Sote tumeshiriki kuua vyama vya upinzani

Abby Newton

JF-Expert Member
Nov 12, 2017
1,227
2,197
Upinzani uko hoi bin Taabani.Ni km mgonjwa anaesubiri siku tu ya kwenda kumzika lakini ndugu na jamaa tayari wameshakata tamaa.

Tumefika hapa kwasababu ya kila mmoja wetu anahusika, japo wachache wanaulaumu upande mmoja wa shiringi. Kivipi?

1. Magogoni, Bunge na Mahakama.
Mihimili hii mitatu imetengeneza utatu mtukufu wa kuwabana wapinzani kila kona. Wapinzani hawana pa kupumulia, bila kuvisahau vyombo vya dola.

2. Vyombo vya habari. Hawa wamekuwa very bias katika kueleza habari na "kubalance" mzani.Ni mara chache Wapinzani kupewa "air time"hasa kwenye mainstream media. Praise team imetawala kuanzia asubuhi hadi jioni.

3. Wananchi. Sijui ni mihemko, ulimbukeni, ujinga au uoga baadhi yetu tumeaminishwa na kuamini eti wapinzani ni wapinga maendeleo, vibaraka wa mabeberu na wasioitakia mema nchi hii. Tumesahau kuwa ni hawahawa wapinzani tunaowadharau leo ndio waliosimama kidete kuvumbua "corruption skendo"kubwa kubwa kama Richmond,Dowans, Meremeta, mikataba mibovu ya madini, rushwa kubwa n .k

Ile dhana kwamba wapinzani ndio watetezi wa wanyonge na maslahi ya nchi tumeitupilia mbali. Unafiki umetutawala.

4. Watumishi wa serikali
Hapa namaanisha hasa watumishi wa Halimashauri kama Waalimu, watendaji na maafisa Ugani. Hawa wamekuwa km tawi la chama ndani ya serikali. Waliunda vikundi( Jumuia) kuhakikisha ushindi wa mia kwa mia unapatikana. Sijajua walifanya kwa mapenzi au woga wa kulinda mkate wao. Wamesahau ni wapinzani ndio wamekuwa wakiwatetea wapandishiwe mishahara pamoja na vyeo.

5. Wasomi elimu ya juu.
Imefika hatua Profesa si wa kuheshimika tena. Mtu anadhalilisha elimu yake na kwenda kinyuma na taaluma yake ili mradi tu aonekane akiunga juhudi. Wameogopa kukosoa na kuonya pale mambo yanapooenda ovyo na kubaki wakisifia hata visivyostaili kusifia.

6. Wasanii wa mziki,filamu na vichekesho.
Hawa ndo wameonyesha usanii wa kiwango cha juu. Umeona wapi nchi nzima wasanii wote kuwa chama tawala we umeona wapi?...

7. Viongozi wa dini.
Nina wasi wasi km Bwana Yesu au mtume Muhammed S.A wakirudi leo wanaweza kumpata kiongozi wa dini mwenye hadhi na viwango vya kuingia mbinguni.( Kulingana na imani zetu).

Viongozi wengi wa dini ni wanafiki, waoga na wenye upendeleo.

Wamekubali kutumika na kuegemea upande mmoja. Sifa ya kiongozi bora wa dini ni kusimama katika haki maana Mungu ni wa HAKI.

7. Wapinzani wenyewe.Tamaa ya vyeo, pesa na usaliti,ni kirusi kingine kilichowaangamiza wapinzani wenyewe. Wengi si wapinzani halisia bali ni wafuata upepo wa mafanikio. Ndio maana wengi wapo tayari kuuza utu wao na kutumika kuhujumu vyama vyao.

Hivyo, tunapoendelea kuwashangaa akina Mdee nazani tuendelee pia kujishangaa wenyewe km taifa je tunaelekea wapi? Je ni kweli wapinzani hawana maana tena au sisi ndo hatujielewi?

