Spika Makinda awadhalilisha wasomi wanasheria

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,899
Hata hivyo Spika Makinda alielezea jinsi anavyokerwa na baadhi ya wasomi ambao huwapotosha wananchi kuhusu Muswada wa kuundwa kwa tume itakayoratibu mchakato wa wananchi kutoa maoni kuhusu Katiba mpya.

Alisema wasomi hao ambao wamesoma robo ya elimu inayohitajika, wamelenga kufanya upotoshwaji ili wananchi waamini kwamba Serikali imeandaa Muswada wa Katiba mpya jambo ambalo halikuwa na ukweli wa aina yoyote.

Alisema Muswada ambao ulisababisha baadhi ya wasomi kuzomea bila kujua nini kimeandikwa, ulikusudia kupata maoni ya wananchi juu upatikanaji wa tume hiyo kulingana na mapendekezo ya Rais Jakaya Kikwete.

"Baadhi ya wasomi wetu wamepata elimu robo robo, wameshindwa kuelewa Muswada unataka nini….hawa ni watu wa kuelimisha wananchi kweli, wengine wanazomea kiholela tu bila kuusoma vyema," alisema.

Alisema Muswada huo uliwasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge, lakini kabla haujasomwa mara ya pili wananchi walipata fursa ya kutoa maoni katika vituo vya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, lakini kuliibuka vurugu zilizosababisha kurejeshwa serikalini.

Hata hivyo alisema Kamati za Bunge zilizokuwa zikiratibu maoni hayo zilipata maoni mengi ambayo yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha Taifa linapata utaratibu ambao utasaidia upatikanaji wa Katiba mpya.

Source: Habari leo - Makinda: sitishiki, natumia busara
 
"Baadhi ya wasomi wetu wamepata elimu robo robo, wameshindwa kuelewa Muswada unataka nini….hawa ni watu wa kuelimisha wananchi kweli, wengine wanazomea kiholela tu bila kuusoma vyema," alisema.

Source: Habari leo - Makinda: sitishiki, natumia busara

Sishangai kwani elimu yake inamruhusu kutoa comment za aina hii kutokana na upeo wake finyu unaotokana na elimu yake duni!! Ref: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/87236-anne-semamba-makindas-profile-2.html
 
Huyo bibie bwana lakini wenye elimu robo robo hiyo ndiyo iliyolifanya bunge lihairishe kuujadili
 
Kwa hiyo hiyo Advance Diploma yake ndo elimu ya juu kuliko wote? Bi Kiroboto kweli hazimtoshi!
 
Kwa hiyo hiyo Advance Diploma yake ndo elimu ya juu kuliko wote? Bi Kiroboto kweli hazimtoshi!

Hii ndio elimu anayojivunia na kuwadhalilisha wanasheria mahiri kuwa ni roborobo? Angalia kiwango cha elimu yake hapo unaweza fikiri atawaelewa wenye elimu juu yake?

Anne Semamba Makinda's Profile!​
EDUCATIONAL HISTORY
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Development & Management - Morogoro Administration Course 1971 1975 ADV DIPLOMA
Kilakala Girls' Secondary School(Marian College) A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Masasi Girls' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Peramiho Girls' Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Uwemba Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY
 
Hii ndio elimu anayojivunia na kuwadhalilisha wanasheria mahiri kuwa ni roborobo? Angalia kiwango cha elimu yake hapo unaweza fikiri atawaelewa wenye elimu juu yake?

Anne Semamba Makinda's Profile!​
EDUCATIONAL HISTORY
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Development & Management - Morogoro Administration Course 1971 1975 ADV DIPLOMA
Kilakala Girls' Secondary School(Marian College) A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Masasi Girls' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Peramiho Girls' Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Uwemba Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY

Mwenye elimu ya uhakika huheshimu elimu walizonazo wenzi au anaofanya kazi nao, lakini ukiona mtu anadharau kiwango cha elimu ya walio juu yake kwa kiwango ujue ameishiwa na anachofanya sasa ni hoja ya nguvu kuendesha bunge badala ya nguvu ya hoja.
 
Juzi nilimsikia Spika wa zamani wa Bunge la Tz,Pius Msekwa akisema kwamba yeye alipokuwa Spika ilibidi ARUDI SHULE KUSOMA SHERIA, yaani Bachelor Degree of Law ili aweze kulisimamia na kuliendesha Bunge kwa ufanisi.

Sasa huyu Kibibi Semamba Makinda aliyewekwa kwenye Usipika na Mafisadi al-maarufu Mapacha matatu EL,RA na AC ataliweza Bunge hili wakti hana hata Cheti cha mambo ya Sheria?????

