Star TV mmepotosha watazamaji wenu

Star TV mmepotosha watazamaji wenu

jebibay

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2012
Posts
1,431
Reaction score
642
Asubuhi hii kuna kipindi cha Star Tv kinachozungumzia mada kuhusu dhana halisi ya demokrasia. Nimeshangaa mwongoza kipindi kudai kwamba Barack Obama ni muislam na kusema kwamba pamoja na kwamba yeye ni muislam, wamarekani ambao wengi ni wakristo walimchagua. Mchambuzi aliyepo studio naye akakubaliana kwamba Barack Obama ni muislam !

Barack Obama ni mkristo na kwa muda mrefu amekuwa akisali kwenye kanisa linalojulikana kama United Church of Christ na ndipo alipobatizwa na baadaye alijiunga na kanisa la kibaptisti......Kwa kifupi ni Mkristo na si muislam....

Hivyo hicho mlichowaeleza watazamaji wenu sio sahihi. Mmewapotosha !
 
Kwani alipoapishwa alibeba biblia au kuruani
 
waandishi wa star tv chadema imewakolea mpaka akili zinawatoka,kazi yao kualika BAVICHA waje waitukane serikali na nchi oamoja na watanzania,wakiwa hapo studio wanajifanya wachambuzi,lakini sasa wanaumbuka,tutashuhudia hao wanaojiita wachambuzi wakichukua fomu za kugombea kupitia Chadema
 
Kweli, wasahihishe kosa hilo. Babae Muislam, ***** Mkristo.
 
waandishi wa star tv chadema imewakolea mpaka akili zinawatoka,kazi yao kualika BAVICHA waje waitukane serikali na nchi oamoja na watanzania,wakiwa hapo studio wanajifanya wachambuzi,lakini sasa wanaumbuka,tutashuhudia hao wanaojiita wachambuzi wakichukua fomu za kugombea kupitia Chadema

yanausianaje na Obama hayo na ww mbona unajifanya mujuaji asiejua
 
Asubuhi hii kuna kipindi cha Star Tv kinachozungumzia mada kuhusu dhana halisi ya demokrasia. Nimeshangaa mwongoza kipindi kudai kwamba Barack Obama ni muislam na kusema kwamba pamoja na kwamba yeye ni muislam, wamarekani ambao wengi ni wakristo walimchagua. Mchambuzi aliyepo studio naye akakubaliana kwamba Barack Obama ni muislam !

Barack Obama ni mkristo na kwa muda mrefu amekuwa akisali kwenye kanisa linalojulikana kama United Church of Christ na ndipo alipobatizwa na baadaye alijiunga na kanisa la kibaptisti......Kwa kifupi ni Mkristo na si muislam....
A
Hivyo hicho mlichowaeleza watazamaji wenu sio sahihi. Mmewapotosha !
Hili ni tatizo la waandishi wetu na start tv/radio free Afrika wamezidi. Hawafanyi research kabla ya kutamka.
 
waandishi wa star tv chadema imewakolea mpaka akili zinawatoka,kazi yao kualika BAVICHA waje waitukane serikali na nchi oamoja na watanzania,wakiwa hapo studio wanajifanya wachambuzi,lakini sasa wanaumbuka,tutashuhudia hao wanaojiita wachambuzi wakichukua fomu za kugombea kupitia Chadema
Waliosema hayo ni waajariwa wa star tv ambayo inamilikiwa na Mwenyekiti wa ccm wa mkoa wa mwanza!
 
Hata baba yake hakuwa muislamu. Maeneo ya vijijini kama kule alikokulia Hussein Obama, watu hutumia majina yeyote tu. Utakuta Asha ambaye ni mkristo au asiye na dini. Baba Obama hakuwa na dini
 
waandishi wa star tv chadema imewakolea mpaka akili zinawatoka,kazi yao kualika BAVICHA waje waitukane serikali na nchi oamoja na watanzania,wakiwa hapo studio wanajifanya wachambuzi,lakini sasa wanaumbuka,tutashuhudia hao wanaojiita wachambuzi wakichukua fomu za kugombea kupitia Chadema
Nashangaa kwanini mpaka sasa hivi hujaangukiwa na nyundo la life ban kutokana na hiyo ID yako,achilia mbali huo utumbo wako.
 
Star tv hawapo serious. HakunA producer wa kucorrect walichokisema?
 
Mgeni aliyepo Star Tv kwenye hichi kipindi si Bavicha. Ni mzee ambaye inaelekea ni mwalimu kwa sababu ametambulishwa kuwa ni mwalimu....

waandishi wa star tv chadema imewakolea mpaka akili zinawatoka,kazi yao kualika BAVICHA waje waitukane serikali na nchi oamoja na watanzania,wakiwa hapo studio wanajifanya wachambuzi,lakini sasa wanaumbuka,tutashuhudia hao wanaojiita wachambuzi wakichukua fomu za kugombea kupitia Chadema
 
Hata baba yake hakuwa muislamu. Maeneo ya vijijini kama kule alikokulia Hussein Obama, watu hutumia majina yeyote tu. Utakuta Asha ambaye ni mkristo au asiye na dini. Baba Obama hakuwa na dini

acha kupotosha ww familia ya mzee Husein Obama ni Islamic kabisa fatilia kwanza ndio uje hapa ucdhani tu
 
startv hawajui wasemayo.
Obama si mwislamu baba ndio mwisilam uisilam unasema ukizaliwa nje ya ndoa utafata dini ya mama
 
Back
Top Bottom