Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 710
- 1,610
Kwa miaka mingi, Marekani na Israel zimekuwa na hofu kuwa Iran inatengeneza bomu la nyuklia. Israel anaamini bomu hilo likikamilika, Iran italitumia kuifuta nchi yao kwenye ramani, hivyo wamekuwa wakitafuta namna ya kuzuia mpango huo kwa nguvu.
madarakani Januari 20, 2025, aliweka msimamo mkali wa "Maximum Pressure". Alitaka Iran iache kabisa urutubishaji wa uranium na iharibu mitambo yake yote, jambo ambalo Iran ililiona kama ni kudhalilishwa na kupoteza uhuru wake.
Wiki iliyopita, nchi ya Oman ilijaribu kuwakutanisha Marekani na Iran ili kuzuia vita. Hata hivyo, Marekani ilitoa masharti magumu ambayo Iran iliyakataa katakata. Mazungumzo hayo yalivunjika rasmi tarehe 26 Februari, na wajumbe wa Iran wakagoma kuendelea na diplomasia.
Baada ya diplomasia kufeli, Marekani na Israel hazikusubiri. Siku ya Jumamosi, tarehe 28 Februari, zilianzisha operesheni kubwa ya anga. Walishambulia vituo vya nyuklia, kambi za jeshi, na makazi ya viongozi wa juu wa Iran mjini Tehran ili kuuvunja nguvu utawala huo mara moja.
Leo Machi 1 hali ni ya taharuki. Kuna ripoti kuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Khamenei, ameshambuliwa vibaya na kuuawa. Iran imekanusha na kujibu kwa kurusha makombora kuelekea Israel na kambi za Marekani. Dunia nzima ina hofu ya kuanza kwa Vita ya Tatu ya Dunia, huku bei ya mafuta ikipanda kwa kasi ya ajabu.
-----------
Israel imedai kuwa ilirusha zaidi ya mabomu 1,200 nchini Iran ndani ya siku moja, ambapo Jeshi la Anga la nchi hiyo limesema mashambulizi hayo yalifanyika kwa ushirikiano na Marekani.
Miongoni mwa maeneo yaliyoshambuliwa ni pamoja na shule ya msingi ya wasichana iliyopo Minab, katika jimbo la Hormozgan kusini mwa Iran, ambapo takribani watu 148 wameripotiwa kupoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa “makumi ya watoto wasio na hatia” waliuawa katika shambulio hilo la shule, na kusisitiza kuwa tukio hilo “halitapita bila kujibiwa.”
----------
Wizara ya Ulinzi ya Falme za Kiarabu UAE yathibitisha Iran kushambulia kwa Makombora
Iran ilirusha mamia ya makombora na droni kuelekea Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo, ikieleza kuwa jumla ya makombora 137 na droni 209 zilirushwa siku ya Jumamosi, huku mengi yakizuiliwa na mifumo ya ulinzi wa anga.
Katika tukio lililotokea kwenye uwanja wa ndege wa Abu Dhabi, mtu mmoja aliuawa na wengine saba kujeruhiwa baada ya mabaki ya vifaa vilivyodunguliwa kuanguka eneo hilo, wakati pia uwanja wa ndege wa Dubai—ambao ni miongoni mwa wenye shughuli nyingi zaidi duniani kwa safari za kimataifa—ulilengwa na mashambulizi hayo
------------
Viongozi wa Iran waliouawa katika shambulizi la Israel na Marekani
IRNA yatangaza shambulizi la Israel katika mji wa Tehran
Shirika la habari la Iran (IRNA) imeripoti milipuko mikubwa katika mji mkuu Tehran, ikisababisha sauti za mlipuko zikisikika maeneo ya Seyyed Khandan, viunga vya Qasr, Vanak Square na Barabara ya Motahari, huku moshi na uharibifu unaonekana kuibuka ikiwa ni baada ya Jeshi la Israel kutangaza kufanya mashambulizi ya makombora ya anga katikati ya mji wa Tehran.
-------------
Iran inaona kisasi kama jukumu na haki halali kufuatia mauaji ya Ayatollah- Amesema Rais wa Iran
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa kutafuta kisasi kwa kuuawa kwa Kiongozi Mkuu Ayatollah Ali Khamenei na maafisa wengine wa ngazi ya juu wa Iran ni “dharura na haki halali” ya nchi hiyo.
“Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona kuwa kutafuta haki na kulipiza kisasi kwa wale waliotekeleza na kuagiza uhalifu huu wa kihistoria ni dharura na haki halali, na itatumia nguvu zake zote kutimiza wajibu huu mkubwa,” alisema Rais Pezeshkian, akitoa pole zake.
--------------
Kiongozi mkuu wa usalama wa Iran ametoa onyo kuwashambulia Marekani na Israel kwa kishindo zaidi
“Jana Iran ilirusha makombora kuelekea Marekani na Israel, na yaliwadhuru,” alisema Larijani kwenye mtandao wa X.
