Mwanamke mmoja anasema:
Nilifundisha watoto wangu kunikumbatia… katika nyakati tofauti za mchana.
Siku moja nikamwambia mwanangu:
“Nikumbatie kwa nguvu sana!”
Na kwa utani nikamwambia:
“Nisharge tafadhali, sina chaji!”
Akanijibu: “Sawa mama, sasa umeshakuwa na 1000%!”
Tangu siku hiyo, nikaanza kusema: “Nani atanisharge sasa?!”
Na wanaporudi kutoka shuleni, najifanya mlegevu…
Nawapokea kwa kumbatio la joto,
Na huwaambia: “Sijawaona tangu asubuhi… sina chaji, bado niko 55%!”
Kumbatio na je wajua nini maana ya kumbatio?
Kumbatio huvunja kila umbali kati yako na watoto wako.
Huleta furaha, utii, baraka ya watoto, na mapenzi yao kwako…
Huzidisha mapenzi baina ya wanafamilia na maelewano kati yao.
Huongeza homoni ya furaha, huboresha hisia na hutuliza nafsi kwa kuridhika.
Ni tiba ya maradhi yao — na watoto wanaopata kumbatio kutoka kwa mama zao hupona haraka zaidi kuliko wengine.
Huimarisha kinga ya mwili, huongeza akili za watoto, na huleta furaha ya ndani.
Ni uthibitisho mkubwa wa upendo na shauku — ni nguzo muhimu ya malezi.
Ushauri muhimu sana kwa akina mama:
Wakumbatieni watoto wenu mara kwa mara — kwani huwapa hisia ya usalama.
Na ujisikie kwamba kumbatio hilo linakuchaji kweli na linawachaji wao pia.
Lakini kinachopanda si asilimia ya chaji, bali ni asilimia ya furaha…
Ulimbeba miezi tisa tumboni,
Ulimbeba alipokuwa mchanga,
Endelea kumbeba hadi akue…
Kwa sababu kumbatio ni lishe muhimu kwa ukuaji salama na afya wa watoto wako…
Kwa kuwa linawafanya wahisi kuwa uko karibu nao.