Nawasilisha
 
Tufanye nini sasa??? Tusiishie kunyosheana vidole.Tutafute ufumbuzi.Unadhani nini kifanyike?
 
Chama cha siasa ni kama binadamu kinazaliwa,kinakua kinapata umaarufu mwishowe kinakufa na maisha yanasonga mbele kama kawaida.
 
Tuungane na kugoma kutoa sadaka kwenye nyumba za ibada walau mwaka mmoja. Ili hao viongozi wa dini waisome namba
 
Kama kuna mtu aliyekuwa na nia ya dhati kabisa ya kuuua upinzani, ni aliyechaguliwa kuwa rais na baadae mwenyekiti wa ccm John Magufuli.
Na kwa kutumia mamlaka vibaya, hao wengine wote uliowataja, walitishwa, walifukuzwa kazi, walipewa rushwa ya kila aina ikiwamo ajira, pesa, vyeo zaidi, na wananchi kunyimwa haki ya kuhudumiwa na serikali yao licha ya kulipa kodi kila siku, na aliyeyafanya haya ni John Magufuli.
Nina uhakika, John Magufuli asingeshika madaraka aliyonayo sasa hivi, vyama vya siasa vingekuwepo tena na uimara wake kama lengo la uwepo wake lililokusudiwa.
Sasa hamna haja ya kuzunguka mbuyu kutaja taasisi na watu wasiohusika kuviua na kuvuruga taratibu tuliojiwekea na kuzikubali.
 
Tufanye nini sasa??? Tusiishie kunyosheana vidole.Tutafute ufumbuzi.Unadhani nini kifanyike?
Hata ww toa mawazo yako mkuu maana ni sehemu ya Tatizo.Kazi ya kuonyesha tatizo nimeimaliza mkuu
 
Nafikir pia aina ya mgombea aliesimamishwa hakuwa anajua utamaduni na mahitaji halisi ya wananchi wa kawaida.Watanzania sio watu wafujo na wanahofia machafuko sana,kitendo cha TL kuhubir maandamano n kitawaka mara kitanuka was bad strategy

Pia agenda ya uhuru na maendeleo ya watu haikuwa na mashiko kwa walio wengi maana shighuli zao zinakwenda sasa ukiwaambia wasimchague aliewajengea barabara wakuchague wewe ulete uhuru wasnt making any sense to majority

Aina ya wanachama wake wengi wao si wapiga kura na wengi hawakwenda kupiga kura hoji vijana wa kat ya19-27 wafuasi wa chadema kati ya 10 6 hawakupiga kura

Mafungamano ya TL na mataifa ya nje was soo bad maana saiv nchi ipo kwenye mchakato wa kunufaika na mali zake ambazo zilikuwa zikinufaisha wazungu sasa kitendo cha kuwakumbatia was bad strategy

Agenda ya ushoga pia,kitendo cha TL kushindwa kuonesha nia ya dhat ya kuupinga hadharan was bad

Kupima performance ya chadema kupitia uchaguz wa2015 was bad maana iliwafanya warelax kwa kuona chama kime kuwa wasijue kuwa 2015 mpambano ulikuwa kati ya cna ccm b.matokeo yanaonesha kuwa wananchi wanaimani na ccm kuliko upinzani ndio maana Lowassa (ccm)alipata kura nyingi kuliko Lissu licha ya umaaruf wake wote

NB:chadema inatakiwa kutoka kwenye siasa za kiuharakati na kuwa chama chenye lengo la kushika dola na si chama cha wahuni kama ilivyo sasa.

Kufuatia kitendo cha TL kukimbia nchi watz wengi wameamini agenda ya yeye kutumwa na mabeberu hivyo kwa namna yoyote ile hafai kugombea tena2025. Wananchi wanaweza kuwa wameichoka ccm ila hawaoni mbadala ndo maana wanaendelea kuichagua
 
Sawa Kabisa!!! Na binadamu wengi tumekuwa watu wa kujaribu jaribu ladha tofauti ....ngoja tujaribu mitano hii bila wapinzani kuna kitu tutajifunza na kukifanyia kazi uchaguzi ujao...ama kuwafikiria tena wapinzani au kuwasahau kabisa!!!
 
