South Africa: Julius Malema ataka Kiswahili kiwe lugha moja Afrika nzima

Kiswahili ndiyo "lingua-franca" ya ukanda wa nchi za Maziwa Makuu. Kinazungumzwa sana Afrika baada ya Kiarabu na Kifaransa. Ni Lugha rasmi, Kenya, Tanzania na Uganda. Katika nchi ya DRC, Kiswahili kinazungumzwa zaidi pia na kinazungumzwa zaidi kwenye majimbo matano kusini mwa nchi hiyo (DRC). Kimeshatumika katika muziki, na sanaa ya filamu. Mwanamuziki Michael Jackson katika wimbo wake wa "Liberian Girl" katumia Kiswahili, mtoto wa Bob Marley (Damian Marley) akishirikiana na NAS katika wimbo wao wa "As We Enter" kadhalika wametumia Kiswahili. Nitamatishe kwa kusema kuwa, bila shaka hii ndiyo lugha ya Kiafrika inayostahili kutumika rasmi. Asante Julius Malema.
 
Kiswahili kinaheshimiwasana dunia,waafrika wa west Afrika wanakikubali sana kiswahili,wazungu ndiio usiseme wanafikiri nchi zoteza Afrika wanazungumza kiswahili

Kenya ndio inang'ara kwa kiswahili kuliko Tanzania ughaibuni,Wakenya wanaitumia fursa ya kukitumia kiswahili kama lugha ya Afrika Mashariki ijapokuwa wao wenyewe Kiswahili hawakijui.,

Takriban walimu wengi wanaofundisha kiswahili nchi za Ulaya na Marekani ni wakenya....watanzania bado tuko katika kupigana wenyewe kwa wenyewe nani ana sera nzuri za siasa wakati wenzetu wanapiga hatua kivyengine,....
 
Kiswahili ndiyo "lingua-franca" ya ukanda wa nchi za Maziwa Makuu. Kinazungumzwa sana Afrika baada ya Kiarabu na Kifaransa. Ni Lugha rasmi, Kenya, Tanzania na Uganda. Katika nchi ya DRC, Kiswahili kinazungumzwa zaidi pia na kinazungumzwa zaidi kwenye majimbo matano kusini mwa nchi hiyo (DRC). Kimeshatumika katika muziki, na sanaa ya filamu. Mwanamuziki Michael Jackson katika wimbo wake wa "Liberian Girl" katumia Kiswahili, mtoto wa Bob Marley (Damian Marley) akishirikiana na NAS katika wimbo wao wa "As We Enter" kadhalika wametumia Kiswahili. Nitamatishe kwa kusema kuwa, bila shaka hii ndiyo lugha ya Kiafrika inayostahili kutumika rasmi. Asante Julius Malema.
Ni jambo pia la kujivunia kuona waafrika wenzetu wanapenda lugha yetu na kuitamani iwe yao. Hatuna budi kumtumia bwana Malema salamu za umoja na kumzawadia uraia wa kidiplomasia ili kazi hii tuifanye pamoja na kwa kasi inayotakiwa.
 
Wazo zuri japo utekelezaji wake mgumu lakn ni swala la muda tu.
Binafsi naona kiswahili kikisambaa sehemu kubwa ya africa baada ya miongo kadhaa ijayo that is nature.
 
Nakubaliana naye Mia kwa Mia Africa iwe Na lugha yake.Kiswahili kitakuwa mkombozi wa wengi mimi nikiwemo.Nikisafiri nje napata shida sana kisa tu kingereza hakipandi
baki tu apa nchini usisafiri kama mkuu....
 
Jamaa ana siasa kali za kizalendo, yaani za kibaguzi, racist, black nationalist, tribalist

Ni kama wale wazungu wapinga uhamiaji wasiopenda nchi zao kuingiliwa na Weusi ama Waarabu

Huyu anazungumzia Kiswahili kwa kuwa tu ana chuki na wazungu na sio kwamba linaamini katika intergration ya ukweli baina ya binadamu hapa duniani

Muda huu tu BBC wameripoti Waafrika weusi wanauawa huko Afrika Kusini kisa tu sio wazawa, wazungu pia wanauawa kisa siasa za kichochezi na kibaguzi za huyo jamaa

Na ishu ya kuunganisha Afrika sijui ni ndoto ya saa ngapi

Nchi nyingi za Afrika zimeshindwa tu kujiunganisha kwa ndani zenyewe, unawaza bara zima kuungana, DRC, Sudan, Nigeria, Ethiopia, Cameroon n.k watu wanabaguana na kuuana kisa tu kabila tofauti ama dini, na viongozi wao wameshindwa kuwaunganisha, malaika gani ataunganisha bara zima?

Halafu single currency kwa biashara ipi tunayofanya pamoja?

Nchi za Kiafrica zinafanya biashara na China na Marekani & Ulaya kwa 90%, sisi hatuna vitu vya kuuziana labda sijui unga na maziwa

Sababu hatuzalishi bidhaa, tunaingiza kutoka ulaya na china kisha tunawauzia bidhaa ghafi, sasa hapo utahitaji single currency ya kazi gani? Au mihemko ya kuiga EU?

Wanasiasa wengine bana
Yuko sahihi. Ndoto ya Mwalimu nyerere PAN Afrikanism ilikuwepo tangu zamani. Yuko sahihi kabisa. Kuonyesha yuko fair kasema kiswahili na siyo lugha ya kwao.
 
Hizo taasisi nyeti hapo juu au yoyote Tanzania inayoheshimika mwalikeni Julius Malema aje Tanzania atoe mihadhara. Jamaa ana akili ana nyota na juu ya yote amekipa promo kiswahili huyu ni mtu muhimu kwetu na Afrika kwa ujumla.
 
Kwa ninavyojua Malema ni kawaida kuashiria anataka mapinduzi ya nguvu pia ni mbaguzi sidhani kama Kigoda kitawezana na kariba hiyo
 
Back
Top Bottom