Sophia Simba, Madabida wavuliwa uanachama CCM. Emmanuel Nchimbi apewa onyo kali

....kwa tangazo hili ina maana kuwa SS pia amefukuzwa ubunge; hakuna kiinua mgongo hapo!
 
Kwani mama simba anashutuma gani za kuhitaji kusafishwa mkuu?
Hii siyo sawa. Huyu Mama kafanya vitu vingi kwa chama ila dakika ya mwisho katubuniwa. She is now close to retirement if not already retired, atapata wapi marafiki wapya Chadema, hasa ukuzingatia wala siyo mtu wa huko jamaa walivyo wajivuni? Ni kama Kigunge, hana raha. Au Sheikh Takadir "Mtakadini" 1958. Alikufa hana raha. Why did she do it?
Anabaki mkiwa ukizingatia aliokuwa nao katika harakati za chama kama Hayati Kitwana Kondo na wengine hawapo tena duniani.
 
Kiongozi wa uasi, aliyezungumza usiku ule (Emmanuel Nchimbi) kapewa onyo akiwa tayari Balozi, tena balozi ambae aliteuliwa baadae huku wenzake wa awali wakishinda pale foreign kwenye mabenchi wakisoma magazeti kusubiri vituo; Wafuasi wa nchimbi wanasamehewa/wanafukuzwa uanachama, tena baada ya mmoja wao (Sofia Simba) kuweka wazi kabisa kwamba yeye na siasa za CCM sasa imetosha.

Ama kweli CCM vituko kuisha mwiko.
 
Back
Top Bottom