Adrienne akamwambia Shawn kuwa wanasafiri na marafiki zake kwenda kijijini kusalimia wazazi wa Doreen, Shawn akawauliza mnaendaje, Adrienne akamjibu tunaenda na bus za kawaida, Mmasai Shawn kupenda masifa akamwomba awapeleke na gari, Adrienne akakataa, mmasai aka-insist awapeleke, Adrienne akamwambia lakini safari ni ndefu utaweza kweli kuendesha gari, Shawn anajigamba mimi tena, hapa ni full mass nondo wakacheka, Adrienne akamjibu ngoja nitaongea na Chanel naona ana gari jipya kama atakubali twende nalo,
Huku bondeni malavi davi kwa sana, George hataki kumwachia Carrie and vice versa utadhani bolt na nut, wamegandana kama bigjii na meza, Carrie ameshaonyeshwa mali zote za George za Africa kusini, kesharithishwa kila mali za George, na Carrie akamwelezea kuhusu assets zake za Tanzania, George akamtania kumbe na mimi mkali ee? Akawa anajitamba. George akamwelekeza ku invest katika hisa, akamwambia kuna hisa zinauzwa Tanzania nataka kwenda kuzinunua, unaonaje ukiuza bar zako nakampuni ya usafi ukaziweka baadhi ya pesa kwenye hisa na ukanunua nyumba ukapangisha? Maana umesema kuendesha bar inakusumbua na watu wa usafi sio yakinifu katika kazi, we mtoto mzuri hautakiwi kukaa kwenye jua tena na huu mri wako, unatakiwa uwe na akaunt swizz bank tayari, invest big achana na akili ndogo, Carrie akawa mdogo anasikiliza darasa, mmakua ana nondo za investment kama nini. Carrie akamwambia sasa tunafanyaje na harusi? Inafanyika Tanzania au hapa? Maana hata sijawaambia wazazi wangu na lazima nikupeleke kijijini kwetu wazazi wakakuone na dada zangu, George akamwambia wazazi wangu watafurahi kuja Tanzania wamekaa huku zaidi ya miaka 20, na nimeshawanunualia nyumba Tanzania mikocheni, harusi itabidi ifanyike Tanzania lakini mwakani, kwa sasa tumeshachelewa kujipanga, ila Christmass itabidi tule wote huku na wazazi wakufahamu mkwe wao, wakapanga na kupangua weee na mechi juu.
Doreen amekaa mwenyewe nyumbani upweke umemjaa, imeshapita wiki hajamsikia James, akitaka kumpigia roho inasita, akakumbuka zile mil 3 aliomuomba, akaona akipiga kumkumbushia mil 3 ataonekana low class nay eye hakutaka, akampigia Adrienne kumwomba amsaidie mil 3, Adrienne akamwambia alafu Shawn anataka kuja kwenye safari yetu, ame offer ku drive mpaka singida ila na mimi nitamsaidia ongea na bibie Chanel twende na gari yake, Doreen akamwuliza Shawn yupi tena? Adrienne akamwelezea, Doreen akacheka sana, shogangu una kismati, juzi tu hata wiki 2 hazijapita ulikuwa kama mjane unalia lia leo unacheka, mmeshatiana nini!?
Adrienne: bwana tutaongea tukionana mepnzi kwahiyo keshoi kutwa safari saa ngapi sasa?
Doreen: alfajiri saa 12 na uache uvivu uamke mapema huyo bwana akuamshe mapema ivo, kule ni mbali asee. Mimi nitakuwa na chanel hapa kwangu maana kesharudisha nyumba anatafuta nyumba nyingine, ila amelala sasa, anajiandaa kwenda kazini mchana ndio siku ya mwisho kwake anachukua likizo kesho akiamka nitamwambia ujumbe wako. Simu ikakatwa
Chanel: nikiamka utaniambia nini? Akamwuliza Doreen
Doreen: akamwelezea yote ambayo Adrienne alimwambia, unajua Adrienne keshapata bwana wa kimasai anaitwa Shawn, na ndio amejitolea kutuendesha na gari yako mpaka singida na kurudi
Chanel: akaweka mikono kichwani, che! Si juzi tu alikuwa analia? Kweli huyu msukuma ana nyota kali! Am happy for her, gari ipo kwa Carrie ila ameniachia funguo ya nyumba yake, itabidi nikachukue funguo wa gari nyumbani kwa Carrie nimpelekee Adrienne nikamwone na huyo shemeji wa wiki 1. I hope hatomzingua tena Adrienne
Doreen: sasa mami inakuwaje kuhusu issue yako mpendwa wangu? Unataka kuwa spinster kama mimi?
Chanel: bwana sitaki kuongelea hili swala la hao mabwana, nimewarusha ndege wote juu atakayerudi atakuwa wa kwangu Mungu kanipangia. Mara simu ya Chanel ikaita, ni Pedeshee, akaipokea akamweka loud speaker, nambie Marion, naona leo umenikumbuka
Pedeshee: baby sijalala wiki nzima nakuwaza wewe tu, sina raha kabisa, yani nakupend…. Ile hajamalizia sentensi Chanel kusikia neon nakupe… akamkatia simu
Doreen: wewe vepe mbona umemmkatia simu mwenzio? Una kichaa au?
