Nimependa sana strategies za technical bench la Taifa Stars kuelekea mchezo wa leo.
Mwalimu ameamua kutumia mfumo wa kushambulia ili tupate goli la mapema na kupunguza kasi ya wao kucheza na kutushambulia.
Mwalimu atatumia mfumo wa 4-3-3 kwa kuwapanga kwa pamoja kule mbele Ngassa, Ulimwengu, Sama Goal wakati Viungo watakuwepo Damayo, Sure Boy na Kiemba. Nyuma kama kawaida Juma K Juma, Nyoni, Kapombe, Yondani na Agrey.
Kwahivo leo tutarajie ushindi, tuna kila sababu ya kushinda ugenini kutokana na maandalizi mazuri ya timu yetu!