Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,080
- 136,564
- Thread starter
- #21
Zungumza kiswahili we mnyantuzu
Bhe nang’ho ka lekaga shi amakelege gako.
Zungumza kiswahili we mnyantuzu
Na wewe mara mia shenzi kabisaBhe nang’ho ka lekaga shi amakelege gako.
Na wewe mara mia shenzi kabisa
Acha ugomvi🤣🤣
Tanzania nadhani ukipeperusha bendera nyumbani kwako huo ni msala...kama unabisha jaribu uone?
Ova
Unataka kusema nini? Hata kama hawakubaliani na viongozi wao lakini si viongozi katili Kama Magufuli na wenye kauli za hovyo Kama MagufuliKwani unadhani Marekani kila raia anakubaliana na viongozi waliopo madarakani?
😂😂😂 .....?Sema tu unataka kutuonyesha unaishi marekani, tunawajua nyie wanyantuzu
Kwani unadhani Marekani kila raia anakubaliana na viongozi waliopo madarakani?
Kama ni hivyo basi hamna hata haja ya kuwa na bendera, siyo?
Kwani Marekani kuna amani na upendo tele?
Hii Mada Ya Kuonyesha Uzalendo Kwa Kupeperusha Bendera Imenikaa Kwa Kweli.,,,,,,,wakuu Niombe Kuuliza Hivi Ikitokea Umeamua Kumiliki Bendera Yako Kiuzalendo ,,Taratibu Za Kuipandisha Na Kuishua Kila Siku Zitakuwa Ni Zile Zile Za Kupuliza Filimbi Ili Watu Wapitao Karibu Na Makazi Yako Wasimame Au Waweza Kuishusha Kiholela Tuu,,,,,, Halafu Nipende Kujuzwa Bei Ya Bendera 1 Na Mahali Pa Kuipata Hata Kama Ni Kwa Kufuata Taratibu
Kwangu elimu haina darasa. Elimu haina kuhitimu wala wahitimu. Elimu ni jambo endelevu.
Moja ya elimu yangu ninayojivunia ni fursa niliyoipata ya kuweza kutembelea sehemu mbalimbali hapa duniani. Na si kutembelea tu, bali hata kuishi na kufanya kazi.
Kati ya somo nililoweza kujifunza ni hili la kitu kinachoitwa uzalendo.
Uzalendo huu nauzungumzia katika muktadha wa nchi mbili: Tanzania na Marekani.
Kwa yeyote ambaye kaishi Marekani na Tanzania kwa muda wa kutosha [fanya makadirio yako mwenyewe muda wa kutosha ni kiasi gani], atakubaliana na mimi kuwa Wamarekani wapo kwenye kiwango kingine kabisa katika kuonyesha fahari ya uzalendo kwa nchi yao.
Katika utaifa wa kisasa, bendera huwa ndo alama bainishi ya nchi/ taifa.
Wamarekani wengi, bila kujali wanatoka kwenye kada ipi, ni watu wanaolipenda kwelikweli taifa lao.
Na mapenzi hayo huonyeshwa na vile ambavyo hupenda kupeperusha bendera ya taifa lao.
Iwe ni kwa watu wenye kipato cha chini, cha kati, cha juu na kadhalika, uzalendo wao huonyeshwa na vile wanavyopeperusha bendera yao kwenye makazi yao, kwenye magari yao, sehemu zao za kazi na biashara, na kadhalika.
Ona mfano huu kwa mfano. Kwa muonekano tu wa mazingira, hapo panaonekana ni eneo la watu wenye kujiweza.
View attachment 1149927
Sasa hebu angalia na hii. Kwa muonekano tu unaweza kuhitimisha kuwa aishiye hapo si mtu wa kipato kikubwa. Ni ki trailer tu kilichojichokea.
View attachment 1149929
Sasa jiulize ni kitu gani hapo unachokiona kilichopo kwenye picha zote mbili? Ni bendera!
Uzalendo wa hivi bado sijauona Tanzania. Sababu hasa sijui ni ipi.
Hivi kwa mfano nikiamua kuweka kamlingoti kadogo nyumbani kwangu halafu nipeperushe bendera yetu ya Tanzania, nitasumbuliwa na watu wasiojulikana licha ya kwamba lengo langu la kufanya hivyo ni uzalendo?
Hili suala la bendera na uzalendo Mzee Mwanakijiji aliwahi kulidokeza siku za hapo nyuma.
Tanzania kwa miaka mingi ilikuwa ni kuinajisi bendera ya Taifa ikitumika tofauti na majengo ya serikali na mashule.
Nadhani ilikuwa jinai hata kuwanayo tu bendera,wakati wenzetu wakitumia kutengeneza hadi mavazi,na vitu mbalimbali vya urembo.
Nakubali kwa Marekani na Brasil(z) ndiyo nchi zilizo juu sana kwa matumizi ya bendera zao kama alama ya uzalendo,Brazil mtu anavaa chini rangi ya kijani na juu atavaa njano au atachanganya anavyoona inapendeza ilimradi amevaa alama za Taifa lake.
Haya ya kwetu sasahivi ndiyo kidogo yamelegea lakini ilikuwa ni kitu kizito na kigumu kuamua kukitumia.