“Leo tutawapiga kwa nguvu ambayo hawjawahi kuikumbuka hapo awali.”
Lugha yake ilikuwa kama onyo lililotolewa na Rais Donald Trump dhidi ya Iran siku hiyo hiyo.
“Iran imetangaza itapiga vikali leo, zaidi ya jinsi walivyowahi kupigwa hapo awali,” aliandika Rais Trump kwenye mitandao ya kijamii.
“Lakini bora wasifanye hivyo, kwani iwapo watafanya, tutawapiga kwa nguvu ambayo haijawahi kuonekana hapo awali!”
--------
PICHA: Raia wa Iran wameanza kukimbilia nchi jirani kwa usalama
People cross from Iran into Turkiye at Kapikoy border
------------
Updated: Idadi ya vifo yafika 8 na Majeruhi 27
......
Watu 4 wauawa kufuatia shambulizi la Iran katika mji wa Beit Shemesh, Israel
Watu wasiopungua wanne wameuawa na takribani 20 kujeruhiwa kufuatia shambulio la kombora la balestiki kutoka Iran katika mji wa Beit Shemesh, ulioko karibu kilomita 30 magharibi mwa Jerusalem
Jeshi la Israel limesema kupitia taarifa kwenye Telegram kuwa vikosi vya uokoaji na utafutaji, kwa kushirikiana na timu za matibabu pamoja na helikopta ya kuwahamisha majeruhi, vinaendelea na operesheni katika eneo lililopigwa.
----------
Wanajeshi 3 wa Marekani wauawa na 5 kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran
Jeshi la Marekani limethibitisha kuwa wanajeshi watatu wameuawa na watano kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran — vifo vya kwanza vya Marekani tangu mashambulizi yaanze, kwa mujibu wa Jeshi la Marekani limethibitisha kuwa wanajeshi watatu wameuawa na watano kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran — vifo vya kwanza vya Marekani tangu mashambulizi yaanze, kwa mujibu wa US Central Command (CENTCOM)..
Pia soma:
madarakani Januari 20, 2025, aliweka msimamo mkali wa "Maximum Pressure". Alitaka Iran iache kabisa urutubishaji wa uranium na iharibu mitambo yake yote, jambo ambalo Iran ililiona kama ni kudhalilishwa na kupoteza uhuru wake.
Wiki iliyopita, nchi ya Oman ilijaribu kuwakutanisha Marekani na Iran ili kuzuia vita. Hata hivyo, Marekani ilitoa masharti magumu ambayo Iran iliyakataa katakata. Mazungumzo hayo yalivunjika rasmi tarehe 26 Februari, na wajumbe wa Iran wakagoma kuendelea na diplomasia.
Baada ya diplomasia kufeli, Marekani na Israel hazikusubiri. Siku ya Jumamosi, tarehe 28 Februari, zilianzisha operesheni kubwa ya anga. Walishambulia vituo vya nyuklia, kambi za jeshi, na makazi ya viongozi wa juu wa Iran mjini Tehran ili kuuvunja nguvu utawala huo mara moja.
Leo Machi 1 hali ni ya taharuki. Kuna ripoti kuwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Khamenei, ameshambuliwa vibaya na kuuawa. Iran imekanusha na kujibu kwa kurusha makombora kuelekea Israel na kambi za Marekani. Dunia nzima ina hofu ya kuanza kwa Vita ya Tatu ya Dunia, huku bei ya mafuta ikipanda kwa kasi ya ajabu.
-----------
Israel imedai kuwa ilirusha zaidi ya mabomu 1,200 nchini Iran ndani ya siku moja, ambapo Jeshi la Anga la nchi hiyo limesema mashambulizi hayo yalifanyika kwa ushirikiano na Marekani.
Miongoni mwa maeneo yaliyoshambuliwa ni pamoja na shule ya msingi ya wasichana iliyopo Minab, katika jimbo la Hormozgan kusini mwa Iran, ambapo takribani watu 148 wameripotiwa kupoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa “makumi ya watoto wasio na hatia” waliuawa katika shambulio hilo la shule, na kusisitiza kuwa tukio hilo “halitapita bila kujibiwa.”
----------
Wizara ya Ulinzi ya Falme za Kiarabu UAE yathibitisha Iran kushambulia kwa Makombora
Iran ilirusha mamia ya makombora na droni kuelekea Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya nchi hiyo, ikieleza kuwa jumla ya makombora 137 na droni 209 zilirushwa siku ya Jumamosi, huku mengi yakizuiliwa na mifumo ya ulinzi wa anga.
