Star tv mijadala.

Mpevu

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
1,805
173
Waungwana,
Mimi binafsi nimekuwa nikifatilia mijadala mingi na yenye tija kwa taifa hili kupitia luninga ya Star, ambapo baadhi ya mijadala hiyo nimepata kuchangia.
Ninadhani sasa,, ya kwamba iwafikie waendeshaji wa kipindi hicho cha TUONGEE ASUBUHI kwamba watujulishapo juu ya mjadala/midahalo wakusudiayo kuirusha hewani siku hiyo ya j2 basi itapendeza zaidi kama wawe wanatupa taarifa humu jamvini walau 5-days kabla ya kipindi ili kama wanahitaji michango TULIVU na yenye TIJA toka humu iweze kuwasaidia na kuisaidia jamii kiujumla.
Tutoapo michango kwa 1/2/3-days before wengine huwa hatuna utulivu wa kuchambua/kunyambua vema na kujenga hoja nzuri, na badala yake huwa tunatoa michango ya papo hapo while huenda ni topic yenye ujenzi kwa taifa na jamii kiujumla.
Naomba kuwasilisha na iwafikie wadau hao nguli wa tasnia ya habari nchini.
 
Ni kweli mda wanaotoa kwa ajili ya kujadili mada hizo huwa ni kidogo hapa jf, nadhani mkuu ameipata hii!
 
Waungwana,
Mimi binafsi nimekuwa nikifatilia mijadala mingi na yenye tija kwa taifa hili kupitia luninga ya Star, ambapo baadhi ya mijadala hiyo nimepata kuchangia.
Ninadhani sasa,, ya kwamba iwafikie waendeshaji wa kipindi hicho cha TUONGEE ASUBUHI kwamba watujulishapo juu ya mjadala/midahalo wakusudiayo kuirusha hewani siku hiyo ya j2 basi itapendeza zaidi kama wawe wanatupa taarifa humu jamvini walau 5-days kabla ya kipindi ili kama wanahitaji michango TULIVU na yenye TIJA toka humu iweze kuwasaidia na kuisaidia jamii kiujumla.
Tutoapo michango kwa 1/2/3-days before wengine huwa hatuna utulivu wa kuchambua/kunyambua vema na kujenga hoja nzuri, na badala yake huwa tunatoa michango ya papo hapo while huenda ni topic yenye ujenzi kwa taifa na jamii kiujumla.
Naomba kuwasilisha na iwafikie wadau hao nguli wa tasnia ya habari nchini.

SAFI IKO POA SANA HATA MiMI NAIFUATILIAGA
 
Waungwana,
Mimi binafsi nimekuwa nikifatilia mijadala mingi na yenye tija kwa taifa hili kupitia luninga ya Star, ambapo baadhi ya mijadala hiyo nimepata kuchangia.
Ninadhani sasa,, ya kwamba iwafikie waendeshaji wa kipindi hicho cha TUONGEE ASUBUHI kwamba watujulishapo juu ya mjadala/midahalo wakusudiayo kuirusha hewani siku hiyo ya j2 basi itapendeza zaidi kama wawe wanatupa taarifa humu jamvini walau 5-days kabla ya kipindi ili kama wanahitaji michango TULIVU na yenye TIJA toka humu iweze kuwasaidia na kuisaidia jamii kiujumla.
Tutoapo michango kwa 1/2/3-days before wengine huwa hatuna utulivu wa kuchambua/kunyambua vema na kujenga hoja nzuri, na badala yake huwa tunatoa michango ya papo hapo while huenda ni topic yenye ujenzi kwa taifa na jamii kiujumla.
Naomba kuwasilisha na iwafikie wadau hao nguli wa tasnia ya habari nchini.

Nitoe shukrani zangu za kipekee kabisa kwa niaba ya Msimamizi wa Vipindi Star TV kwa WanaJF wote ambao wamekuwa nasi bega kwa bega kushiriki nasi kwa kuchukua muda wao kutafiti masuala muhimu kabisa yenye Tija kwa Taifa kwa kutoa mawazo ambayo kwa kweli ni haki ya msingi ya kila Mtanzania ili kuisaidia serikali yetu na kuikumbusha wajibu wake katika kumletea Mtanzania Ustawi mzuri.
Tumekuwa tukitoa mada wikiendi kwa uzoefu imeonyesha ni muda ambao wanaJF wengi wanakuwa busy katika mtandao. Lakini wazo la kutoa mada mapema ni jema na tumelipokea na kwa kuanzaia naomba kuwasilisha mapema mada ya Ijumaa wikii na Jumapili:

'' Kwa nini watanzania wananyimwa fursa ya kuwa na Nishati ya uhakika ya Umeme'' IJUMAA WIKI HII - 24.12.2010

