South Africa Airlines mbioni kufilisika.

South Africa Airlines mbioni kufilisika.

D 007

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2012
Posts
206
Reaction score
147
Kwa mujibu wa ripoti zilizochunguzwa na kuwasilishwa na Serikali ya Zuma Bungeni Shirika la Ndege, South African Airways liko mbioni kufilisika.

Shirika hilo limekuwa likijiendesha kwa hasara kwa miaka 7 mfululizo na karibia litashindwa kuwalipa mishahara wafanyakazi wake.

Shirika limeomba msaada wa £560m ili kujikwamua kutoka katika hali hiyo mbaya ya kifedha inayowakabili Zuma, Kimsingi serikali yetu tujifunge mkanda kurejesha shirika letu la ATC, kwa nidhamu ya hali ya juu kuipigania National Carrier.

Biashara ngumu sana hii especially kama hauna systems in place, technological advancement is key in making sure an airline's bottom line grows. GOOD MORNING ..007

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tanzania tupo kinyume sana, Atcl ilijiendesha kwa hasara kwa zaidi ya muda huo na haikuwahi kufilisika, hapo ilikua na ndege moja tu.
Wenzetu miaka 7 ya hasara na kufilisika juu, hapo Bwana Zuma katoka kuombwa pesa ya kujenga reli ya Tanzania.
 
Hakuna biashara pasua kichwa kama ya NDEGE sema na sisi tumeingia kichwa kichwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Katika yote, heshima kwa aviation industry hakuna kitu naheshimu kama route connection. Mfano mdogo sana, Lufthansa ikiondoka Dar kuelekea Frankfurt kupitia Jeddah humo ndani ya ndege kuna abiria wa almost kila route na wenye majukumu tofauti tofauti. Inatakiwa ifike Jeddah on-time ili wanaoishia Jeddah waendelee na majukumu yao; wanaounganisha ndege kuelekea maeneo mengine ya dunia waweze kufanya hivyo.

Wakati huo huo ndege hiyo hiyo iweze kuwawahi abiria wanaoisubiri pale Jeddah kutokea routes nyingine kuelekea Frankfurt na iwahi Frankfurt ili wanao-connect routes nyingine waweze kuwahi ndege zinazowasubiri pale. Dah, hii biashara sio mchezo uki-messup unafilisika sio mchezo na kumbuka kumchelewesha abiria maana yake tayari umempoteza mteja wa kesho.
 
Hakuna biashara pasua kichwa kama ya NDEGE sema na sisi tumeingia kichwa kichwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Biashara yoyote ya chombo cha moto ni ngumu sana basi tuu. Watu wengi wanafanya kibishi bishi tuu
Angalia matajiri wa magari ya mikoa wanavyopata shida wakati mwingine kwa sababu katika ishu za kusafiri wakati mwingine uwezi amini biashara asilimia 100 [emoji817]
 
Mashirika mengi ya ndege yanalia basi tu kilio chao huwa hatukisikio
 
Katika yote, heshima kwa aviation industry hakuna kitu naheshimu kama route connection. Mfano mdogo sana, Lufthansa ikiondoka Dar kuelekea Frankfurt kupitia Jeddah humo ndani ya ndege kuna abiria wa almost kila route na wenye majukumu tofauti tofauti. Inatakiwa ifike Jeddah on-time ili wanaoishia Jeddah waendelee na majukumu yao; wanaounganisha ndege kuelekea maeneo mengine ya dunia waweze kufanya hivyo.

Wakati huo huo ndege hiyo hiyo iweze kuwawahi abiria wanaoisubiri pale Jeddah kutokea routes nyingine kuelekea Frankfurt na iwahi Frankfurt ili wanao-connect routes nyingine waweze kuwahi ndege zinazowasubiri pale. Dah, hii biashara sio mchezo uki-messup unafilisika sio mchezo na kumbuka kumchelewesha abiria maana yake tayari umempoteza mteja wa kesho.

Wanaoweza hii biashara ni waarabu tu emirates, etihad na Qatar. Mijamaa inafuata ratiba mnooo li A380 linaamshwa ontime hata kama lina abiria sita. Viairline vya uchochoroni kama KQ na SAA na vipanga boy vyao kama hawajapata level seat wanahairisha safari. Unadhani nani atarudi kwa upumbavu huu? Bora ethiopian airlines anajijua kwakuwa huduma mbovu basi na nauli pia inakuwa ipo chini
 
Wanaoweza hii biashara ni waarabu tu emirates, etihad na Qatar. Mijamaa inafuata ratiba mnooo li A380 linaamshwa ontime hata kama lina abiria sita. Viairline vya uchochoroni kama KQ na SAA na vipanga boy vyao kama hawajapata level seat wanahairisha safari. Unadhani nani atarudi kwa upumbavu huu? Bora ethiopian airlines anajijua kwakuwa huduma mbovu basi na nauli pia inakuwa ipo chini
Wale wana privilege ya wese Mkuu; linasiadia ku-subsidize maeneo mengine. Vinginevyo, sioni ni kwa vipi utaburuza A380 DAR - DOHA (karibu km 4000) ukiwa na abiria 6 usifilisike.
 
Wale wana privilege ya wese Mkuu; linasiadia ku-subsidize maeneo mengine. Vinginevyo, sioni ni kwa vipi utaburuza A380 DAR - DOHA (karibu km 4000) ukiwa na abiria 6 usifilisike.

Ni kweli mkuu ila inasaidia kuongeza wataja. Kipindi flani nilikuwa natakiwa nitoke central africa republic na KQ hadi nairobi then nichukuwe SAA hadi Jburg (kwakuwa KQ ya kwenda SA ilionekana imejaa) basi KQ kutoka CAR baada ya kuona column haijatimia wakaghairisha safari hadi kesho yake. Iliniathiri kwasababu ilibidi nilipie rebooking ya SAA kwenda jburg na mambo mengine kibao yalivurugika. Nikajiapiza next time kwa ishu kama hiyo sichukui tena ndege za kishenzi
 
Back
Top Bottom