Katika tukio lililotokea kwenye uwanja wa ndege wa Abu Dhabi, mtu mmoja aliuawa na wengine saba kujeruhiwa baada ya mabaki ya vifaa vilivyodunguliwa kuanguka eneo hilo, wakati pia uwanja wa ndege wa Dubai—ambao ni miongoni mwa wenye shughuli nyingi zaidi duniani kwa safari za kimataifa—ulilengwa na mashambulizi hayo
------------
Viongozi wa Iran waliouawa katika shambulizi la Israel na Marekani
- Ayatollah Ali Khamenei- Kiongozi Mkuu wa Iran (Supreme leader)
- Ali Shamkhani, - Mshauri wa masuala ya usalama (Khamenei’s security adviser)
- General Abdolrahim Mousavi,- Mkuu wa Majeshi Iran (Iran’s Armed Forces chief of staff)
- Aziz Nasirzadeh, - Waziri wa Ulinzi(Minister of Defence)
- Mohammad Pakpour, IRGC commander-in-chief
IRNA yatangaza shambulizi la Israel katika mji wa Tehran
Shirika la habari la Iran (IRNA) imeripoti milipuko mikubwa katika mji mkuu Tehran, ikisababisha sauti za mlipuko zikisikika maeneo ya Seyyed Khandan, viunga vya Qasr, Vanak Square na Barabara ya Motahari, huku moshi na uharibifu unaonekana kuibuka ikiwa ni baada ya Jeshi la Israel kutangaza kufanya mashambulizi ya makombora ya anga katikati ya mji wa Tehran.
-------------
Iran inaona kisasi kama jukumu na haki halali kufuatia mauaji ya Ayatollah- Amesema Rais wa Iran
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kuwa kutafuta kisasi kwa kuuawa kwa Kiongozi Mkuu Ayatollah Ali Khamenei na maafisa wengine wa ngazi ya juu wa Iran ni “dharura na haki halali” ya nchi hiyo.
“Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaona kuwa kutafuta haki na kulipiza kisasi kwa wale waliotekeleza na kuagiza uhalifu huu wa kihistoria ni dharura na haki halali, na itatumia nguvu zake zote kutimiza wajibu huu mkubwa,” alisema Rais Pezeshkian, akitoa pole zake.
--------------
Kiongozi mkuu wa usalama wa Iran ametoa onyo kuwashambulia Marekani na Israel kwa kishindo zaidi
“Jana Iran ilirusha makombora kuelekea Marekani na Israel, na yaliwadhuru,” alisema Larijani kwenye mtandao wa X.
“Leo tutawapiga kwa nguvu ambayo hawjawahi kuikumbuka hapo awali.”
Lugha yake ilikuwa kama onyo lililotolewa na Rais Donald Trump dhidi ya Iran siku hiyo hiyo.
“Iran imetangaza itapiga vikali leo, zaidi ya jinsi walivyowahi kupigwa hapo awali,” aliandika Rais Trump kwenye mitandao ya kijamii.
“Lakini bora wasifanye hivyo, kwani iwapo watafanya, tutawapiga kwa nguvu ambayo haijawahi kuonekana hapo awali!”
--------
PICHA: Raia wa Iran wameanza kukimbilia nchi jirani kwa usalama
People cross from Iran into Turkiye at Kapikoy border
------------
Updated: Idadi ya vifo yafika 8 na Majeruhi 27
......
Watu 4 wauawa kufuatia shambulizi la Iran katika mji wa Beit Shemesh, Israel
Watu wasiopungua wanne wameuawa na takribani 20 kujeruhiwa kufuatia shambulio la kombora la balestiki kutoka Iran katika mji wa Beit Shemesh, ulioko karibu kilomita 30 magharibi mwa Jerusalem
Jeshi la Israel limesema kupitia taarifa kwenye Telegram kuwa vikosi vya uokoaji na utafutaji, kwa kushirikiana na timu za matibabu pamoja na helikopta ya kuwahamisha majeruhi, vinaendelea na operesheni katika eneo lililopigwa.
----------
Wanajeshi 3 wa Marekani wauawa na 5 kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran
Jeshi la Marekani limethibitisha kuwa wanajeshi watatu wameuawa na watano kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran — vifo vya kwanza vya Marekani tangu mashambulizi yaanze, kwa mujibu wa Jeshi la Marekani limethibitisha kuwa wanajeshi watatu wameuawa na watano kujeruhiwa vibaya katika operesheni dhidi ya Iran — vifo vya kwanza vya Marekani tangu mashambulizi yaanze, kwa mujibu wa US Central Command (CENTCOM)..
Pia soma:
- Iran Imethibitisha Kuwa Kiongozi Mkuu, Khamenei ameuawa
- Israel yadai kwamba Ayatollah Khamenei ameuawa, kwa mujibu wa ripoti ya Channel 12 na Israel Media
- Trump: Watu wa Iran saa ya ukombozi imewadia. Kwa miaka mingi mmeiomba Marekani msaada lakini hamkuupata, Tutakapomaliza kazi yetu chukueni nchi yenu
- Israel na Marekani zaishambulia Iran. Serikali ya Israel yatangaza hali ya hatari
- Alireza Arafi ateuliwa na Baraza la Uongozi la Iran kushikilia nafasi ya Kiongozi Mkuu kwa muda
- Israel yadai kuua Makamanda 40 na kuharibu mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran