Spika wa wanafunzi ahamia CCM amekihama CHADEMA; Asema kwa sasa CHADEMA hakina dira

Kajimaliza mwenyewe, afadhali angeanza mambo hayo akiwa amemaliza shule. NYAMBAFUUUUUUUU
 
Waswahili wanasema "ukiwa mnafikiri ukiwa kijana,ukizeeka unakuwa mchawi".Pole rafiki yangu Mwangomango.Mara ya kwanza ulipokuwa unaongea kwenye runinga kuhusu kuhamia CCM,nilishangaa kiana na nikakutumia sms ikisema "hongera rafiki yangu kwa urudi CCM".Najua kinachokupeleka CCM sio dira ila unataka kupunguza makali ya maisha.Kutokana na maisha kuwa mazonge na vijana kutotaka kujihangaisha matokeo yake na kama alivyofanya Mwangomango.CHADEMA haiwezi kuyumba kwa kuondoka kwake.Simdharau,lakini Mwangomango ni nani katika siasa za bongo?Kinachoniuma mimi ni jinsi tunavyodhalilisha taaluma zetu,na kuonenya kuwa madarasa mengi tuliyoyapitia ni kupoteza muda.Nenda Mwangomango,Nenda.

nilionana na Mwangomango jumatano nikiwa na nakala ya Mwanahalisi yenye kichwa cha habari" Slaa akwamisha mpango wa JK wa kujivua gamba", alilisoma kwa dakika chache, na akashindwa kukoment chochote, jamaa kaingia choo cha kike
 
Mwangomango?!!!! ni nani ktk JF si ni kinyago tu?! acheni kuzungumzia watu wapumbavu! mnapoteza muda wenu!
 
Watu kama hawa mimi ndio huwa nawaita "pseudoacademician"! ningefurahi kama angejiuzulu na uspika kwa sababu nafahamu katika bunge la wanafunzi analoongoza kuna watu makini, so watu makini hawawezi kuongozwa na vilaza kama huyu!
 
Watu kama hawa mimi ndio huwa nawaita "pseudoacademician"! ningefurahi kama angejiuzulu na uspika kwa sababu nafahamu katika bunge la wanafunzi analoongoza kuna watu makini, so watu makini hawawezi kuongozwa na vilaza kama huyu!

alishajiuzulu
 
Hawa watoto wanasoma muda gani Kama wanashiriki na siasa?

Njaa tu, wawe CCM au upinzani, wangekuwa wanaipenda nchi hii wangeweka juhudi kwenye masomo kwa kuwa taifa linajinyima kuwasomesha, mwl nyerere aliwahi kuwaita watu hao wanaotumia rasilimali kidogo za taifa kujinufaisha wao binafsi kama wasaliti wa jamii yao.
 
Kila mtu ana haki yake ambayo ndiyo demokrasia.ila kwa mwana halisi ya maaendeleo unaweza kwa muda mfupi kutumia kupima mabadiliko na matokeo ya mabadiliko ili kuweza kufikia maamuzi yaliyo madhubuti,hivyo siwezi kujua nini kilimshawishi kufanya maamuzi hayo magumu kama chama kilivyoamuua kufanya.dira iliyokuwa imemweka alipokuwa sasa imebadilika,basi huko dira ni hilo gamda tu au nakadhalika
 
Ni ridhaa yakje kufanya hivyo,japo kunaweza kukawepo kamsukumo fulani kalikompeleka huko-tumbo
 
Kama "USOMI" Ndio huu tena wa Chuo Kikuu,kwa sababu ulizozitoa hakuna haja ya vyama vya siasa kuinvest ktk higher institutions! Je hili nalo ni zao la shule za kata! Au ni kufikiri kwa kutumia tumbo? Dah! KAZI IPO!

Natumai ni kufikiri kwa kutumia tumbo !
 
Back
Top Bottom