Chanel: yani nikilisikia neon Nakupenda kwa mara nyingine tena nahisi ningetapika, what is Love?! am beginning to resent LOVE!
Doreen: mwenzetu una trust issues ikija kwenye swala la mapenzi sio? Haya mapenzi yamekufanya nini? Chanel akamwelezea wapi waliagana na neon Love / Nakupenda. Na hakutaka kuonana nalo tena maana lilimtesa vibaya mno, yeye yupo radhi ale raha ila asiambiwe nakupenda.
Doreen akajaribu kuongea nae na kumwelewesha kuhusu mapenzi na upendo na yafananayo, akamwambia sasa ulienda kumwomba Mungu akupe gogo au chuma? Utaingiaje kwenye ndoa kama haupendwi, kwani wewe ni mtumwa au changudoa?, Chanel darasa likamkolea,kwahiyo ukiambiwa nakupenda unajibuje mami? Chanel akacheka, eti najibu nakupenda pia, uuuuwi huku anacheka, Doreen akamwambia unaona sasa? Kumbe sio mbaya ee si unaona mpaka ukismile unapendeza usoni unang’aa, sasa hawa mabwana wawili nani anakupenda zaidi?
Kwakweli Pedeshee naona ananipenda kikwelii, ila sasa sijui ukweli kuhusu biashara zake, asije akawa jambazi maana zote anazifanyia nje ya Tanzania, sasa sijui kama ni halali, ila Mark sijui kuhusu upendo wake, labda nimtafute baby mama mke wake niongee nae nijue kwanini wameachana, maana muda mwingi yupo controlling, kila kitu nifanye kwakufuatia anachotaka yeye, najiona kama sina uhuru kwake, ila kwa Marion, akawa anasmile, Doreen akawa anamwangalia huku ana smile, Yule mlugulu ni noma hata hanisumbui, nakuwa myself nikiwa nae, naweza hata kujamba na nisiogope ila kwa Mark ah yule mkali hata simwelewi, naona upendo zaidi kwa Mario lakini sio Mark, ila Marion mfuuupi mpaka naona aibu.
Doreen: haya mama nadhani umeshajijibu na utajua cha kufanya, mimi nataka uwe happy umelala wiki 2 unalia huku ndani usiku kucha nakusikia, nikija kukugongea unanyamaza, mtafute Mario wako akupe dudu kabla hatujaenda Singida usije ukaenda kubaka wanyama na wana kijiji kule buree! Ila usije ukawa unampenda Marioo kwa pesa zake buree maana hizo uwa zipo na zinaweza kukata baadae, am just saying, haya mapenzi ya pesa ndio siyawezi asee, lakini hauwezi uzuia moyo, umpende akiwa nazo na asipokuwa nazo, alafu zijue assets zake zipo vipi msije mkatuletea aibu hapa kama ni punda ujing’atue mapemaa maana hilo litakuwa balaa, kuhusu ufupi sasa hapo sijui waswahili wanasema ukipenda boga penda na maua yake..
Chanel: eh we mama una mashauri mengi James umembwaga wapi labda? Sijamwona tangu nije hapa!
Doreen: huyu nae anadhani anafanana na huyo mpare wako, controlling na mimi siwezi kabisa mwanaume wa ivyo, nilimpa uhuru wangu akanicontrol kama mtumwa, sasa nikaamua kumkazia akanuna, ndio kaondoka, afu nilimwomba mil 3 kumtest mpaka leo kimya sijui napeleka nini kwa wazee hii aibu. Aya mami jiandae uende ofisini ukaombe ruhusa uonane na huyo Mrs Shawn na Mrs Mark mimi nipo tu ndani leo hata sitoki nitakuwa napaki hapa.
Chanel akaenda ofisini akaomba likizo ya wiki 2, akaenda nyumbani kwa Carrie akachukua funguo wa gari yake akampelekea Adrienne akamkuta yupo na Shawn wanakula hotelini, Adrienne akiwa na furaha sana, akashangaa huyu Shawn mchawi nini, ndani ya wiki mbili rafkietu anacheka, kweli huu ni mwujiza, akawasogelea we Adrienne nimekupigia wala haupokei kumbe unatongozwa kimwili na huyu bwashee, anaitwa?
Adrienne: karibu rafkiangu huku anamkumbatia, karibu ukae, Chanel anashangaa Adrienne imekuwaje?! Akatambulishwa Shawn and vice versa!
Chanel: nimefurahi kukufahamu Shawn, karibu kwenye ukoo wetu wa marafiki wa 4, sasa Adrienne mimi sion mkaaji sana, nimekuletea funguo wa gari tunasafiri keshokutwa saa 12 alfajiri, mkachukue gari nyumbani kwa Carrie, maana mimi mweupee sijui chochote kuhusu magari, I hope kila kitu kitakuwa in order though! Akambusu Adrienne kichwani akamwambia am happy for you Chicca! Bye Shawn, nimefurahi kukuona.
