Sophia Simba: Wanawake Jeshi Kubwa hang'oki CCM

Sophia Simba: Wanawake Jeshi Kubwa hang'oki CCM

njeeseka

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2012
Posts
1,374
Reaction score
985
Akiongea na akinamama ccm. Anasema Wanaosema kuna wengine watahama chama cha ccm wanajidanganya, mikakati ya wapinzani wanaijua kwani hukohuko kuna vijana wao wanawapa taarifa. Amevaa vazi limeandikwa BAKI CCM

Wajameni GT hamjambo!!!!

Wanawake ni jeshi kubwa. Ni kweli na Hilo halina ubishi. Ila jeshi la kutembea ki analogia wakati tupo kwenye digital hilo sio jeshi. Nayasema haya kwa sababu zifuatazo:

Baada ya kumaliza pilika pilika za uchaguzi wa Viti maaalum ndani ya CCM, wale tuliokuwa tukifatilia kwa karibu na kutazama jumuiya yetu kwa macho matatu tumegundua UWT is a "SLEEPING GIANT".

Hivyo basi kwa kuwa Octoba ni kesho; tunaelekeza nguvu zetu kuamsha hili li giant ili tupate kura nyingi 90% za wanawake wa TZ kwenye Urais, Wabunge na Madiwani. Kura nyingi zitatuongezea viti zaidi.

Umoja wetu ndio USHINDI wetu. Hili linahusu wanachama wote waliogombea wukakosa, waliopata, waliojeruhiwa kwa namna moja au nyingine, wanachama hai, wapya na wale wanaohitaji kuamshwa, n.k. Kwa kifupi malezi yetu ni Chama mbele mtu baadae.

Baada ya Mhe Magufuli kuapishwa tutaanza mchaka mchaka wa kuliamsha li sleeping giant ki digital zaidi. Nina maana gani ninaposoma haya:-
1. Tunahitaji kui restructure, reengineer, reengage, reinforce, reorganise etc UWT
2. UWT inatakiwa kufahamu iko kwenye mfumo wa vyama vingi na sio chama kimoja
3. Wasomi wengi zaidi wanatakiwa ndani ya chama; sina maana nime ignore wasio wasomi la hasha. We need VISIONARY LEADERS
4. Mambo ya kujuana, ili mtu apigiwe kura ni aibu kubwa. oh! Huyu wifi yangu, oh! Mtoto wa dada yangu, oh! kaolewa na mwanangu nk kuwa sera ya mgombea yanatia aibu na kumdhalilisha mwanamke.
5. Yapo mengi siwezi kuyaweka hapa ila
6. Baada ya Octoba 2015 tunataka MABADILIKO ili 2017 tujipange kupata viongozi na sio bora viongozi.

WANAWAKE TUJIPANGE POPOTE ULIPO NA KAMA HUNA KADI YA UWT SASA NI WAKATI SAHIHI NENDA KWENYE KATA YAKO HAKIKISHA UMEPATA KADI NA KUILIPIA. Usiache kumshika mkono jirani yako, rafiki nk kuhakikisha nae anapata kadi. Mengine yatafata baadae.

Naomba kutoa hoja, nakaribisha contrastive criticism, kuunga mkono hoja, kuongeza nyama nk.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.

Queen Esther
 
Akiongea na akinamama ccm. Anasema Wanaosema kuna wengine watahama chama cha ccm wanajidanganya, mikakati ya wapinzani wanaijua kwani hukohuko kuna vijana wao wanawapa taarifa. Amevaa vazi limeandikwa BAKI CCM
Ni bora astaafu tu siasa. Hana jipya.
 
huyu mama sioni kama kuna kitu anachokijua. hata alityempa uwaziri sijajua alizingatia nini.
labda wana jamvi mnisaidie nisichokijua kwa huyu mama.
 
Asubiri zamu yake wenzake wote wameshakatwa kwa amri ya Mwenyekigoda sasa asubiri zamu yake tu.......Nadhani tunasubiri VAZI litabadilishwa sasa hivi kuwa HAMIA UKAWA.............
 
Tukutane 25/10/2015 kwenye sanduku la kura ndipo CCM watakapotambua kuwa imebaki na wafuasi wanaovaa nguo za kijani,vinywani mwao wako na CCM lakini mioyo yao iko UKAWA kwa Lowassa.
 
Huyu shushu wetu mwacheni tafadhali

Wakati Wewe Ukijinadi Kuwa Huyu Ni Shushu Wenu Lakini Hapo Hapo Na Wewe Usijisahau Kuwa Huko Huko UKAWA Kwenu Karibia 75% Ya Viongozi Wenu Waandamizi Ni Wana UWT Wa CCM Tena WALIOTUKUKA? au Nikutajie Majina Yao Ujifiche Uvunguni Sasa Hivi?
 
ccm kama watamuamini huyu mama wamekwisha...

Lowassa ndo alikwisha kwa kumuamini huyu na Adam Kimbisa.Boys two men mmoja alikuwa anasugua mwingine anagawa hela, ilipofika wakati wa kuchagua mmoja kachagua msuguaji
 
Akiongea na akinamama ccm. Anasema Wanaosema kuna wengine watahama chama cha ccm wanajidanganya, mikakati ya wapinzani wanaijua kwani hukohuko kuna vijana wao wanawapa taarifa. Amevaa vazi limeandikwa BAKI CCM
njeeseka
attachment.php
 
Karata ya ccm kwa wanawake ni mgombea mwenza...nadhani wenye kupiga kura za huruma kwa mwanamke mwenzao ndio eneo lao..
 
Asubiri zamu yake wenzake wote wameshakatwa kwa amri ya Mwenyekigoda sasa asubiri zamu yake tu.......Nadhani tunasubiri VAZI litabadilishwa sasa hivi kuwa HAMIA UKAWA.............

Kwa kuwa kwake Mwnykt wa UWT tayari ana kiti maalum ndo mana hujamsikia akigombea. MWNYKT TAIFA WA UWT HUPEWA UBUNGE WA VITI MAALUM KWA KATIBA YAO
 
Wakati Wewe Ukijinadi Kuwa Huyu Ni Shushu Wenu Lakini Hapo Hapo Na Wewe Usijisahau Kuwa Huko Huko UKAWA Kwenu Karibia 75% Ya Viongozi Wenu Waandamizi Ni Wana UWT Wa CCM Tena WALIOTUKUKA? au Nikutajie Majina Yao Ujifiche Uvunguni Sasa Hivi?

Umbeya tu wataje embu
 
Back
Top Bottom