Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Uzi Maalum wa mijadala yote ya michakato ya ziara za kampeni za mgombea nafasi ya Urais Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Salum Mwalimu na Mgombea mwenza Devotha Minja.
----------------
Agosti 27, 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemteua Mhe. Salum Mwalimu kugombea Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Devotha Mathew Minja kugombea Kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA).
Hafla hiyo ya uteuzi iliyofanyika kwenye Ofisi za Tume zilizopo Njedengwa, jijini Dodoma leo tarehe 27 Agosti, 2025 imeongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele
Soma pia GE2025 - Salum Mwalimu wa CHAUMMA atinga na nyomi kuchukua fomu ya Urais
Chanzo: Tume ya uchaguzi Tanzania
----------------
Agosti 27, 2025
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemteua Mhe. Salum Mwalimu kugombea Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Devotha Mathew Minja kugombea Kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA).
Hafla hiyo ya uteuzi iliyofanyika kwenye Ofisi za Tume zilizopo Njedengwa, jijini Dodoma leo tarehe 27 Agosti, 2025 imeongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele
Soma pia GE2025 - Salum Mwalimu wa CHAUMMA atinga na nyomi kuchukua fomu ya Urais
Chanzo: Tume ya uchaguzi Tanzania