Kwani huu umaskini umeanza leo au JK ndiyo kaingia kwenye 'uongozi' leo? Au alikuwa anangoja hadi awe Rais ndiye auone umaskini, halafu umnyime usingizi!
Pia inategemea umaskini wa 'watu wake wapi' anaouzungumzia!
Wale watu wake wanaopiga risasi wengine au wale watu wake wanopigwa risasi?
Watu wake wanaokula Richmond au watu wake wanaolizwa na madhara ya Richmond?
Watu wake (Msolla & Co) au watu wake (Wanafunzi wa Ukraine, UDSM, etc)?
Watu wake Nchimbi na Chitalilo (elimu fake) au watu wake wa-machinga (bora elimu na si elimu bora).
Kwa wenzangu hapo juu mnaolalamikia u-rais wa JK na kasoro zake, naona mna mantiki kuwa JK aliutaka u-rais ili aweze kuutumia ipasavyo.
Je, hakuna uwezekano kuwa labda JK aliutaka u-Rais just for the sake of kuwa Rais (Wajukuu waseme kuwa babu aliishawahi kuwa Rais wa Tanzania), bila kujua kuwa atafanya nini akiwa Rais?