Sawa Basii Leo twende hatua nyingine ya kujifunza html katika hatua hii nitakueleza kutumia baadhi ya tag na kuunda page yetu yenye kichwa na maelezo na katika kipengele hiki ndio tutaanza kutumia tool ulizodownload kwa ajili ya coding na kuona matikeo
Katika nafasi iliopita siku elezea vizuri kuhusu tag ya title nilioweka katikati ya head tag <title>: Hii nitag ya kueleza kichwa cha mahudhui yaliopo katika page
Mfano katika codes hizi
HTML:
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title>Kichwa cha Mahudhui(Maelezo yangu binafsi)</title>
</head>
</html>
Ndugu hapo kwenye title unaona nimeeandika kichwa kuelezea mahudhui yatakayokuwepo ndani ya page
Hapo nilipoandika "Kichwa cha Mahudhui" Nimejaribu kukuelezea wewe kuhusu dhumuni la title tag ila hapo kwenye mabano ndio title yangu kuwa "Maelezo yangu binafsi"
yaani nitaeleza kuhusu maelezo yangu mwenyewe
Hivyo codes hizi zinaweza kuonekana kama hivi
HTML:
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title>Maelezo yangu binafsi</title>
</head>
</html>
Yaah jaribu kucopy hizi codes na kuzipaste kwenye code editor yako na urun
Utagundua kwamba hayo maneno hayajaonekana kwenye browser bali juu hapo kwenye tab
Hii pia usaidia kwenye SEO kusaidia search engine kufikia page zako
Oukey Sasa tujifunze tag Mpyyaaa
Tuanze na HEADING TAG-- hizi ni tag zinazo eleza kuwa kinachoandikwa ni heading na sikuzote tag hizi hua maandishi yake ni yamekoza (bold)
Tagi zahead hupungua kulingana na tag yenyewe ,Angalia hapo chini
<h1>Hua na Maandishi Makubwa
<h2>Hua na maandishi Madogo kushinda h1
<h3>Hua na Maandishi Madogo kushinda h2
<h4>Hua na Maandishi madogo kushinda h3
<h5>Hua na Maandishi madogo kushinda h4
<h6>Hua na maandishi madogo kushinda h5
Hakuna h7 au h8 na Kuendelea yote yataonekana sawa na h6
Pia apo iyo "h" inamaanisha heading na namba inayofuta ni kama cheo
Tag hizi huwekwa ndani ya <body> kumbuka kuwa nilikwambia kwenye body tag ndipo tunapoandaa content yaani kila tag iliyo kwenye body itaonekana tofauti na zilizo kwenye head hua ni za kueleza yaliomo
Tazama copy code hizi na uziweke kwenye editor yako uone kitakachotokea kupishana kwa heading tag
HTML:
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title>Kichwa cha Mahudhui(Maelezo yangu binafsi)</title>
</head>
<body>
<h1>Hua na Maandishi Makubwa</h1>
<h2>Hua na maandishi Madogo kushinda h1</h2>
<h3>Hua na Maandishi Madogo kushinda h2</h3>
<h4>Hua na Maandishi madogo kushinda h3<h4>
<h5>Hua na Maandishi madogo kushinda h4</h5>
<h6>Hua na maandishi madogo kushinda h5</h6>
<body>
</html>
Najua utaona mabadiliko kutoka katika browser yako
Tuangalie tag nyingine inayoitwa paragraph <p>: Tag hii hutumika kuandika maandishi/sentensi
KUMBUKA KUWEKA CLOSING TAG KWENYE KILA TAG
Mfano
HTML:
<p>Hii ni sentensi yangu hahahaha πππ</p>
Nadhani hapo Umenipata sasa Tuunde page kamili ya html kutumia tag tulizo jifunza soma codes hapo chini
HTML:
<!DOCTYPE html>
<html>
<head>
<title>Maelezo yangu binafsi</title>
</head>
<body>
<h1>Haya ni Maelezo yanihusuyo Mimi</h1>
<h2> Jina langu na tabia</h2>
<p>Jina Langu ninaitwa Binadamu Mtakatifu<br>Mimi simtu mbaya na mtu mwema na Mwenye maarifa.</p>
<h3>Kazi yangu ni ipi?</h3>
<p> Mimi ni Software developer na blogger</br>
</body>
</html>
Copy codes hizo na uzipaste kwenye editor kuona matokeo yake
Hapo najua mnajiuliza kuhusu jambo jipya yaani tag mpya ya </br>: TAG hii haina closing tag yaani inaweza kusimama yenyewe kama yenyewe pia inatumika kuruka na kuanza mstari mpya chini yake
Mfano unapoandika paragraph ukaamua kukata kwa kuruka chini Mfano
HTML:
<p>Hii ni sentensi yangu hahahaha,
hapa ngoja nikateπππ</p>
Itaonekana katika mstari mmoja sababu computer itapuuza mstari ulioruka
Ili kufanya hivyo tutatumia</br>
Mfano
HTML:
<p>Hii ni sentensi yangu hahahaha,</br> hapa ngoja nikateπππ</p>
Matokeo utayaona copycode kisha paste na urun kwenye editor yako
Ahsante kwa kufuatilia weka screenshot tushare wate matokeo
Itaendelea