Staili nyingine ya wizi ATM

Staili nyingine ya wizi ATM

Nimekusoma! Pole sana,nenda kwy bank inayomiliki hiyo atm uwashitaki cz wanapaswa kua na mlizi na pia wanatumia cctv kumonitor watu kwy izo atm kwa iyo wapo liable na usalama wa fedha zako!
 
Tuendelee kujihadhari sana tunapoingia vibanda vya ATM hasa ukikuta mtu stranger

Hii ni simulizi.......

Nimeingia ATM nataka kutoa pesa anaingia mdada na kuniuliza maswali kadhaa, najaribu kutoa fedha zinagoma baada ya muda nakuta nikihangaika kutafuta ATM nyingine nakuta fedha zmekombwa

Yaani nashindwa hata kuandika zaidi kilichotokea mbaya zaidi nakuta hata kadi si ile yangu na ni mpya kabisa ikionesha ni maaum kwa kuibia

Kwa sababu uchunguzi unaendele sitaweka data zote humu ila muhimu kushirikishana uzoefu kwa waliokumbwa na masaibu kama haya
Hii haina mantiki yeyote na wala haieleweki mara mdada, ushungi helezimekwama. Ww ni mgeni kwa matumizi ya ATM.
 
Jamani wizi huo upo, kuna ndg yangu kaibiwa hela zote kwenye account yake ambapo alienda kutoa hela kwenye atm na akamkuta dada mmoja mfupi kiasi, mweupe, mwembamba na alikuwa kavaa ushungi, huyo dada alikuwa anahangaika kutoa hela kwenye atm jirani na aliyoitumia ndg yangu. Anadai yy aliingiza kadi yake kwenye mashine akatoa kiasi cha fedha alichohitaji na kadi ikatoka, pasipo kuangalia akaweka kadi yake kwenye wallet. Baada ya siku kadhaa kaenda kutoa hela kwenye atm na kadi ambayo si yake bila mwenyewe kujua, alipoingiza password ikagoma so akaingia ndani kulalamika, si ndio kushangaa kadi si yake, kuomba bank statement akakuta pesa zishalambwa, na alipoomba kuona picha akaambiwa camera ni mbovu, alipoomba benk wamlipe kaambiwa ukiibiwa kupitia kwa macashier wa bank unaweza kulipwa lakini ukiibiwa kwenye atm au simbanking hulipwi kwani huo ni uzembe wako. Tukio hili limetokea moro
 
Acha kulia lia mwanaume,, katafute zingine,,
Ussiombe yakukute kijana, mtu kahustle kibubu kimeshiba halafu mpuuzi anakuja kulamba kilaini usawa wenyewe huu..?

Wale maafande kwenye vibanda vyao wamekuwa wakijifungia baada ya lile tukio lilopita siku chache, bila kujali usalama wa wateja na pesa zao.
 
ATM zipi?
za umoja switch?
visa?

mimi pia kuna kitu nime experience leo nasubiri jumatatu nika confirm kitu
 
AISEEEEE
Jamani wizi huo upo, kuna ndg yangu kaibiwa hela zote kwenye account yake ambapo alienda kutoa hela kwenye atm na akamkuta dada mmoja mfupi kiasi, mweupe, mwembamba na alikuwa kavaa ushungi, huyo dada alikuwa anahangaika kutoa hela kwenye atm jirani na aliyoitumia ndg yangu. Anadai yy aliingiza kadi yake kwenye mashine akatoa kiasi cha fedha alichohitaji na kadi ikatoka, pasipo kuangalia akaweka kadi yake kwenye wallet. Baada ya siku kadhaa kaenda kutoa hela kwenye atm na kadi ambayo si yake bila mwenyewe kujua, alipoingiza password ikagoma so akaingia ndani kulalamika, si ndio kushangaa kadi si yake, kuomba bank statement akakuta pesa zishalambwa, na alipoomba kuona picha akaambiwa camera ni mbovu, alipoomba benk wamlipe kaambiwa ukiibiwa kupitia kwa macashier wa bank unaweza kulipwa lakini ukiibiwa kwenye atm au simbanking hulipwi kwani huo ni uzembe wako. Tukio hili limetokea moro
 
Hivi walipoleta mobile money hamjaelewa kazi yake, siongelei kwa lililomkuta huyu, mtu unatoa 50elf mpka ukapange foleni bank??
 
Uzi unasikitisha kwa jambo lililokupata ila mtiririko wako hauleweki kabisa,anyway nakusamehe najua itakuwa kwa vile ulipagawa kukuta mkwanja wote hamna,ila next time andika kwa utulivu ujumbe na elimu ifike vizuri.
 
