Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,899
Hata hivyo Spika Makinda alielezea jinsi anavyokerwa na baadhi ya wasomi ambao huwapotosha wananchi kuhusu Muswada wa kuundwa kwa tume itakayoratibu mchakato wa wananchi kutoa maoni kuhusu Katiba mpya.
Alisema wasomi hao ambao wamesoma robo ya elimu inayohitajika, wamelenga kufanya upotoshwaji ili wananchi waamini kwamba Serikali imeandaa Muswada wa Katiba mpya jambo ambalo halikuwa na ukweli wa aina yoyote.
Alisema Muswada ambao ulisababisha baadhi ya wasomi kuzomea bila kujua nini kimeandikwa, ulikusudia kupata maoni ya wananchi juu upatikanaji wa tume hiyo kulingana na mapendekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
"Baadhi ya wasomi wetu wamepata elimu robo robo, wameshindwa kuelewa Muswada unataka nini….hawa ni watu wa kuelimisha wananchi kweli, wengine wanazomea kiholela tu bila kuusoma vyema," alisema.
Alisema Muswada huo uliwasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge, lakini kabla haujasomwa mara ya pili wananchi walipata fursa ya kutoa maoni katika vituo vya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, lakini kuliibuka vurugu zilizosababisha kurejeshwa serikalini.
Hata hivyo alisema Kamati za Bunge zilizokuwa zikiratibu maoni hayo zilipata maoni mengi ambayo yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha Taifa linapata utaratibu ambao utasaidia upatikanaji wa Katiba mpya.
Source: Habari leo - Makinda: sitishiki, natumia busara
Alisema wasomi hao ambao wamesoma robo ya elimu inayohitajika, wamelenga kufanya upotoshwaji ili wananchi waamini kwamba Serikali imeandaa Muswada wa Katiba mpya jambo ambalo halikuwa na ukweli wa aina yoyote.
Alisema Muswada ambao ulisababisha baadhi ya wasomi kuzomea bila kujua nini kimeandikwa, ulikusudia kupata maoni ya wananchi juu upatikanaji wa tume hiyo kulingana na mapendekezo ya Rais Jakaya Kikwete.
"Baadhi ya wasomi wetu wamepata elimu robo robo, wameshindwa kuelewa Muswada unataka nini….hawa ni watu wa kuelimisha wananchi kweli, wengine wanazomea kiholela tu bila kuusoma vyema," alisema.
Alisema Muswada huo uliwasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge, lakini kabla haujasomwa mara ya pili wananchi walipata fursa ya kutoa maoni katika vituo vya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, lakini kuliibuka vurugu zilizosababisha kurejeshwa serikalini.
Hata hivyo alisema Kamati za Bunge zilizokuwa zikiratibu maoni hayo zilipata maoni mengi ambayo yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha Taifa linapata utaratibu ambao utasaidia upatikanaji wa Katiba mpya.
Source: Habari leo - Makinda: sitishiki, natumia busara