Starehe yako ni nini?

Starehe yako ni nini?

BUSARA ZANGU

JF-Expert Member
Joined
May 5, 2013
Posts
778
Reaction score
1,269
Mambo vipi wakuu

Kuna kaswali kakizushi, naomba tubadilishane uzoefu, kwani inafahamika kila mtu kuna kitu flani anakipenda.

Kuna watu wanapenda sana MSOSI. Mnyime kitu chochote lakini sio msosi mzuri.

Kuna watu wanapenda sana TUNGI. Hawa watu wasipo pata kinywaji wanaweza hata kuugua.

Wengine bhana ni NGONO. Umeshawahi kuona mtu anaacha dili ya hela kisa anafuata Papuchi? Mimi nimewaona. Kuna wanawake pia wanatajwa kuwa na pepo la ngono.

KUINGIZA HELA. Hii nayo ni addiction. Hapa kuna watu watakuambia kila mtu anapenda hela, ni kweli lakini si kwa kiwango sawa. Kama mtu anatunza hela tu, hali kiuhakika, havai vizuri...n.k. Kuna mtu nimewahi kumuuliza wewe starehe yako ni ipi, mbona sioni hata siku moja ukipiga kilevi, au Disko au madem, jibu alilonipa ni kwamba akiona hela kwenye akaunti nafsi yake inakuwa na burudaaani.

Kuna wanaopenda disko/mziki balaa.

Kuna wanaopenda soka balaa

Kuna wanaompenda Magufuli balaa.

Wewe unapenda nini ?
 
Ulozi
 
Mi napenda nimuone nimpendaye tu on right time tu.Hela hata ndege hawazijui lakn mapenzi wanayajua.Kwangu mwanamke ndiyo kila kitu maishani maana wabaya wapo lakini wazuri kwangu pia ni wengi.
Sioni umuhimu wa maisha yangu bila viumbe hawa.Kusikiliza sauti zao tu ni zaidi ya amani kwangu.
Mungu wabariki wanawake sina neno zuri la kuwasemea ili wabarikiwe bali wewe wanijua fika mapungufu yangu na ninadhani hukumu yangu mbele yako itajikita sana eneo hili.
Ikiwa utapenda kwa mapenzi yako viumbe hawa wawe mbali nami niko radhi ila ikiwa si mapenzi yako na uchumi wangu utaimarika mara dufu maana nahisi ni ibada.
 
KUBETI, ikipita siku bila kubeti naona kabisa navyo kosa hela, naweza nikaamka usiku wa manane kuzitafuta timu za america kutia mizigoooo.
 
Kulala aisee yani kila kitu nngeshushiwa ili nilale tu ingekua burudani sana
 
Kusafiri
Nakumbuka nipo form V nimepewa pocket money ya shule ikaishia kurasini immigration lengo nianze safari za nje. Nashukuru familia inaelewa hobby ya mtu
 
Back
Top Bottom