Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,088
- 136,599
Kwangu elimu haina darasa. Elimu haina kuhitimu wala wahitimu. Elimu ni jambo endelevu.
Moja ya elimu yangu ninayojivunia ni fursa niliyoipata ya kuweza kutembelea sehemu mbalimbali hapa duniani. Na si kutembelea tu, bali hata kuishi na kufanya kazi.
Kati ya somo nililoweza kujifunza ni hili la kitu kinachoitwa uzalendo.
Uzalendo huu nauzungumzia katika muktadha wa nchi mbili: Tanzania na Marekani.
Kwa yeyote ambaye kaishi Marekani na Tanzania kwa muda wa kutosha [fanya makadirio yako mwenyewe muda wa kutosha ni kiasi gani], atakubaliana na mimi kuwa Wamarekani wapo kwenye kiwango kingine kabisa katika kuonyesha fahari ya uzalendo kwa nchi yao.
Katika utaifa wa kisasa, bendera huwa ndo alama bainishi ya nchi/ taifa.
Wamarekani wengi, bila kujali wanatoka kwenye kada ipi, ni watu wanaolipenda kwelikweli taifa lao.
Na mapenzi hayo huonyeshwa na vile ambavyo hupenda kupeperusha bendera ya taifa lao.
Iwe ni kwa watu wenye kipato cha chini, cha kati, cha juu na kadhalika, uzalendo wao huonyeshwa na vile wanavyopeperusha bendera yao kwenye makazi yao, kwenye magari yao, sehemu zao za kazi na biashara, na kadhalika.
Ona mfano huu kwa mfano. Kwa muonekano tu wa mazingira, hapo panaonekana ni eneo la watu wenye kujiweza.
Sasa hebu angalia na hii. Kwa muonekano tu unaweza kuhitimisha kuwa aishiye hapo si mtu wa kipato kikubwa. Ni ki trailer tu kilichojichokea.
Sasa jiulize ni kitu gani hapo unachokiona kilichopo kwenye picha zote mbili? Ni bendera!
Uzalendo wa hivi bado sijauona Tanzania. Sababu hasa sijui ni ipi.
Hivi kwa mfano nikiamua kuweka kamlingoti kadogo nyumbani kwangu halafu nipeperushe bendera yetu ya Tanzania, nitasumbuliwa na watu wasiojulikana licha ya kwamba lengo langu la kufanya hivyo ni uzalendo?
Hili suala la bendera na uzalendo Mzee Mwanakijiji aliwahi kulidokeza siku za hapo nyuma.
Moja ya elimu yangu ninayojivunia ni fursa niliyoipata ya kuweza kutembelea sehemu mbalimbali hapa duniani. Na si kutembelea tu, bali hata kuishi na kufanya kazi.
Kati ya somo nililoweza kujifunza ni hili la kitu kinachoitwa uzalendo.
Uzalendo huu nauzungumzia katika muktadha wa nchi mbili: Tanzania na Marekani.
Kwa yeyote ambaye kaishi Marekani na Tanzania kwa muda wa kutosha [fanya makadirio yako mwenyewe muda wa kutosha ni kiasi gani], atakubaliana na mimi kuwa Wamarekani wapo kwenye kiwango kingine kabisa katika kuonyesha fahari ya uzalendo kwa nchi yao.
Katika utaifa wa kisasa, bendera huwa ndo alama bainishi ya nchi/ taifa.
Wamarekani wengi, bila kujali wanatoka kwenye kada ipi, ni watu wanaolipenda kwelikweli taifa lao.
Na mapenzi hayo huonyeshwa na vile ambavyo hupenda kupeperusha bendera ya taifa lao.
Iwe ni kwa watu wenye kipato cha chini, cha kati, cha juu na kadhalika, uzalendo wao huonyeshwa na vile wanavyopeperusha bendera yao kwenye makazi yao, kwenye magari yao, sehemu zao za kazi na biashara, na kadhalika.
Ona mfano huu kwa mfano. Kwa muonekano tu wa mazingira, hapo panaonekana ni eneo la watu wenye kujiweza.
Sasa hebu angalia na hii. Kwa muonekano tu unaweza kuhitimisha kuwa aishiye hapo si mtu wa kipato kikubwa. Ni ki trailer tu kilichojichokea.
Sasa jiulize ni kitu gani hapo unachokiona kilichopo kwenye picha zote mbili? Ni bendera!
Uzalendo wa hivi bado sijauona Tanzania. Sababu hasa sijui ni ipi.
Hivi kwa mfano nikiamua kuweka kamlingoti kadogo nyumbani kwangu halafu nipeperushe bendera yetu ya Tanzania, nitasumbuliwa na watu wasiojulikana licha ya kwamba lengo langu la kufanya hivyo ni uzalendo?
Hili suala la bendera na uzalendo Mzee Mwanakijiji aliwahi kulidokeza siku za hapo nyuma.