Spika Ndugai, Mbunge Lissu bado anaendelea na matibabu. Mshahara wake usisimamishwe tafadhali

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Kwa kauli yake mwenyewe aliyoitoa kupitia Sauti ya Amerika almaarufu kama VoA, Mbunge Tundu A.M. Lissu bado anaendelea na matibabu na hivyo bado ni mgonjwa. Lissu amesema kuwa mnamo tarehe 20/2/2018 takribani majuma mawili yajayo atakuwa nchini Ubelgiji kwa upasuaji wa 23 mwilini mwake.

Kama ni taarifa kuhusu matibabu na maendeleo yake, Lissu ameitoa jana mbele ya Balozi Wilson Masilingi aliyekuwapo studioni na kushiriki mazungumzo ya jana. Kama hoja ya kiti cha Spika ni kutopata taarifa ya aliko, anachofanya na matibabu ya Lissu kwa ujumla, Lissu ameweka jambo hilo wazi jana. Kufanyiwa tena upasuaji kunamaanisha kuwa Lissu anaendelea na matibabu.

Kuhusu kurudi nyumbani Tanzania, alipoulizwa Lissu akasema kuwa pale ambapo madaktari wake watamwambia yuko vyema, atarudi. Kwakuwa anakwenda kufanyiwa upasuaji mwingine, Lissu bado ni mpokea matibabu na ataendelea kuwa karibu na hospitali na madaktari wake. Kama raia mwema wa Taifa hili, na kufuatia taarifa aliyoitoa Lissu kuhusu upasuaji, naomba mshahara wake usisimamishwe ili umsaidie.
 
Cha msingi speaker awasiliane na wadhamini wa TL kisha wadhamini wa TL watawasiliana na daktari wa TL awape ripoti kuhusu maendeleo ya TL kama amepona au LA asiendeshwe Kwa hisia aweke ukada pembeni hisia za kina msukuma kasheku zimesimama kwenye ukada zaidi,labda tu itungwe Sheria ukiwa mgonjwa uruhusiwi kuongea na vyombo vya habari. Na speaker anajua TL yuko wapi.Kumbuka dunia inajua inafatilia kila hatua na nadhani kuna nguvu kubwa sana iko nyuma ya TL ili jambo ni jepesi kwa macho ya kawaida. Kumnyima haki zake ni kuiamnisha dunia kumbe yote ni ya kweli aliyosema,check wamemnyima hadi haki zake.Busara itumike
 
Cha msingi speaker awasiliane na wadhamini wa TL kisha wadhamini wa TL watawasiliana na daktari wa TL awape ripoti kuhusu maendeleo ya TL kama amepona au LA asiendeshwe Kwa hisia aweke ukada pembeni hisia za kina msukuma kasheku zimesimama kwenye ukada zaidi,labda tu itungwe Sheria ukiwa mgonjwa uruhusiwi kuongea na vyombo vya habari. Na speaker anajua TL yuko wapi.Kumbuka dunia inajua inafatilia kila hatua na nadhani kuna nguvu kubwa sana iko nyuma ya TL ili jambo ni jepesi kwa macho ya kawaida. Kumnyima haki zake ni kuiamnisha dunia kumbe yote ni ya kweli aliyosema,check wamemnyima hadi haki zake.Busara itumike
Unafikiri ripoti ya matibabu binafsi ya mtu inatolewa kama mantonga ya bara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ile sio taarifa, kwake ilikuwa kama bahati mbaya kuisemea pale (sijui kama huyu mtu aliwahi japo kufikiri kuhusu kutoa taarifa, au kufanya kitu kama hicho). Ile haikuwa taarifa rasmi yeye mwenyewe anajua hilo, upo utaratibu maalumu wa kuwasilisha mambo ya msingi kama hayo, ila huyu mtu ni mjuaji na huwa anajitoa ufahamu kwa makusudi kabisa!. Eti leo hii mtu atoe taarifa bila kufuata utaratibu tena taarifa yenyewe itolewe wakati wa mabishano ni ajabu sana kama tutamsikia na yeye akisimamia hoja yako hii kukubali ile ni taarifa. Ile sio taarifa, ule ni uhuni!
 
Kwa kauli yake mwenyewe aliyoitoa kupitia Sauti ya Amerika almaarufu kama VoA, Mbunge Tundu A.M. Lissu bado anaendelea na matibabu na hivyo bado ni mgonjwa. Lissu amesema kuwa mnamo tarehe 20/2/2018 takribani majuma mawili yajayo atakuwa nchini Ubelgiji kwa upasuaji wa 23 mwilini mwake.

Kama ni taarifa kuhusu matibabu na maendeleo yake, Lissu ameitoa jana mbele ya Balozi Wilson Masilingi aliyekuwapo studioni na kushiriki mazungumzo ya jana. Kama hoja ya kiti cha Spika ni kutopata taarifa ya aliko, anachofanya na matibabu ya Lissu kwa ujumla, Lissu ameweka jambo hilo wazi jana. Kufanyiwa tena upasuaji kunamaanisha kuwa Lissu anaendelea na matibabu.

Kuhusu kurudi nyumbani Tanzania, alipoulizwa Lissu akasema kuwa pale ambapo madaktari wake watamwambia yuko vyema, atarudi. Kwakuwa anakwenda kufanyiwa upasuaji mwingine, Lissu bado ni mpokea matibabu na ataendelea kuwa karibu na hospitali na madaktari wake. Kama raia mwema wa Taifa hili, na kufuatia taarifa aliyoitoa Lissu kuhusu upasuaji, naomba mshahara wake usisimamishwe ili umsaidie.
Pendekezo - Mshahara wa Lissu wapelekewe wakwe wa Ndugai ili maisha yao yabadilike .
 
Cha msingi speaker awasiliane na wadhamini wa TL kisha wadhamini wa TL watawasiliana na daktari wa TL awape ripoti kuhusu maendeleo ya TL kama amepona au LA asiendeshwe Kwa hisia aweke ukada pembeni hisia za kina msukuma kasheku zimesimama kwenye ukada zaidi,labda tu itungwe Sheria ukiwa mgonjwa uruhusiwi kuongea na vyombo vya habari. Na speaker anajua TL yuko wapi.Kumbuka dunia inajua inafatilia kila hatua na nadhani kuna nguvu kubwa sana iko nyuma ya TL ili jambo ni jepesi kwa macho ya kawaida. Kumnyima haki zake ni kuiamnisha dunia kumbe yote ni ya kweli aliyosema,check wamemnyima hadi haki zake.Busara itumike
Mihemuko inatusmubua sana juzi panya alikwa napanda kwenye meza ya kioo nilipo jaribu kumpiga nilivunja kioo
 
Je amefuata utaratibu wa ruhusa ya matibabu?

Wewe ingalau siyo mnafiki, umesimamia hili....

Sasa, badala yake mnaonaje hoja iwe hivi:

Kwa kuwa Tundu Lissu ameshapata nafuu, anaweza kuongea na hata kusafiri kidogo, basi afanye utaratibu wa "kujaza fomu za ruhusa", ziende kwa Jiwe, azipitie na kisha ampe ruhusa Ndugai kumpa ruhusa TL ikibidi na haki yake ya fedha za matibabu....!!

What about that, dude? In your opinion, do you think Jiwe (Bulldozer) can do that?
 
Back
Top Bottom