Somo kutoka uyahudi

Gulwa

JF-Expert Member
Jun 16, 2008
9,790
14,873
Mwanzoni mwa karne ya kwanza huko uyahudi alitokea kijana mdogo aliyejitokeza kupinga na kukosoa baadhi ya taratibu dini ya kiyahudi. Kutokana na umahiri wake katika kuhubiri alifanikiwa kupata wafuasi wengi na kuonekana ni tishio kwa dini na uongozi wa wakati huo.

Viongozi walikaa chini na kuona ni jinsi gani ya kumdhibiti kabla hali haijawa mbaya zaidi. Waliamua kumutengenezea mashtaka ya uongo na wakafanikiwa kuhukumu adhabu ya kifo, akauawa.

Baada ya kifo chake viongozi walisherehekea na kujipongeza kwa kumdhibiti mazushi huyo. Ajabu ni kwamba mpaka sasa zaidi ya miaka 2000 baadaye bado mafundisho na mahubiri yake ni maarufu zaidi duniani kuliko ya binadamu yeyote aliyewahi kuonekana kwenye uso wa dunia.

Kumbe kufungulia watu mashtaka ya uongo hakujawahi kuzima mahitaji ya wakati husika. Tumeona Afrika kusini, Zimbabwe nk. Tanzania je watafanikiwa na kubadili historia?
 
Wanajidanganya tu! Nafasi ambayo ameipata huyu MAMA ningeipata mimi! Hakika ningejiandikia na mimi kahistoria kangu kazuri, ka kuja kukumbukwa vizazi na vizazi!

Ningeangalia tu hitaji kuu la Watanzania walio wengi kwa sasa ni nini? Kujenga uchumi ambao ulishajengwa tangu miaka ya 1960's, au Katiba Mpya ambayo itarejesha matumaini mapya kwa Watanzania walio wengi?

Baada ya hapo, naamini Watanzania wangenikumbuka milele! Ningeweka mifumo ya haki na usawa kwa Watanzania wote (ingawa natambua fika watu kama akina mwigulu na ubinafsi wao wasingekubali), na ningeimarisha uzalendo wa kweli na kwa vitendo!

MAMA, bado hujachelewa! Do something!! Unadhani ukiwapatia Watanzania Katiba Mpya, hayo Makongamano mnayo yapiga marufuku kupitia policcm, yatatokea wapi?
 
Back
Top Bottom