Stanbic wamegoma kutoa orodha ya waliochukua

Stanbic wamegoma kutoa orodha ya waliochukua

Madhara ya chama kutawala muda mrefu. Watu huanza kwiba na kudharau waajiri wao ambao ni wananchi. Unapoona rais wa nchi haelewi kwa majibu yake kwa wananchi, jua kunatatizo. Lapili, tabia yakuwekana madaraka na kundi la watu waliokua na lengo moja tuu, kupora rasilimali za nchi. Fikirieni, ni ndani ya uongozi wake huu, nchi imepitia matatizo makubwa ya kiuchumi. Kumbukeni, waka anaingia madarakani 2005, mzee mkapa aliacha dola moja (1$=900 hadi 1000). Leo jiulizeni tumefika wapi? Ma skendo kibao yenye kuhujumu nchi: EPA, RICHMOND, wanya pori kusafirishwa nje ya nchi, ESCROW, na mikataba mingine kibao isio na manufaa kwa nchi. Kwavile wanawekana, hata akija mwingine wa chama hikihiki, ataendeleza maovu na kufichana.
 
Swali langu ni je hatuwezi kuwalazimisha waitoe hiyo list. Matusi nadhani tupunguze. Mwenyewe nineacha siku hizi.
 
Nilisoma hapa nahisi sikuelewa vizuri. Ila nahisi wana uhusiano.
Stanbic Bank - Wikipedia, the free encyclopedia

Angalia kuna tofauti bayana:

(1) Stanbic Bank is a division of Standard Bank; Standard Bank now trades under the name Stanbic Bank in Tanzania and other African countries.

(2) Standard Chartered PLC is a British multinational banking and financial services company headquartered in London.
 
Kwa kuwa Stanbic wamegoma, na Inaonekana wana baraka za wakubwa flani kutoitoa orodha, je Hakuna sheria za nchi zinazoweza kuwalazimisha kutoa hiyo list? Japo majaji wetu nao walikula cha juu lakini nahisi kutakuwa na taratibu kama sio za hapa basi hata kimataifa.

Hakuna sehemu tunaweza kuishtaki stanbic wakatoa ile list?

Na akili yangu inanituma kwamba ujio wa Zuma ulikuwa na kitu flan kuhusu Escrow kwa sababu stanbic ni member wa standard bank ambao ni South Africa based.

Ebu tuchangamshe akili hapa.
Mkuu hizo sheria zinatekelewa na kusimamiwa na nani?duh wtz mnamoyo sana-To change this we need new utawala mpya nje ya ccm.
 
Angalia kuna tofauti bayana:

(1) Stanbic Bank is a division of Standard Bank; Standard Bank now trades under the name Stanbic Bank in Tanzania and other African countries.

(2) Standard Chartered PLC is a British multinational banking and financial services company headquartered in London.

Standard charted Sijasema mimi, Ebu Soma vizuri ndugu.
 
Taifa la mazuzu mpaka mataifa ya nje yanatuambia tumeibiwa lkn baadh yetu wanakataa,tujiulize kama kwel tuna akil timamu
 
Kwenye Orodha ya Stanbic na Mbiwe yumo. Ndo maana hali iko hivyo
Mbowe nae anaweza kusababisha serikali na vyombo vyake vikapata ganzi?Basi cheo cha amiri jeshi Mkuu tulikitupa kwenye msitu wa hifadhi ya milima udzungwa.
 
Mie najiuliza hivi kumbe kama kuna vikundi vya kigaidi vinafadhiliwa fedha kuhujumu nchi yetu na fedha hizo zikapotia kwenye mabenki yetu kumbe serikali haina uwezo wa kuziamuru benki hizo kutoa taarifa ya nani kalipwa fedha hizo?
Kama sheria zetu haziwezi kupata taarifa hizo toka mabenki yetu basi tuko hatarini sana.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mkuu hizo sheria zinatekelewa na kusimamiwa na nani?duh wtz mnamoyo sana-To change this we need new utawala mpya nje ya ccm.
I thought, kama wapinzani wameweza kuwa convince donors wanaweza wakatia presume hapo pia tukapata list.
 
Nchi ikiingia katika RUSHWA system yote huwa inaparanganyika,siyo serikali,bunge na mahakama wote chali.Hivi kwa nini Rais wetu hakuliongelea hili? BOT inajua taratibu sahihi za uchukuaji wa fedha kwa nini Gavana yupo kimya? Najuta kukishuhudia kizazi cha nyoka mapema hivi.Hata akina Kigunge watetezi wa Azimio la Arusha enzi hizo kimya.Wote hao walikuwa wanafiki kwa Mwalimu.Zuma na ANC yake ni aibu sana South Africa mpaka waafrika wenzao wanawashangaa.Rushwa rushwa unatupeleka wapi sasa na viongozi wetu?
 
Back
Top Bottom