Money Penny
JF-Expert Member
- Jun 20, 2016
- 18,204
- 17,560
- Thread starter
- #21
Jumapili wakiwa kanisani, maana wote waliamua kwenda kusali kanisani kwa Doreen, wakati wa sadaka, wakiwa wanapita mbele kwenda kutoa sadaka, mara Adrienne akamwona James akiwa amekaa seat ya nyuma, akamfinya Carrie, “isn’t that James, the one who approached Doreen?!” Carrie akasema Yes, ndio mwenyewe, embu ngoja tukakae tutamcheki kwenye seat vizuri. Wakaenda kuketi, ilipofika zamu ya James kupita mbele, wote wakaambizana, muangalieni James, Doreen alishtuka, roho ikampasuka mpaka mwili ukaanza kutetemeka, akainama chini kujificha asionekane. Ibada ilipoisha, wakiwa wanasalimiana nje ya kanisa, akaja James kuwasalimia.
Adrienne akamwuliza James, are you stoking us? Au unasali hapa? James akamwambia, hapana sisali hapa, kuna rafkiangu amenikaribisha nije alafu yeye hajaja, ila sio mbaya, sikujua na nyie mnasali hapa, hello girls, and Doreen how are you? Nimesubiria simu yako sijakupata. Carrie akamjibu, hi James, tulilala hoi jana tukaamkia kanisani, so please forgive me. James akasema no problem, i understand. So Doreen nitapata namba yako sasa au? Doreen akasema hapana, am not into married men, sorry. James akamwuliza, who said anything about marriage? Am not married. Then Chanel, Adrienne na Carrie wakaangaliana, wakavutana pembeni wakawaacha wawili wakiongea. “Can I take you out for a brunch and lunch please?” Doreen akasema, “No thank you, nipo na marafiki zangu na tumepanga kwenda, kabla hajamaliza sentensi, marafikizake walikuwa wameshawasha gari wanaondoka, akasikia tu Bye Doreen”.
“Kwahiyo naona tupo wawili sasa, je twaweza kwenda kwa brunch?, tukimaliza nitakurudisha nyumbani au popote unapotaka”, akasema James. Doreen hakuwa na jibu ikabidi akubali kwenda na James huku akilaani moyoni mwake shenzi kabisa akina carrie watanikoma!
Sexy love, girl the things you do
(Oh baby baby) Keep me sprung, keep running back to you
Oh I love making love to you Babygirl you know you're my (sexy love)
Wimbo ulisikika wakiwa kwenye Gari ya James Wote wawili wakiwa kimya Kwa Muda mrefu, Doreen akiwa amegeukiwa upande wa dirishani huku anafinya violence, moyoni mwake anajiuliza hivi mimi nina kitu gani nafanana na huyu mbuzi beberu pori? Mwanaume mwenyewe hajui hate kuvaa. Kabahatisha tu kwenye Gari sijui ka rent mana wanaume wa duniani shida sana, Mungu wangu hii ishakuwa balaa sasa, huyu mwanaume ananiwekea nuksi ananiharibia maombi yangu,mwanaume mwenyewe kwanza mweusiiiiiii kama kuzimu.
Ivi nikijiangalia nilivyo mrembo namna hii nawaka hivi, huyu mwanaume atanipeleka wapi? He looks cheap to me. Kwanzaa nimesoma IST tangu nursery mpaka form 6, nikaenda University of London wapi na wapi? huyu mwanaume anaonekana kasoma kayumba tu, we have nothing in common anakitu gani anaweza kufanya cha kunishitua mimi Doreen, hapa duniani nimeona kila kitu kabla yake, kwanza nina wasiwasi na umri wake, yasije yakawa yale yale mambo ya Adrienne ya Pupils. MUNGU wangu, ivi hili jini umelileta kwangu la nini labda? ! Yani mimi nimekuomba mkate wewe umenipa jiwe?! What the hell?!
Kwenye Gari James alikuwa mwenye furaha sana, James Akajisemea moyoni kweli Mungu yupo, chuma kama hiki ningekipata wapi kudadeki?! Motto mwake, na hivi nimemuwekea mapigo ya mamtoni anafurahije sasa!? Akamuangalia Doreen akaona kama hayupo comfortable anajifinya vidole amegeukia pembeni, anang’ata mdomo, kama amekasirika anataka kulia, akapunguza sauti ya redio, akamwuliza, "Doreen, uko sawa? Doreen akajibu, sawa. Leo umependeza sana, inaelekea kupendeza ni kawaida yako maana hata jana ulikuwa zaidi. Ulipoingia tu pale hotelini na macho yangu yalipokuona moyo ulienda mbio Sana". Doreen akasmile akaendelea kukaa kimya, ila moyoni akajibu shenzi zako, mavi wee. Wakafika Sheraton hotel Muda wa saa 7 kasoro mchana, waiter akatokea, akawapa menu. Doreen akamwambia hapana mimi nahitaji 1 muffin and hot chocolate. Waiter akamwuliza James na wewe kaka? James akajibu bado nachagua kaka nivulie kidogo. Akaendelea kuchagua ndani ya dk 15, Doreen akajisemea moyoni, He is soo classless, yani hapa Mungu anamuumbua hatari, Doreen akawa ameshaletewa muffin na hot chocolate anakaribia kumaliza kula.
Waiter akaja, enhe kaka naamini mambo tayari sasa, ndio James akaagiza anavyotaka.
James akaanza maswali, nambie mrembo, unafanya shughuli gani hapa mjini?
