Somo la uzalendo 🇹🇿 🇺🇸

Somo la uzalendo 🇹🇿 🇺🇸

Uzalendo wa mtu kwa nchi yake uko kwenye vitendo vyake, matamshi yako na hata anavyojisikia moyoni mwake kuliko kwenye viashiria kama bendera na nyimbo ya taifa.

Na ukumbuke viashiria kama bendera au nyimbo za taifa kila nchi ina utaratibu wake, nchi kama Marekani hairuhusi kuinamisha bendera yao chini lakini nchi zingine duniani hawajali hilo.
 
Ramani tumechorewa,mfumo wa utawala tumewekewa , bendera yenyewe haina hata miaka 60...huo uzalendo ni wa nini hasa??
 
Tanzania nadhani ukipeperusha bendera nyumbani kwako huo ni msala...kama unabisha jaribu uone?

Ova
 
NAKAZIA:
TUKILINGANISHA DEMOKRASIA YETU NA MAREKANI TUSISAHAU KULINGANISHA NA UZALENDO WETU NA WAO.
 
Kwani unadhani Marekani kila raia anakubaliana na viongozi waliopo madarakani?

Umewahi kuona kwenye hafla ya kitaifa ya Marekani watu wanavaa nguo za vyama? Umewahi kuona huko Marekani vyombo vya dola kuonyesha wazi wazi kufanya upendeleo kwa chama kilicho madarakani? Umekosa vya kufananisha au na wewe unataka uonekane unajua kuanzisha uzi?
 
Kama ni hivyo basi hamna hata haja ya kuwa na bendera, siyo?

Kwani bendera ndio kipimo cha uzalendo zaidi ya alama ya taifa? Kwa hiyo ili ujue mtu ni mzalendo ni kwa kuweka bendera ya taifa alipo?
 
Hii Mada Ya Kuonyesha Uzalendo Kwa Kupeperusha Bendera Imenikaa Kwa Kweli.,,,,,,,wakuu Niombe Kuuliza Hivi Ikitokea Umeamua Kumiliki Bendera Yako Kiuzalendo ,,Taratibu Za Kuipandisha Na Kuishua Kila Siku Zitakuwa Ni Zile Zile Za Kupuliza Filimbi Ili Watu Wapitao Karibu Na Makazi Yako Wasimame Au Waweza Kuishusha Kiholela Tuu,,,,,, Halafu Nipende Kujuzwa Bei Ya Bendera 1 Na Mahali Pa Kuipata Hata Kama Ni Kwa Kufuata Taratibu
 
Hii Mada Ya Kuonyesha Uzalendo Kwa Kupeperusha Bendera Imenikaa Kwa Kweli.,,,,,,,wakuu Niombe Kuuliza Hivi Ikitokea Umeamua Kumiliki Bendera Yako Kiuzalendo ,,Taratibu Za Kuipandisha Na Kuishua Kila Siku Zitakuwa Ni Zile Zile Za Kupuliza Filimbi Ili Watu Wapitao Karibu Na Makazi Yako Wasimame Au Waweza Kuishusha Kiholela Tuu,,,,,, Halafu Nipende Kujuzwa Bei Ya Bendera 1 Na Mahali Pa Kuipata Hata Kama Ni Kwa Kufuata Taratibu

Maswali yako yamenichekesha ingawa ni ya msingi.
 
Ukitembea sehemu mbalimbali Tanzania pia utaona bendera za CCM zinapepea kwenye nyumba nyingi ,magari mengi nimeyaona yakiwa na bendera na nembo za CCM, ofisi nyingi zina picha ya Mh.Rais,huu wote sio uzalendo kwako?
Kwangu elimu haina darasa. Elimu haina kuhitimu wala wahitimu. Elimu ni jambo endelevu.

Moja ya elimu yangu ninayojivunia ni fursa niliyoipata ya kuweza kutembelea sehemu mbalimbali hapa duniani. Na si kutembelea tu, bali hata kuishi na kufanya kazi.

Kati ya somo nililoweza kujifunza ni hili la kitu kinachoitwa uzalendo.

Uzalendo huu nauzungumzia katika muktadha wa nchi mbili: Tanzania na Marekani.

Kwa yeyote ambaye kaishi Marekani na Tanzania kwa muda wa kutosha [fanya makadirio yako mwenyewe muda wa kutosha ni kiasi gani], atakubaliana na mimi kuwa Wamarekani wapo kwenye kiwango kingine kabisa katika kuonyesha fahari ya uzalendo kwa nchi yao.

Katika utaifa wa kisasa, bendera huwa ndo alama bainishi ya nchi/ taifa.

Wamarekani wengi, bila kujali wanatoka kwenye kada ipi, ni watu wanaolipenda kwelikweli taifa lao.

Na mapenzi hayo huonyeshwa na vile ambavyo hupenda kupeperusha bendera ya taifa lao.

Iwe ni kwa watu wenye kipato cha chini, cha kati, cha juu na kadhalika, uzalendo wao huonyeshwa na vile wanavyopeperusha bendera yao kwenye makazi yao, kwenye magari yao, sehemu zao za kazi na biashara, na kadhalika.

Ona mfano huu kwa mfano. Kwa muonekano tu wa mazingira, hapo panaonekana ni eneo la watu wenye kujiweza.


View attachment 1149927


Sasa hebu angalia na hii. Kwa muonekano tu unaweza kuhitimisha kuwa aishiye hapo si mtu wa kipato kikubwa. Ni ki trailer tu kilichojichokea.

View attachment 1149929

Sasa jiulize ni kitu gani hapo unachokiona kilichopo kwenye picha zote mbili? Ni bendera!

Uzalendo wa hivi bado sijauona Tanzania. Sababu hasa sijui ni ipi.

Hivi kwa mfano nikiamua kuweka kamlingoti kadogo nyumbani kwangu halafu nipeperushe bendera yetu ya Tanzania, nitasumbuliwa na watu wasiojulikana licha ya kwamba lengo langu la kufanya hivyo ni uzalendo?

Hili suala la bendera na uzalendo Mzee Mwanakijiji aliwahi kulidokeza siku za hapo nyuma.
 
Rangi za bendera ya Marekani ziko hadi kwenye chupi, vaa chupi yenye rangi za bendera ya Tanzania kama hujabambikiwa kesi eti umeidharau bendera ya Tanzania.

Tanzania kwa miaka mingi ilikuwa ni kuinajisi bendera ya Taifa ikitumika tofauti na majengo ya serikali na mashule.
Nadhani ilikuwa jinai hata kuwanayo tu bendera,wakati wenzetu wakitumia kutengeneza hadi mavazi,na vitu mbalimbali vya urembo.
Nakubali kwa Marekani na Brasil(z) ndiyo nchi zilizo juu sana kwa matumizi ya bendera zao kama alama ya uzalendo,Brazil mtu anavaa chini rangi ya kijani na juu atavaa njano au atachanganya anavyoona inapendeza ilimradi amevaa alama za Taifa lake.
Haya ya kwetu sasahivi ndiyo kidogo yamelegea lakini ilikuwa ni kitu kizito na kigumu kuamua kukitumia.
 
Back
Top Bottom