"Square Peg In A Round Hole"-ELIMU NI NINI?

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,990
22,523
Nitakwenda na kuileta ile hotuba ya Mbeki pale mlimani alipoweka wazi kuwa matatizo ya Afrika yanasababishwa na wale wenye ELIMU!

Kauli ya MBEKI ni NZITO na ya kutafakari kwani alipoitowa pale mlimani kwa masaa mawili mfululizo bila kupumzika alionyesha kukerwa sana na mikataba ambayo tumeingia na MAKABURU wa nchini mwake ambao hata sisi tuliwasaidia kumpinga na kumwondoa madarakani.

NI WAZI KUWA MADAI YAKE NI YA WAZI KUWA UMASIKINI WETU NA UFUKARA,MAGONJWA NA NJAA VIMESABABISHWA NA WENYE ELIMU.

Sasa naomba tuanze na mjadala huu...JE ELIMU NI NINI?
 
Hotuba hiyo hapo chini ni ya MBEKI kwa wasomi kabla hata sisi hatujajuwa vizuri kuhusu kashfa za UFISADI!
Ni wazi yeye alikuwa na data zaidi yetu na ndio maana alikuwa na MACHUNGU MWANA HUYU WA AFRIKA ALIYEMSHINDA JK NA MAMLUKI WENGINEO WA MZUNGU NA MWARABU!
Swali linabaki pale pale...ELIMU NI NINI?
Naomba mchangiaji usioigope kutowa jibu...Towa jibu based on your understanding..Ni swali linaloweza kuwapa hata maprofessa shida...Ila hapa jf hatuogopi kutowa mawazo yetu kwa UHURU...
Kutokana na ukweli kuwa mafisadi almost all of them are EDUCATED...THE....What is EDUCATION?

__________________
 
Na kwa kuanzia mimi mwenyewe binafsi..Kabla sijaelezea maana halisi ya square peg in a round hole...Mimi naona nitowe kile ambacho nimejifunza kwamba elimu ni nini... na pia naomba nikosolewe kwani mjadala huu ni MUHIMU SANA....

BINAFSI NASEMA ELIMU NI MWENDELEZO WA KIJAPI.
 
Hapa nimeona kimya...Ina maana hakuna mwenye definition yake ya kuwa elimu ni nini?
Je kati ya kipaji na elimu...Kipi hutangulia?
Na kipi hutoa mwongozo pale inapokuja kwenye uamuzi wa direction ya future yako?
Kama kuna mwenye maoni...
 
Mwalimu alitufundisha kuwa..ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA...Je kama tukiamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha yetu sisi kama watu binafsi..Ni kivipi tutaweza kuamini kuwa elimu hiyo hiyo ni ufunguo wa maisha ya kila mtu bila kujali utofauti wao wa kabila,dini na hata rangi?
Je...Elimu ni nini?
 
Inawezekana hoja yangu kuwa elimu ni mwendelezo wa kijapaji imekubalika na wengi.

Na kwasababu hiyo basi...Naomba niwaase wazazi na vijana jambo moja...Kuwa kabla huja amuwa kuwa ni mchepuo gani wa elimu wa kuchukuwa...Jaribu kufanya utafiti kuhusu kipaji chako...Kwani wakati huu vipaji ndio hulipa watu...Mfano ni michezo,biashara,udokta,siasa nk.

Kama jamii yetu ikijipanga upya kwa kuzingatia hayo...Basi tutaepuka ile dhana ya square peg in a round hole...Kwa maana square haiwezi kufiti kwenye tundu la mduara...Ni vitu viwili tofauti...Utakuta watu wana vipaji vya tofauti lakini wanakwenda kusomea mambo ya tofauti kwasababu tu anachosomea ndio kina lipa kwa kupata kazi kiurahisi.

Na hapo ukiangalia kwa makini wenye uwezo wa kusoma ni wachache...Wengi wao wazazi wao ni matajiri ama viongozi wa nchi.

Vipaji Tanzani na Afrika vimezikwa moja kwa moja kwa sababu hiyo hapo juu.

Kwasababu tukijiuliza swali la msingi tutakuja kugunduwa kuwa kipaji cha wafanya biashara kilianza kabla hata ya slylabus ya bishara.

Mfano halisi ni Batter trade...Utakuta kuwa watu walikuwa wakifanya mambo base on specialization.

Hatuwezi kui apply dhana ya specialization kwenye karne hii ya 21...Lakini tunaweza kujifunza yale positive ya kimsingi...Kwamba kipaji mtu huzaliwa nacho...Na mtu anaweza kutumia elimu kukiendeleza kipaji chake badala ya kwenda na kusomea yale asiyokuwa na kipaji nacho....

To be continued...
 
Elimu ni ile uliyoipata inayokuwezesha kuwa raia bora wa dunia.
kujali maumbile uliyoyakuta na utakayoyaacha.
kujua nafasi na wajibu wako ktk ulimwengu.
inayokuwezesha kuyapa umuhimu hahitaji yako na ya walimwengu wengine.
inajifunzwa tangu unapozaliwa mpaka unapokufa.
Mbeki alimaanisha tumewapa nchi watu wasio na elimu, bali wenye nafasi na pesa za kudanganya watanzania,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…