaliana na wewe.

Stickers 5 kwenye gari za nini? Kwanza sticker ya road licence inatosha. Tunapokata road licence tunaenda traffic police kwa ukaguzi kwanza (ambao wanaangalia kama gari liko ktk hai nzuri ya kutembea kwa mwaka mzima, na limekamilika - ikiwa ni pamoja na fire extinguisher). Inasikitisha sana watu waliopewa dhamana kufanya maamuzi ya kipuuzi puuzi ....
 
Back
Top Bottom