Mimi naona Bunge lipige KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA SPIKA maana kwa kweeeri anatia kichefuchefu na aibu tupu.

Aondoke akaungana na yale Magamba mennzake waliomweka kwenye nafasi hiyo.
 
Mbona kwenye hayo maelezo hapo juu hasemi ukweli ni upi sasa kama wasomi walikuwa wanawapotosha wananchi? Watu wengine bana,... wanavaa mavazi makubwa kuliko size zao!
 
Hivi wakati anaongea na huyu mwandishi wa gaezeti la HL walikuwa wapi na mama Makinda alikuwa na hali gani kichwani manake naona haya majibu kama ya mlevi tena akiwa baa:A S 39:
 
Juzi nilimsikia Spika wa zamani wa Bunge la Tz,Pius Msekwa akisema kwamba yeye alipokuwa Spika ilibidi ARUDI SHULE KUSOMA SHERIA, yaani Bachelor Degree of Law ili aweze kulisimamia na kuliendesha Bunge kwa ufanisi.

Sasa huyu Kibibi Semamba Makinda aliyewekwa kwenye Usipika na Mafisadi al-maarufu Mapacha matatu EL,RA na AC ataliweza Bunge hili wakti hana hata Cheti cha mambo ya Sheria?????

Mimi naona Bunge lipige KURA YA KUTOKUWA NA IMANI NA SPIKA maana kwa kweeeri anatia kichefuchefu na aibu tupu.

Aondoke akaungana na yale Magamba mennzake waliomweka kwenye nafasi hiyo.

Jaribu kusoma kidogo saikoloji ya wanawake wakiishiwa hoja, na angalia anavyoendesha vikao vya bunge kwa kutumia mamlaka bila hoja na hoja inapomshinda anaishia kudharau watoa hoja eti wamesoma roborobo hii inaingia akilini kweli?

Ningemwona kama akili zake zimekaa vizuri kama anaibua hoja za kuwajibu watoa hoja sasa hii ya elimu robo robo ya kiwango cha sheria wakati yeye ana robo robo ya elimu ya sekondari tu na juu zaidi ni Advanced diploma huyo ndiye Speaker wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
No legal background please don't miss this point. Just a JK puppet and she end the same way she came in.
 
Hata hivyo Spika Makinda alielezea jinsi anavyokerwa na baadhi ya wasomi ambao huwapotosha wananchi kuhusu Muswada wa kuundwa kwa tume itakayoratibu mchakato wa wananchi kutoa maoni kuhusu Katiba mpya.

Alisema wasomi hao ambao wamesoma robo ya elimu inayohitajika, wamelenga kufanya upotoshwaji ili wananchi waamini kwamba Serikali imeandaa Muswada wa Katiba mpya jambo ambalo halikuwa na ukweli wa aina yoyote.

Alisema Muswada ambao ulisababisha baadhi ya wasomi kuzomea bila kujua nini kimeandikwa, ulikusudia kupata maoni ya wananchi juu upatikanaji wa tume hiyo kulingana na mapendekezo ya Rais Jakaya Kikwete.

"Baadhi ya wasomi wetu wamepata elimu robo robo, wameshindwa kuelewa Muswada unataka nini….hawa ni watu wa kuelimisha wananchi kweli, wengine wanazomea kiholela tu bila kuusoma vyema," alisema.

Alisema Muswada huo uliwasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge, lakini kabla haujasomwa mara ya pili wananchi walipata fursa ya kutoa maoni katika vituo vya Dodoma, Dar es Salaam na Zanzibar, lakini kuliibuka vurugu zilizosababisha kurejeshwa serikalini.

Hata hivyo alisema Kamati za Bunge zilizokuwa zikiratibu maoni hayo zilipata maoni mengi ambayo yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha Taifa linapata utaratibu ambao utasaidia upatikanaji wa Katiba mpya.

Source: Habari leo - Makinda: sitishiki, natumia busara


Kwa hiyo Mama Makinda anatuambia kuwa muswada ulikuwa mzuri kabisa shida ilikuwa ni uelewa mdogo wa 'wasomi robo robo'? Pengine angetoa ufanunuzi kwa nini yeye mwenyewe Makinda alikubali muswada utolewe (withdrawn) kama ulikuwa hauna shida? Niseme tu kitendo cha Mama Makinda, Werema, Wasira na wengine wengi kutoka CCM kuongelea muswada ambao umeondolewa bungeni ni aibu kwao na madaharau kwa wananchi kwamba tunaongozwa na watu wenye uelewa mdogo. Inakuwaje unasifia kitu ulichosema kwamba hakifai? Na ni hao wasomi robo-robo ndio wameonesha point moja baada ya nyingine juu ya nini hasa kibovu kwenye mswada. Sasa nani amesoma robo robo - aliyandaa mswada mbovu uliokatiliwa au hao walioonesha ubovu?
 
