Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Wanamke mmoja (35) mkazi wa kijiji cha Iyula kata ya Msia wilayani Mbozi mkoani Songwe amekutwa amefariki dunia baada ya kuangukia katika mto mdogo wa Jodan uliopo katika mtaa wa Keselia kwenye Halmashauri ya mji wa Tunduma mkoani Songwe.
Richard Mwampashe ni kaka wa marehemu ambaye anasema dada yake alikuja kuhani msiba wa mtoto wake na kwamba kwa mara ya mwisho mwanamke ameaga kwenda ng'ambo ya kijiji jirani kwenye vilabu vya pombe ambapo hakuweza kurudi nyumbani baadae ikabainika alifia mtoni.
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Songwe Mathius Nyange amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema marehemu alienda kulewa pombe ambazo zilimzidi kiasi cha kushindwa kuvuka daraja na kuteleza kisha kupoteza maisha ambapo mwili wake umehifadhiwa katika kituo cha afya Tunduma kwa uchunguzi zaidi.
Baadhi ya wananchi wamesema marehemu alikunywa pombe kupindukia na kushindwa kuvuka daraja hilo huku wakilalamikia muundombinu mbovu wa daraja ambapo tukio hilo limetokea na kuitaka serikali iufanyie marekebisho.ili kuepusha matukio ya aina hiyo.
Aidha kamanda Nyange ametoa wito kwa jamii kuepuka unywaji wa pombe uliokithiri kiasi cha kushindwa kujitambua.
Chanzo: ITV
Richard Mwampashe ni kaka wa marehemu ambaye anasema dada yake alikuja kuhani msiba wa mtoto wake na kwamba kwa mara ya mwisho mwanamke ameaga kwenda ng'ambo ya kijiji jirani kwenye vilabu vya pombe ambapo hakuweza kurudi nyumbani baadae ikabainika alifia mtoni.
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Songwe Mathius Nyange amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema marehemu alienda kulewa pombe ambazo zilimzidi kiasi cha kushindwa kuvuka daraja na kuteleza kisha kupoteza maisha ambapo mwili wake umehifadhiwa katika kituo cha afya Tunduma kwa uchunguzi zaidi.
Baadhi ya wananchi wamesema marehemu alikunywa pombe kupindukia na kushindwa kuvuka daraja hilo huku wakilalamikia muundombinu mbovu wa daraja ambapo tukio hilo limetokea na kuitaka serikali iufanyie marekebisho.ili kuepusha matukio ya aina hiyo.
Aidha kamanda Nyange ametoa wito kwa jamii kuepuka unywaji wa pombe uliokithiri kiasi cha kushindwa kujitambua.
Chanzo: ITV