Mbona ACT wapo imara nasikia Mh. Bernard K. Membe anaendelea kupanga safu ya Mawaziri maana 2025 amesema hapatoshi, CCM ijiandae kufungasha virago na kukabidhi ikulu.
 
3. Wananchi. Sijui ni mihemko, ulimbukeni, ujinga au uoga baadhi yetu tumeaminishwa na kuamini eti wapinzani ni wapinga maendeleo, vibaraka wa mabeberu na wasioitakia mema nchi hii. Tumesahau kuwa ni hawahawa wapinzani tunaowadharau leo ndio waliosimama kidete kuvumbua "corruption skendo"kubwa kubwa kama Richmond,Dowans, Meremeta, mikataba mibovu ya madini, rushwa kubwa n .k

Ile dhana kwamba wapinzani ndio watetezi wa wanyonge na maslahi ya nchi tumeitupilia mbali. Unafiki umetutawala.

4. Watumishi wa serikali
Hapa namaanisha hasa watumishi wa Halimashauri kama Waalimu, watendaji na maafisa Ugani. Hawa wamekuwa km tawi la chama ndani ya serikali. Waliunda vikundi( Jumuia) kuhakikisha ushindi wa mia kwa mia unapatikana. Sijajua walifanya kwa mapenzi au woga wa kulinda mkate wao. Wamesahau ni wapinzani ndio wamekuwa wakiwatetea wapandishiwe mishahara pamoja na vyeo.

5. Wasomi elimu ya juu.
Imefika hatua Profesa si wa kuheshimika tena. Mtu anadhalilisha elimu yake na kwenda kinyuma na taaluma yake ili mradi tu aonekane akiunga juhudi. Wameogopa kukosoa na kuonya pale mambo yanapooenda ovyo na kubaki wakisifia hata visivyostaili kusifia.

6. Wasanii wa mziki,filamu na vichekesho.
Hawa ndo wameonyesha usanii wa kiwango cha juu. Umeona wapi nchi nzima wasanii wote kuwa chama tawala we umeona wapi?...

7. Viongozi wa dini.
Nina wasi wasi km Bwana Yesu au mtume Muhammed S.A wakirudi leo wanaweza kumpata kiongozi wa dini mwenye hadhi na viwango vya kuingia mbinguni.( Kulingana na imani zetu).

Viongozi wengi wa dini ni wanafiki, waoga na wenye upendeleo.

Wamekubali kutumika na kuegemea upande mmoja. Sifa ya kiongozi bora wa dini ni kusimama katika haki maana Mungu ni wa HAKI.

7. Wapinzani wenyewe.Tamaa ya vyeo, pesa na usaliti,ni kirusi kingine kilichowaangamiza wapinzani wenyewe. Wengi si wapinzani halisia bali ni wafuata upepo wa mafanikio. Ndio maana wengi wapo tayari kuuza utu wao na kutumika kuhujumu vyama vyao.

Hivyo, tunapoendelea kuwashangaa akina Mdee nazani tuendelee pia kujishangaa wenyewe km taifa je tunaelekea wapi? Je ni kweli wapinzani hawana maana tena au sisi ndo hatujielewi?

Nawasilisha
Walio umaliza upinzani hawa hapa 👇👇👇
images (22).jpeg

Cha ajabu bado wapo madarakani utazani,chama mali yao.

NB
Kama kiongozi ukikosa Msimamo kwa tamaa ya hela ndogo,basi hata unaowaongoza nao watanunulika,alianza mwenyikiti kununuliwa wakafuatia viongozi walio chini yake.

So matokeo ya leo unayo yaona msingi wake ulianza kujengwa hapo kwenye hiyo picha.
 
