South Africa: Julius Malema ataka Kiswahili kiwe lugha moja Afrika nzima

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Hakuna Matata: Malema calls for adoption of Swahili as Africa’s common language

Malema1.png

Julius Malema is the leader of South Africa’s Economic Freedom Fighters (EFF) party.

The leader of South Africa’s Economic Freedom Fighters (EFF) party, Julius Malema, has called for the adoption of a common language in Africa, hinting at Swahili being that language.

Malema made the remarks at a media briefing organized by the EFF, where he issued a speech touching on a series of issues, including the Donald Trump tweet on South Africa’s land reforms.

“We must develop a common language that can be used throughout the continent. Like Swahili, if it can be developed as the language of the continent,” he said.

Swahili is the most spoken language in Africa, commonly used in East and Central African states. It is an official language in Kenya and Tanzania.

Approximately 100 million people are able to converse in Swahili. That figure means Swahili is spoken by more people than Korean or Italian.

Swahili is also an official language of the African Union.

In the EFF media briefing, Malema also called for the unification of Africa, routing for a single currency, single president and single currency

========

Kiongozi wa chama cha watetezi wa Uhuru wa kiuchumi (EFF) cha Afrika Kusini, Julius Malema, ametoa wito wa kupitishwa kwa lugha moja itakayotumika barani Afrika, huku akipendekeza lugha ya Kiswahili kuwa lugha hiyo.

Malema aliyasema hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari ulioandaliwa na EFF, ambapo aliongelewa mambo mbalimbali ikiwemo ujumbe wa Rais wa Marekani kwenye mtandao wa Twitter kuhusu marekebisho ya sheria ya ardhi Afrika Kusini.

"Tunatakiwa kuzalisha lugha moja ambayo itatumika kwenye bara zima. Kwa mfano Kiswahili, kinaweza kukuzwa ili kitumike barani kote" alisema Malema.

Lugha ya kiswahili ni lugha inayotumika sana barani Afrika, ambapo kinatumika sana Afrika mashariki na kati. Ni lugha rasmi kwa nchi ya Tanzania na Kenya.
 
Jamaa ana siasa kali za kizalendo, yaani za kibaguzi, racist, black nationalist, tribalist

Ni kama wale wazungu wapinga uhamiaji wasiopenda nchi zao kuingiliwa na Weusi ama Waarabu

Huyu anazungumzia Kiswahili kwa kuwa tu ana chuki na wazungu na sio kwamba linaamini katika intergration ya ukweli baina ya binadamu hapa duniani

Muda huu tu BBC wameripoti Waafrika weusi wanauawa huko Afrika Kusini kisa tu sio wazawa, wazungu pia wanauawa kisa siasa za kichochezi na kibaguzi za huyo jamaa

Na ishu ya kuunganisha Afrika sijui ni ndoto ya saa ngapi

Nchi nyingi za Afrika zimeshindwa tu kujiunganisha kwa ndani zenyewe, unawaza bara zima kuungana, DRC, Sudan, Nigeria, Ethiopia, Cameroon n.k watu wanabaguana na kuuana kisa tu kabila tofauti ama dini, na viongozi wao wameshindwa kuwaunganisha, malaika gani ataunganisha bara zima?

Halafu single currency kwa biashara ipi tunayofanya pamoja?

Nchi za Kiafrica zinafanya biashara na China na Marekani & Ulaya kwa 90%, sisi hatuna vitu vya kuuziana labda sijui unga na maziwa

Sababu hatuzalishi bidhaa, tunaingiza kutoka ulaya na china kisha tunawauzia bidhaa ghafi, sasa hapo utahitaji single currency ya kazi gani? Au mihemko ya kuiga EU?

Wanasiasa wengine bana
 
Back
Top Bottom