Hayo ndio maneno ya wanaume siku zote kudhalilisha wanawake. Ndio kila sehemu kuna kubebwa lakini kwa jinsi mlimani ya wakati huo (sina uhakika na sasa) isingelikuwa mtu ambaye hata hajui kabisa kuongea kiingereza aweze kubebwa na walimu wote kuanzia DS mpaka yale masomo yenyewe ya LLB.
Hiyo course ilikuwa inaongoza kuchukua watu wenye uwezo wakati huo (around 60) nchi nzima. Kuna watu walikuwa wana disco mpaka hata wakiwa mwaka wa tatu. Sasa nashangaa huyu mama ambaye hajui kabisa kiingereza angewezaji kupita hiyo miaka mitatu?
Sophia Simba alianzia kusoma certificate tena hapo hapo UDSM hivyo yeye ni mpambanaji kutokea chini. Hakuwa na uwezo mkubwa sana kama wanafunzi wengine lakini pia ni makosa makubwa sana kufikiri mtu kama Sophia Simba ni mjinga.
Najua sio fluent wa kuongea kiingereza kama anavyo ongea Kiswahili lakini kusema hajui kiingereza kabisa nafikiri is either outright false or exaggerated beyond belief.
Mkuu kujua kiingereza kabisa au kutojua kabisa, hakuna maana yoyote. Kama anajua kiingereza kabisa, yeye si mtu wa kwanza, na kama hajui kiingereza kabisa yeye si mtu wa kwanza, wapo wengi tu. Issue ni kwamba je anaweza kuwa mwakilishi wa Tanzania? Does she have what it takes to be a qualified representative? Kusoma chuo Kikuu, Kuongea kiingereza peke yake si vigezo tosha. Vina nafasi yake, lakini pekee havitoshelezi.
Tunatakiwa kujudge kutokana na utendaji wake kwenye ofisi alizofanya kazi, maneno aliyosema, in public and in private, tabia zake, mienendo yake n.k. Tuangalie uwezo wake wa kufikiri, kuongea (hata kwa kiswahili) not amount of words she can speak or for how long she can speak, but substance of what she has spoken. Hapo ndio kuna tatizo.
tunaweza kujua yeye ni nani akilini mwake.
Tuangalie aliingia kwenye ofisi alizoingia kwa njia gani. was it for merit, Know how or was for know who.
Kufaulu mitahini na kupata certificates kunawezekana kwa strategies nyingi tu, so vyeti peke yake si kigezo. Tuangalie rekodi ya jumla ya utendaji wake, tusimhukumu kwa kiingereza tu