'' Kuna Ulazima gani wa matumizi ya Nguvu kupita kiasi kwa Jeshi la Polisi katika kukabiliana na Watuhumiwa/Wahalifu'' Jumapili BOXING DAY

Merry x-mas Wadau

Naomba kuwasilisha

Yahya M
 
'' Kwa nini watanzania wananyimwa fursa ya kuwa na Nishati ya uhakika ya Umeme'' IJUMAA WIKI HII - 24.12.2010

Muongozaji,
Taifa letu hili ni changa na lenye changamoto lukuki katika ukiaji wake, tunazo changamoto hasi na chanya.
  • Taifa halina misingi/mipango endelevu juu ya janga hili la umeme.
  • Taifa haliwezi kusonga mbele kimaendeleo pasipokuwa na nishati kamilifu na yenye kuvutia hata wawekezaji.
  • Kwa nyakati tofauti taifa limeshuhudia tatizo la nishati bila ufumbuzi wa kudumu, tunarithisha tatizo hili kwa vizazi pasipo kulitafutia ufumbuzi yakinifu.
  • Nishati ya umeme inadidimiza wananchi kwa kushindwa kuendeleza hali zao za ujasiriamali na kukuza uchumi wa taifa letu.
  • Maendeleo yahitaji nishati, hapa namaanisha maendeleo ya rasilimali watu-KIELIMU, maendeleo ya nchi-KIVIWANDA etc,,vyote vyategemea nishati hii adhimu ya umeme. kinyume chake kumekuwa na mipango mibovu na isiyo na dira ya janga la umeme kuwa ni historia walau tu kwa kizazi hiki.
  • Katika kipindi hiki cha mitikisiko ya uchumi duniani, tungetegemea kutoweza kuona janga la umeme kuikumba nchi yetu...bali matokeo yake tumeruhusu kuuyumbisha uchumi wa nchi tena kwa tatizo la nishati.
nadhani ifike wakati sisi wananchi wa kawaida tuangaliwe vema na wakuu wetu wa nchi,
 
'' Kwa nini watanzania wananyimwa fursa ya kuwa na Nishati ya uhakika ya Umeme'' IJUMAA WIKI HII - 24.12.2010

Muongozaji,

Taifa letu hili ni changa na lenye changamoto lukuki katika ukiaji wake, tunazo changamoto hasi na chanya.
  • Taifa halina misingi/mipango endelevu juu ya janga hili la umeme.
  • Taifa haliwezi kusonga mbele kimaendeleo pasipokuwa na nishati kamilifu na yenye kuvutia hata wawekezaji.
  • Kwa nyakati tofauti taifa limeshuhudia tatizo la nishati bila ufumbuzi wa kudumu, tunarithisha tatizo hili kwa vizazi pasipo kulitafutia ufumbuzi yakinifu.
  • Nishati ya umeme inadidimiza wananchi kwa kushindwa kuendeleza hali zao za ujasiriamali na kukuza uchumi wa taifa letu.
  • Maendeleo yahitaji nishati, hapa namaanisha maendeleo ya rasilimali watu-KIELIMU, maendeleo ya nchi-KIVIWANDA etc,,vyote vyategemea nishati hii adhimu ya umeme. kinyume chake kumekuwa na mipango mibovu na isiyo na dira ya janga la umeme kuwa ni historia walau tu kwa kizazi hiki.
  • Katika kipindi hiki cha mitikisiko ya uchumi duniani, tungetegemea kutoweza kuona janga la umeme kuikumba nchi yetu...bali matokeo yake tumeruhusu kuuyumbisha uchumi wa nchi tena kwa tatizo la nishati.
nadhani ifike wakati sisi wananchi wa kawaida tuangaliwe vema na wakuu wetu wa nchi,

Kwa niaba ya mwendeshaji wa Mjadala wa Kesho,
Mchango wako umefika Mpevu
Yahya M
 
Kwa hili Startv wanastahili pongezi na hususan ktk uchambuzi wa umuhimu wa katiba mpya. Kama statiopn nyingine zitaiga basi itakuwa ni ukombozi kwa Watz
 
' Kuna Ulazima gani wa matumizi ya Nguvu kupita kiasi kwa Jeshi la Polisi katika kukabiliana na Watuhumiwa/Wahalifu'' Jumapili BOXING DAY
Wenzetu wa jeshi la polisi hawana elimu yakutosha kuhusu haki ya mtuhumiwa, Kisheria mtuhumiwa anahaki zake, anahaki ya kusikilizwa, badala ya kutumia mabuvu na nguvu nyingi hata mahali ambapo hapana umuhimu wa kutumia, Naomba jeshi la polisi wapewe elimu na jinsi ya kukabiliana na mtuhumiwa na si kutumia mabavu. UNAJUA MKUU URITHI WA MJERUMANI NA MUARABU UNATUHARIBU SANA.
 
Back
Top Bottom