Spika Ndugai awaonya upinzani wasifukuze wabunge, awataka wajifunze kutoka CCM!

CCM watawavuwaje uanachama wabunge wake wakati wabunge hao wamekubali kuburuzwa na kukubaliana na kila matakwa ya wakubwa wao? Badala ya kuwalaumu wapinzani Ndugai ambaye ni Spika wa Bunge, aliongoze Bunge kubadili Kifungu kidogo (1) kifungu (b) kwenye Ibara ya 67 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Kifungu kidogo (1) Kifungu (f) cha Ibara ya 71 vinavyolazimisha wabunge watokane na vyama vya siasa na vyama vya siasa kupewa madaraka ya kumnyang'anya ubunge mtu kupitia kumtoa kwenye chama chao cha siasa.

Tatizo siyo vyama vya siasa bali katiba iliyovipa vyama vya siasa uungu wa kuumba na kuua ubunge wa mtu anayepingana na chama husika cha siasa!!
Unamaana wanaovuliwa wamekataa kuburuzwa ndani ya vyama vya upinzani,na kimsingi kuna usultani ndani ya vyama vya upinzani
 
Ndio hapo sheria ikitekelezwa mnalialia!Hakuna uhalifu unaotendeka bali ni sheria kuwa msumeno huacha maumivu makali mno!Huwezi pangs mikakati ya kukivuruga chama halafu uchekewe tu,"utafukuzwa tu"!Halafu sio kila jambo likiwa kwenye katiba ya JMT ndio liwe hivyo hivyo kwenye katiba za vyama!Umeelewa?
CHADEMA ni chama cha kiimla...tunamshukuru Mungu kayafunua haya...hakika..'nchi haiwezi kupewa walafi'
 
CHADEMA ni chama cha kiimla...tunamshukuru Mungu kayafunua haya...hakika..'nchi haiwezi kupewa walafi'
Tumeshawatambua humu,kuna baadhi yenu huwa akili zimeganda!Mnawaza kwa kutumia matumbo!Endeleeni na porojo zenu
 
Iga mazuri...la sivyo usilalamikie 'udikteta'...kumbe hammaanishi mnalosema na nyie ni wale wale tu....ndio maana kuna mahali nimekuambia viongozi wote wa upinzani ni ambao wamekosa fursa CCM...upinzani bado haikuwahi kuwa na viongozi kindakindaki.
Hapa hapana igizo, ni kutanabahisha tu kuwa"usicheke kundule" na lako vivyo!
 
Unamaana wanaovuliwa wamekataa kuburuzwa ndani ya vyama vya upinzani,na kimsingi kuna usultani ndani ya vyama vya upinzani
Ninachosema ni kuwa kwa upinzani inaonekana kwa kuwa wabunge wake huenda tofauti ya mitizamo ya viongozi wao. Kwa mfano watu waliwashangaa kina Nchimbi kutoka kwenye ukumbi wa mikutano kwa kuwa si utamaduni wa CCM. Tofauti ya CCM na upinzani ni kuwa kwenye CCM wana nidhamu ya woga wakati wenzao wa Upinzani wanakubali kuwa na mitizamo iliyotofauti.
 
Walimsifi kuwa Ndugai ndiye suluhisho la wanaukuta kurudi bungeni,jana kawakosoa masultani wa vyama hivyo kuacha kufukuza fukuza wabunge...wameanza kushupaza shingo.Sasa hivi utawasikia ''Bora ya Dr.Tulia''
mkuu Mansoor alikuwa chama gani?, je mwanasheria mkuu kipindi cha bunge la katiba???...........na huyu kiara wamwafaka wa zenji jee!,......
 
Ninachosema ni kuwa kwa upinzani inaonekana kwa kuwa wabunge wake huenda tofauti ya mitizamo ya viongozi wao. Kwa mfano watu waliwashangaa kina Nchimbi kutoka kwenye ukumbi wa mikutano kwa kuwa si utamaduni wa CCM. Tofauti ya CCM na upinzani ni kuwa kwenye CCM wana nidhamu ya woga wakati wenzao wa Upinzani wanakubali kuwa na mitizamo iliyotofauti.
 
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Jana aliwaonya viongozi wa vyama vya upinzani waache tabia yao ya usultani kufukuza uanachama wabunge wanaotofaitiana nao. Amesema hayo huku akiwakumbusha Mbunge ni mwakilishi wa wananchi na kama akifukuzwa uanachama basi atapoteza sifa ya kuwa mbunge na kuwakosesha uwakilishi wananchi.

Amewaasa wajifunzi kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) jinsi wanavyoshughulikia nidhamu za wabunge wao ambao wanaenda kinyume na maamuzi ya chama. Ni CCM pekee ambayo haijawahi kumvua mbunge uanachama kwa kutofautiana na Uongozi. Hivi majuzi CUF imewafutia uanachama wabunge wake Sakaya na Maftah,katika Bunge lililopita Hqamad Rashid alifutwa uanachama akaelekea mahakamani, CHADEMA walimfukuza Zitto Kabwe na NCCR-Mageuzi walimfutia uanachama David Kafulila kabla ya kufanya usuluhishi.

Ndugai katoa somo na kwa tabia hii ni dhahiri viongozi wa vyama vya upinzani hawataki kukosolewa,wanakumbatia usultani na ufalme.
Katika CCM tuna Kukolimba, tuna Kusokoine, au tuna Kumaalim.
 
Back
Top Bottom