Alisema wasomi hao ambao wamesoma robo ya elimu inayohitajika, wamelenga kufanya upotoshwaji ili wananchi waamini kwamba Serikali imeandaa Muswada wa Katiba mpya jambo ambalo halikuwa na ukweli wa aina yoyote.

Wanasheria walao wamefikia kiwango cha roborobo, Spika wa Makinda hata kupitia tu walikopata wezake robo robo hakuna anachojifunia ni

Anne Semamba Makinda's Profile!

EDUCATIONAL HISTORY
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Development & Management - Morogoro Administration Course 1971 1975 ADV DIPLOMA
Kilakala Girls' Secondary School(Marian College) A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Masasi Girls' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Peramiho Girls' Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Uwemba Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY

Hakuna elimu ya sheria na anakabidhiwa jukumu la kuwa msimamizi wa watunga sheria ndio usanii wa ccm
 
Me namuongezea la asha ngedele

Huyu bibi Anna Roborobo Makinda mambo yanamshinda anaishia kudharau wanasheria na kesho watatumia taaluma yao anayoidharau kumwondoa kwa aibu kiti alichokalia, maana walimwoka madaraka wengi wameshaenguliwa.
 
Tanzania hatu fuatagi protocol hata siku moja. Speaker yeye ni kiongozi wa tawi moja la uongozi (Bunge) na serikali (Executive) nao wana viongozi wao. Tokea lini kiongozi wa tawi moja aka zungumza kwa niaba na kutetea tawi lingine? Serikali si ina raisi, si ina waziri mkuu, si ina waziri husika? Iweje yeye ndiyo atokeze kuzungumza hata. Tanzania separation of power na separation of party and state hakuna kabisa.
 
huyu mama ni jasiri kama kihiyo wa temeke, mimi nilijua hata kafika mwaka wa kwanza UNIVERSITY akadisco kumbe ni ile IDM-MZUMBE wakati ule wa ujimaa,
na hakutoboa baada ya hapo duh
hapa kazi tunayo


GENERAL

ID No.: 1268
Salutation: HONOURABLE
First Name: Anne
Middle Name: Semamba
Last Name: Makinda
Member Type: Constituency Member
Constituent: Njombe Kusini
Political Party: CHAMA CHA MAPINDUZI
Office Location: P.O. Box 38, Njombe
Office Phone:
Office Fax: 2112538
Office E-mail: amakinda@parliament.go.tz
Member Status: Current Member
Start Date:
End Date:
Date of Birth 15 July 1949

EDUCATIONAL HISTORY
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
Institute of Development & Management - Morogoro Administration Course 1971 1975 ADV DIPLOMA
Kilakala Girls' Secondary School(Marian College) A-Level Education 1969 1970 HIGH SCHOOL
Masasi Girls' Secondary School O-Level Education 1965 1968 SECONDARY
Peramiho Girls' Middle School Primary Education 1961 1964 PRIMARY
Uwemba Primary School Primary Education 1957 1960 PRIMARY

EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
- Regional Commissioner 1995 2000
Ministry of Community Development, Women Affairs and Children Minister 1990 1995
State,Prime Minister's & First Vice President Office Coordination of Union Matters 1983 1990
State,Prime Minister's & First Vice President Office In charge of Central Government Coordination 1983 1990
Tanzania Government In charge of Information and Broadcasting 1983 1990
State,Prime Minister's & First Vice President Office Minister 1983 1990
National Bank of Commerce Board Member 1978 1983
Surveyors Building Contractors Consultants Board Member 1978 1983
Tanzania Railways Corporation Board Member 1977 1983
Tanzania Legal Corporation Board Member 1977 1983
Mbeya Textile Company Board Member 1977 1983
National Textile Company Board Member 1976 1983
Tanzania Elimu Supplies Board Member 1976 1983
The Public Accounts Committee of the Parliament Member 1975 1983
Tanzania Audit Corporation Auditor 1975 1976
The Institute of Development Management-Mzumbe Board Member 1971 1976

POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
CCM-Chama Cha Mapinduzi Member of National Executive Council 1977 Todate
TANU/CCM-Chama Cha Mapinduzi Ten Cells Leader 1975 1983
TANU Chairman -Youth League-IDM, Mzumbe 1971 1975
TANU Chairman -Youth League-Kilakala 1969 1970
TANU Chairman of Youth League 1965 1968
 
Back
Top Bottom