Upinzani uko hoi bin Taabani.Ni km mgonjwa anaesubiri siku tu ya kwenda kumzika lakini ndugu na jamaa tayari wameshakata tamaa.

Tumefika hapa kwasababu ya kila mmoja wetu anahusika, japo wachache wanaulaumu upande mmoja wa shiringi. Kivipi?

1. Magogoni, Bunge na Mahakama.
Mihimili hii mitatu imetengeneza utatu mtukufu wa kuwabana wapinzani kila kona. Wapinzani hawana pa kupumulia, bila kuvisahau vyombo vya dola.

2. Vyombo vya habari. Hawa wamekuwa very bias katika kueleza habari na "kubalance" mzani.Ni mara chache Wapinzani kupewa "air time"hasa kwenye mainstream media. Praise team imetawala kuanzia asubuhi hadi jioni.

3. Wananchi. Sijui ni mihemko, ulimbukeni, ujinga au uoga baadhi yetu tumeaminishwa na kuamini eti wapinzani ni wapinga maendeleo, vibaraka wa mabeberu na wasioitakia mema nchi hii. Tumesahau kuwa ni hawahawa wapinzani tunaowadharau leo ndio waliosimama kidete kuvumbua "corruption skendo"kubwa kubwa kama Richmond,Dowans, Meremeta, mikataba mibovu ya madini, rushwa kubwa n .k

Ile dhana kwamba wapinzani ndio watetezi wa wanyonge na maslahi ya nchi tumeitupilia mbali. Unafiki umetutawala.

4. Watumishi wa serikali
Hapa namaanisha hasa watumishi wa Halimashauri kama Waalimu, watendaji na maafisa Ugani. Hawa wamekuwa km tawi la chama ndani ya serikali. Waliunda vikundi( Jumuia) kuhakikisha ushindi wa mia kwa mia unapatikana. Sijajua walifanya kwa mapenzi au woga wa kulinda mkate wao. Wamesahau ni wapinzani ndio wamekuwa wakiwatetea wapandishiwe mishahara pamoja na vyeo.

5. Wasomi elimu ya juu.
Imefika hatua Profesa si wa kuheshimika tena. Mtu anadhalilisha elimu yake na kwenda kinyuma na taaluma yake ili mradi tu aonekane akiunga juhudi. Wameogopa kukosoa na kuonya pale mambo yanapooenda ovyo na kubaki wakisifia hata visivyostaili kusifia.

6. Wasanii wa mziki,filamu na vichekesho.
Hawa ndo wameonyesha usanii wa kiwango cha juu. Umeona wapi nchi nzima wasanii wote kuwa chama tawala we umeona wapi?...

7. Viongozi wa dini.
Nina wasi wasi km Bwana Yesu au mtume Muhammed S.A wakirudi leo wanaweza kumpata kiongozi wa dini mwenye hadhi na viwango vya kuingia mbinguni.( Kulingana na imani zetu).

Viongozi wengi wa dini ni wanafiki, waoga na wenye upendeleo.

Wamekubali kutumika na kuegemea upande mmoja. Sifa ya kiongozi bora wa dini ni kusimama katika haki maana Mungu ni wa HAKI.

7. Wapinzani wenyewe.Tamaa ya vyeo, pesa na usaliti,ni kirusi kingine kilichowaangamiza wapinzani wenyewe. Wengi si wapinzani halisia bali ni wafuata upepo wa mafanikio. Ndio maana wengi wapo tayari kuuza utu wao na kutumika kuhujumu vyama vyao.

Hivyo, tunapoendelea kuwashangaa akina Mdee nazani tuendelee pia kujishangaa wenyewe km taifa je tunaelekea wapi? Je ni kweli wapinzani hawana maana tena au sisi ndo hatujielewi?

Nawasilisha
Upinzani haujauawa mmewapora ushindi tu.
 
Upinzani uko hoi bin Taabani.Ni km mgonjwa anaesubiri siku tu ya kwenda kumzika lakini ndugu na jamaa tayari wameshakata tamaa.

