Staili nyingine ya wizi ATM

Staili nyingine ya wizi ATM

shuda ya mobile money ni ukomo so huyu alishafikia ukomo na alikua ankwenda kuongeza kwa ATM
Hivi walipoleta mobile money hamjaelewa kazi yake, siongelei kwa lililomkuta huyu, mtu unatoa 50elf mpka ukapange foleni bank??[/QUOTE
 
tatizo unaongea kilugha cha kwenu, ungenyoosha kiswahili na kueleza kiurefu imekuaje tungejua ushauri gani unakufaa. hizo data zako kaa nazo wala hatuzitaki na sisi
tawire mwayego
 
Jamani wizi huo upo, kuna ndg yangu kaibiwa hela zote kwenye account yake ambapo alienda kutoa hela kwenye atm na akamkuta dada mmoja mfupi kiasi, mweupe, mwembamba na alikuwa kavaa ushungi, huyo dada alikuwa anahangaika kutoa hela kwenye atm jirani na aliyoitumia ndg yangu. Anadai yy aliingiza kadi yake kwenye mashine akatoa kiasi cha fedha alichohitaji na kadi ikatoka, pasipo kuangalia akaweka kadi yake kwenye wallet. Baada ya siku kadhaa kaenda kutoa hela kwenye atm na kadi ambayo si yake bila mwenyewe kujua, alipoingiza password ikagoma so akaingia ndani kulalamika, si ndio kushangaa kadi si yake, kuomba bank statement akakuta pesa zishalambwa, na alipoomba kuona picha akaambiwa camera ni mbovu, alipoomba benk wamlipe kaambiwa ukiibiwa kupitia kwa macashier wa bank unaweza kulipwa lakini ukiibiwa kwenye atm au simbanking hulipwi kwani huo ni uzembe wako. Tukio hili limetokea moro

Nimekuwa nadadisi matukio mengi ya watu kuibiwa fedha kwenye ATM hapa Bongo na nimegundundua kitu kimoja: Wengi wa waathirika wanafanya uzembe unaowezesha matapeli kupata access ya kadi zao na password. Kusema ukweli sisi watanzania hatupo makini kwa vitu vingi sana. Kuanzia kuandika, kufanya kazi na kutunza kadi zetu. Ukienda ATM nyingi kutoa fedha unakuta foleni. Sasa jambo moja ni kuwa watu wengi sana hawako makini wanapoingia kwenye ATM na kuingiza password zao. Watu wako free utafikiria wananunua pombe. Juzi juzi kuna mama mmoja alipoteza Driving licence, ATM card na kitambulisho chake. Sasa kituko kilichotokea. Aliyeviokota akaamua kuvipiga picha vyote na kuvianika hapa JF eti anamtafuta mwenyewe. Nilipoamua kutahadharisha kuwa hakufanya vizuri kuweka picha za vitu muhimu kama hivyo hapa nilishambuliwa kama mpira wa kona. Watu wanabisha na kusema eti ''hakuna usiri'' kwenye vitu kama hivyo. Hivi watu wa aina hii wanaweza kuwa makini wasiibiwe kweli?
 
Mie kwa kumbu kumbu zangu katika hizi mashine niliwahi poteza laki mbili sijui niseme kwa ujinga wangu? Nilichomeka kadi nikaomba laki2 wakati nasikia mashine ikihesabu umeme ukakatika. Ikatoka kadi tu pesa haikutoka ikabidi nimuulize askari mlinzi pale yale mazingira na kama yatakua na athari kwangu. Akawa amenijibu kuwa haina shida na itakuwa haikutoa pesa kutoka ktk account yangu. Nikaondoka na siku ile niliamua kubadili pesa ya kigeni niliyokua nayo kwa ajili ya matumizi. Nilisafiri na baada ya kama wiki tatu nilirudi na nilipoingia katika atm machine kutoa pesa niligundua balance iliyokuwepo ilikua imepungua laki mbili kwa salio langu la mwisho kutoa pesa.
 
Nimewahi kusoma mahali inakuwa hivi;
wewe unapoenda kwenye ile ATM yeye anakuwa ameshaifanyia mchezo mchafu ili utakapotoa ishindikane kwenye hatua za mwisho kabisa.
Wewe unapotoa yeye anakuwa ametega tu anakusikilizia akitegemea utakaoshindwa ni lazima utakimbilia ndani kuomba msaada.
Na kweli, ile dakika moja tu ya wewe kuingia ndani tu yeye anakuja kutoa kiasi ulichoomba wewe huku akitumia password yako ileile. Anacheza na
aisee
 
Mie kwa kumbu kumbu zangu katika hizi mashine niliwahi poteza laki mbili sijui niseme kwa ujinga wangu? Nilichomeka kadi nikaomba laki2 wakati nasikia mashine ikihesabu umeme ukakatika. Ikatoka kadi tu pesa haikutoka ikabidi nimuulize askari mlinzi pale yale mazingira na kama yatakua na athari kwangu. Akawa amenijibu kuwa haina shida na itakuwa haikutoa pesa kutoka ktk account yangu. Nikaondoka na siku ile niliamua kubadili pesa ya kigeni niliyokua nayo kwa ajili ya matumizi. Nilisafiri na baada ya kama wiki tatu nilirudi na nilipoingia katika atm machine kutoa pesa niligundua balance iliyokuwepo ilikua imepungua laki mbili kwa salio langu la mwisho kutoa pesa.
itakua umeme ulivyorud pesa ikatoka akajifaidia mlinzi
 
Back
Top Bottom