Hili tatizo lilinipata NMB ATM Segerea mwisho. Nikafuatilia, Branch. Nikajazishwa fomu. Pesa zikarudishwa. Baada ya wiki kiasi kilichorudishwa kikazuiwa kwa madai kuwa walirudisha kimakosa. Walidai ATM Yao haikutoa fedha nilipofanya transactions, bali kuna transactions nilozofanya CRDB ATM kwa NMB Master card ndizo zilizokuwa effected. Hivyo nikajaza fomu nyingine kudai fedha kwa maelezo kuwa nilitoa hela kupitia CRDB. Nachokumbuka nilifanya transaction 3. Kati ya hizo 2 zilikuwa kwenye NMB ATMs na 1 CRDB ATM. Zote ziligoma kutoa pesa. ATM za NMB zilinipa ujumbe kuwa hakuna mawasiliano. Nilipoenda CRDB nikapewa ujumbe kuwa fedha hazitoshi. Nikauliza salio, ndipo nikagundua fedha ilishakatwa kule kwanye NMB ATM.Nilikuwa na shida kubwa , nikaona nitoe kiasi kilichosalia kinisaidie. Nikaambiwa mwenye kadi hapatikani. Nikaenda branch wakathibitisha fedha kukatwa lakini hawakuwa na namna kwakuwa hizo ATM hazipo chini yao. Wakanielekeza niende mjini. Ilikuwa jioni na ni ijumaa. Hivyo nikawa mpole mpaka jumatatu. Nilipofika nikajaza fomu mbili . Ya kwanza kwaajili ya transactions za NMB ATMs na nyingine kwaajili ya CRDB ATM. Utaratibu ni kujaza transaction moja moja kisha unaweka jumla ya fedha. Nilifanya hivyo. Baada ya wiki fedha zikarudishwa. Wiki nyingine baadae Ile fedha ikazuiliwa kwa madai kuwa ilirudishwa kimakosa. Nimeshajaza fomu nasubiri tena kurudishwa fedha zangu.
 
Tuendelee kujihadhari sana tunapoingia vibanda vya ATM hasa ukikuta mtu stranger

Hii ni simulizi.......

Nimeingia ATM nataka kutoa pesa anaingia mdada na kuniuliza maswali kadhaa, najaribu kutoa fedha zinagoma baada ya muda nakuta nikihangaika kutafuta ATM nyingine nakuta fedha zmekombwa

Yaani nashindwa hata kuandika zaidi kilichotokea mbaya zaidi nakuta hata kadi si ile yangu na ni mpya kabisa ikionesha ni maaum kwa kuibia

Kwa sababu uchunguzi unaendele sitaweka data zote humu ila muhimu kushirikishana uzoefu kwa waliokumbwa na masaibu kama haya
Mkuu umekula maharage ya wapi mbona hueleweki?
 
sijui kama tanzania mnatumia hii system bt huku SA me siendi kudraw pesa kwa ATM huwa nakwenda supermarket then nanunua Gazeti or Juice then ninapokwenda kulipia huwa natoa kadi yangu na kufanya hivi:-mfano total amount ya juice na gazeti ni TSh3000 basi mimi nalipa kwa Tsh200000 ili nirudishiwe chenchi Tshs197000 ambazo nilikuwa ndo nazihitaji kwa matumizi zangu binafsi. Hii imenisaidia sana cz hata pesa zikipotea najuwa wapi nitakwenda malalamiko na pia tuwe makini na ATM za barabarani sio safe kabisa.
 
kama nilivyosema sikuweka wazi kwa sababu kuna details nimezihifadhi kwanza sababu bado anafutalia
Uzi unasikitisha kwa jambo lililokupata ila mtiririko wako hauleweki kabisa,anyway nakusamehe najua itakuwa kwa vile ulipagawa kukuta mkwanja wote hamna,ila next time andika kwa utulivu ujumbe na elimu ifike vizuri.
 
sijui kama tanzania mnatumia hii system bt huku SA me siendi kudraw pesa kwa ATM huwa nakwenda supermarket then nanunua Gazeti or Juice then ninapokwenda kulipia huwa natoa kadi yangu na kufanya hivi:-mfano total amount ya juice na gazeti ni TSh3000 basi mimi nalipa kwa Tsh200000 ili nirudishiwe chenchi Tshs197000 ambazo nilikuwa ndo nazihitaji kwa matumizi zangu binafsi. Hii imenisaidia sana cz hata pesa zikipotea najuwa wapi nitakwenda malalamiko na pia tuwe makini na ATM za barabarani sio safe kabisa.
wezi wana mbinu nyingi sana
 
Alikuuliza maswali yap?
kwani unataka kutoa pesa nyingi> kitu gani umekwama:> na inaonekana walikua wengi kwani wakati anatakla tu kutoka likainia jibaba ilihali yule dada akiwa mle ndani
 
Back
Top Bottom