Bonbdeni mapenzi yakawa mapenzi, Carrie kaenda kutambulishwa kwa wazazi kabla ya Christmass kufika maana sio kwa mauno yale aliompa George. Wazai wakafurahi kuletewa mkwe wa kitanzania, ndio ilikuwa ndoto yao na maombi yao, wakampenda Carrie alivyo, anavyoongea, Carrie akawaletea na zawadi za Kitanzania, wazazi wakachizika, jamani mkwe anaupendo, mtoaji mzuri, kweli mwanetu yupo pazuri.
James akaonekana yupo buzy na kuandaa mazingira ya Lucifer January, moyoni anamkumbuka Doreen lakini wapi, anajikaza kiume anaumia, kila akitaka kumpigia simu amem-miss anashindwa, sio kwa madharau yale alionionyesha, nimehangaika kumletea chakula anajua natoa wapi hela, sio kwa madharau yale, anaweka simu pembeni anaendelea na kazi huku anakula mziki. Baadae akaona simu inaita, namba ngeni, akapokea, akasikia sauti ya mwanamke akamwuliza wewe ni nani? Akajibu mimi Chanel, nahitaji kukuona tafadhali, uko wapi? James akamjibu nipo ofisini, kama unaweza kuja njoo akamuelekeza.
Chanel akatua kwenye mjengo anaofanyia kazi James, pazuuuri kweli anapashangaa, akamwona James anamsubiri reception, wakasalimiana, Chanel hakumpendaga James kwasababu ya majibu yake ya kishenzi kuhusu Adrienne lakini akajikaza ivyo ivyo akaenda kuongea nae, James alaikuwa anampenda sana Chanel, anamwonaga mjanja bingwa, hajazubaa, sio kwa kuwa na wanaume zaidi ya mmoja alafu hawajuani wala nini, akamkaribisha ofisini kwake
Chanel: ofisi yako nzuri jamani utadhania ulaya
James: akawa anacheka asante, karibu Chanel
Chanel: shem umepotea sana, sikuoni nyumbani au umepata nyumba ndogo? Rudi bwana nyumbani
James: aka, rafiki yako hajisomi, nimeamua kumuacha kwanza aendelee kivyake
Chanel: jamani shemeji, rafiki yangu hana raha amekumiss, anakupenda si unajua wewe ndio ulikuwa 1st man wake, jamani mbona unamtesa ivyo rafiki yangu? Au unataka afe? Akamdanganya usiku hata halali analia tu, wiki ya pili, nikienda kumgongea mlango hafungui ananyamaza kimya, jamani shem si mrudiane tu lakini au unataka rafiki yangu awe kichaa? Yule ameshakuwa ndugu yangu kabisaa sitaki kumpoteza
James: si ameenda kwao singida sijui mtwara
Chanel: ai James jamani yani hata kujua anaenda wapi haujui?! Haya bwana mimi ngoja niende, tunaondoka kwenda singida kesho kutwa, mtafute umuage, uje kabisa kulala jamani tunakupenda karibu sana, huku anaondoka
James: asante shemeji nitafikiria karibu sana na safari njema.
Safaree na Stan wameshafika Dubai, Kimaro kawapokea, karibuni sana vijana, karibuni hii ndio palace yangu, nimeinunua wiki 2 zilizopita, akina Safaree wanapashangaa pazuuuri kama jumba la mfalme, kweli kazi inalipa, wakaonyeshwa pa kulala kila mtu na pake, baadae wakaitwa kula chakula, usiku wakatoka kwenda club, kila mmoja akaandaliwa demu wa kutanua nae, Safaree anafurahi maisha ndio haya, Stan anaona kama muujiza, kha pazuri Dubai kweli hii ndio middle east, pazuri sijui ulaya itakuwaje, vijana wakala bata kama hamna kesho, kwenye strip clubs wanamwaga hela kama Jay Z, Safaree amechizika mademu wa kila aina, wanamwaga mahela kama kwenye miziki ya mamtoni, wanakunywa ma wine expensive, Kimaro anawaangalia anacheka, kuleni vijana mnastahili mmezifanyia kazi kwa shida!
Safari ikawadia ya kwenda kijijini singida, wasafiri wamejiandaa wameshapendeza, Shawn kaja kwa Doreen kuwapitia akiwa na Adrienne, wanapendaana wenyewe, Chanel akamwuliza ushalala na huyu bwana au bado uko bikira? Adrienne akasmile, labda mechi ya kwanza itakuwa kijijini porini. Wakawa wanapaki mizigo kwenye gari Shawn anawasaidia, wakamaliza wanataka kutoka, mara wanamwona James huyo anaingia na sanduku, akawaambia na mimi mnataka kuniacha pia? Hamjui kuwa safari haitanoga bila mimi, Doreen akafurahi kumwona akamkimbilia akamkumbatia.
ITAENDELEA SAA LEO 4 NANUSU USIKU