Startimes wameondoa 'free channels'

Startimes wameondoa 'free channels'

Inwezekana mama akawaweza
How? Kipindi kile walikuwa wanaalamishwa Local chanel ziwe free kwa kila King'amuzi lakini wakina DSTV waligoma! Ikabidi DSTV wasiwenazo kabisa, kipindi Nape anateuliwa baada kama ya wiki tu akawaruhusu DSTV kurudisha Local Chanel lakini DSTV waliendelea na kipengere chao kuwa Local Chanel nazo yakupasa ulipie ndo uzione ambapo ni kinyume na sheria, sasa basi kama Startimes nao wamenaza basi jua Azam nae atafuata wakati ilo lilishaondolewa.

Mama atawawezea wapi?
 
Nimekaaaaa nkatafakari Kwanini ving'amzi vya startimes wameamua kuondoa kimaksudi kabisa channel zote za ndani na kubakiza channel moja tu ya TBC1.

Ukiwapigia wanakujibu wajuavyo tu bila kujua wanavunja Sheria imeniuma Sana, yaaaan ving'amuzi vyote Tanzania wanaonesha free channels ila wao wanajifanya kuvimba vichwa, huu ni mwezi wa nne Sasa toka wazifute, ohhh my Tanzania.

Tunaomba katika Hili serikali iliingilie kati channel zirudi Kwa wote watumiao startimes ili haki iwe sawa Kwa wote, Rais Samia, plse tuma watu wako ili wakalitizame na Hilo Tena Kwa uharaka zaidi.
Hivi mnatarajia wapate wapi hela ya operations iwapo kila mtu anategemea free channels?
 
Kwani sheria inasemaje?
Kama wamevunja sheria si ukafungue kesi ya madai upate mamilioni.
Kila kitu serikali, serikali, serikali
Mara Rais, Rais, Rais.
 
Itakua gharama za kulipia serikalini zimepanda na wao wakaamua kutoa free channels, tuanze kuzilipia hizo free channels ili kufidia hizo gharama zilizopanda
 
Nadhani hiyo kampuni ya startimes ndio makubaliano yao ya kuwa " subscription ikiisha basi unaruhusiwa kuendelea kutizama channel inayomilikiwa na serikali."
Nasema hivi maana hata huku +254 wanatuachia KBC na guide".
Bure kabisa!
 
Unauhakika ndugu?? Mbn mm naangalia hapa Free channels na sijakilipia takriban miez mitatu sasa ?
 
Back
Top Bottom