Tumefika hapa kwasababu ya kila mmoja wetu anahusika, japo wachache wanaulaumu upande mmoja wa shiringi. Kivipi?

1. Magogoni, Bunge na Mahakama.
Mihimili hii mitatu imetengeneza utatu mtukufu wa kuwabana wapinzani kila kona. Wapinzani hawana pa kupumulia, bila kuvisahau vyombo vya dola.

2. Vyombo vya habari. Hawa wamekuwa very bias katika kueleza habari na "kubalance" mzani.Ni mara chache Wapinzani kupewa "air time"hasa kwenye mainstream media. Praise team imetawala kuanzia asubuhi hadi jioni.

3. Wananchi. Sijui ni mihemko, ulimbukeni, ujinga au uoga baadhi yetu tumeaminishwa na kuamini eti wapinzani ni wapinga maendeleo, vibaraka wa mabeberu na wasioitakia mema nchi hii. Tumesahau kuwa ni hawahawa wapinzani tunaowadharau leo ndio waliosimama kidete kuvumbua "corruption skendo"kubwa kubwa kama Richmond,Dowans, Meremeta, mikataba mibovu ya madini, rushwa kubwa n .k

Ile dhana kwamba wapinzani ndio watetezi wa wanyonge na maslahi ya nchi tumeitupilia mbali. Unafiki umetutawala.

4. Watumishi wa serikali
Hapa namaanisha hasa watumishi wa Halimashauri kama Waalimu, watendaji na maafisa Ugani. Hawa wamekuwa km tawi la chama ndani ya serikali. Waliunda vikundi( Jumuia) kuhakikisha ushindi wa mia kwa mia unapatikana. Sijajua walifanya kwa mapenzi au woga wa kulinda mkate wao. Wamesahau ni wapinzani ndio wamekuwa wakiwatetea wapandishiwe mishahara pamoja na vyeo.

5. Wasomi elimu ya juu.
Imefika hatua Profesa si wa kuheshimika tena. Mtu anadhalilisha elimu yake na kwenda kinyuma na taaluma yake ili mradi tu aonekane akiunga juhudi. Wameogopa kukosoa na kuonya pale mambo yanapooenda ovyo na kubaki wakisifia hata visivyostaili kusifia.

6. Wasanii wa mziki,filamu na vichekesho.
Hawa ndo wameonyesha usanii wa kiwango cha juu. Umeona wapi nchi nzima wasanii wote kuwa chama tawala we umeona wapi?...

7. Viongozi wa dini.
Nina wasi wasi km Bwana Yesu au mtume Muhammed S.A wakirudi leo wanaweza kumpata kiongozi wa dini mwenye hadhi na viwango vya kuingia mbinguni.( Kulingana na imani zetu).

Viongozi wengi wa dini ni wanafiki, waoga na wenye upendeleo.

Wamekubali kutumika na kuegemea upande mmoja. Sifa ya kiongozi bora wa dini ni kusimama katika haki maana Mungu ni wa HAKI.

7. Wapinzani wenyewe.Tamaa ya vyeo, pesa na usaliti,ni kirusi kingine kilichowaangamiza wapinzani wenyewe. Wengi si wapinzani halisia bali ni wafuata upepo wa mafanikio. Ndio maana wengi wapo tayari kuuza utu wao na kutumika kuhujumu vyama vyao.

Hivyo, tunapoendelea kuwashangaa akina Mdee nazani tuendelee pia kujishangaa wenyewe km taifa je tunaelekea wapi? Je ni kweli wapinzani hawana maana tena au sisi ndo hatujielewi?

Nawasilisha
Upinzani ungekuwa hoi mngetumia AK47 na mabomu kupata kura ?
 
Wapinzani wenyewe wako wako wapi?hawa ambao unalala huku hujui kesho nani utasikia kununuliwa?
 
Back
Top Bottom