Doreen akamjibu sifanyi shughuli yeyote. James akamwuliza inawezekana kweli, au unaishi na wazazi? Doreen akamwambia hapana wazazi wangu wapo mkoa, mimi naishi pekeyangu.
Ohoo! Sasa unaishije bila kazi au unafanya biashara? Akauliza James. Doreen akamjibu sina kazi, natafuta wala biashara sifanyi.
James akamwuliza, umesomea elimu gani? Akamjibu Degree ya finance and economy. James akamwambia basi nitumie cv yako na kila kitu kwenye email yangu, akatoa business card akampa, nitakuangalizia kwa marafiki zangu ajira, tuombe Mungu. Au ulikuwa unapenda kufanya kazi sehemu gani? Doreen akajibu, sehemu yoyote inayolipa vizuri nitashukuru, asante.
Huku nyuma, Chanel, Adrienne na Carrie wakawa wanamvutia picha Doreen, wakaanza kuwaza sasa hivi atakuwa analaani sio kitoto, utadhani hajatoka kanisani. Adrienne akasema I hope that guy is nice maana mimi namashaka nae, Doreen has been through a lot katika maisha yake, wala sitataka ateseke tena in future.
May be we should text her, it’s been hours hatujamsikia, huenda kawa kidnapped, akasema chanel. Carrie akamjibu, mtu mzima anakuwaje kidnapped samahani kweupe hivi, acheni utoto, mwacheni atarudi mwenyewe. Enhe sasa usiku tunaenda kujirusha wapi? Naona tupo wa 3 am sure Doreen atarudi na kusema amechoooka anataka kulala, na hivi kesho sikukuu mimi bado nataka kutoka. Leo wapi wapendwa? Akasema carrie.
Hata sijui, akajibu Adrienne, kwanini tusikae tu ndani au leo kuna bendi inapigwa? Twanga pepeta or something!?
Yah, twendeni kwenye bendi leo, akadakia Chanel, wakakubaliana wanaenda kwenye bandi ya twanga pepeta.
Huku nyuma stori kati ya Doreen na James zimenoga, walipotoka Sheraton wakaenda cocobeach kupunga upepo wakamalizia na slipway for ice cream. Doreen Kuangalia saa mkononi mwake akakuta saa 1 usiku, akakumbuka saa 2 usiku wanatakiwa kutoka na marafiki zake, akaangalia simu akakuta missed call 20 za Adrienne. Akaomba arudishwe nyumbani na James haraka, akadanganya kuna dharura nyumbani kwangu, unaona missed calls 20 nahisi kuna tatizo nyumbani.
Kufika nyumbani, Doreen akashuka haraka huku anakimbia kutoka kwenye gari, akamwambia James asanteeeeeeeeeeeeeeeee, usiku mwemaaaaaaaaa, byeeeeeee, akamuacha James ameduwaa hata kuzima gari akashindwa. James alitegemea good night kiss and hugs, akaambulia kelele za mrembo.
ITAENDELEA
Adrienne akamwuliza James, are you stoking us? Au unasali hapa? James akamwambia, hapana sisali hapa, kuna rafkiangu amenikaribisha nije alafu yeye hajaja, ila sio mbaya, sikujua na nyie mnasali hapa, hello girls, and Doreen how are you? Nimesubiria simu yako sijakupata. Carrie akamjibu, hi James, tulilala hoi jana tukaamkia kanisani, so please forgive me. James akasema no problem, i understand. So Doreen nitapata namba yako sasa au? Doreen akasema hapana, am not into married men, sorry. James akamwuliza, who said anything about marriage? Am not married. Then Chanel, Adrienne na Carrie wakaangaliana, wakavutana pembeni wakawaacha wawili wakiongea. “Can I take you out for a brunch and lunch please?” Doreen akasema, “No thank you, nipo na marafiki zangu na tumepanga kwenda, kabla hajamaliza sentensi, marafikizake walikuwa wameshawasha gari wanaondoka, akasikia tu Bye Doreen”.
“Kwahiyo naona tupo wawili sasa, je twaweza kwenda kwa brunch?, tukimaliza nitakurudisha nyumbani au popote unapotaka”, akasema James. Doreen hakuwa na jibu ikabidi akubali kwenda na James huku akilaani moyoni mwake shenzi kabisa akina carrie watanikoma!
Sexy love, girl the things you do
Oh I love making love to you Babygirl you know you're my (sexy love)
Wimbo ulisikika wakiwa kwenye Gari ya James Wote wawili wakiwa kimya Kwa Muda mrefu, Doreen akiwa amegeukiwa upande wa dirishani huku anafinya violence, moyoni mwake anajiuliza hivi mimi nina kitu gani nafanana na huyu mbuzi beberu pori? Mwanaume mwenyewe hajui hate kuvaa. Kabahatisha tu kwenye Gari sijui ka rent mana wanaume wa duniani shida sana, Mungu wangu hii ishakuwa balaa sasa, huyu mwanaume ananiwekea nuksi ananiharibia maombi yangu,mwanaume mwenyewe kwanza mweusiiiiiii kama kuzimu.
Ivi nikijiangalia nilivyo mrembo namna hii nawaka hivi, huyu mwanaume atanipeleka wapi? He looks cheap to me. Kwanzaa nimesoma IST tangu nursery mpaka form 6, nikaenda University of London wapi na wapi? huyu mwanaume anaonekana kasoma kayumba tu, we have nothing in common anakitu gani anaweza kufanya cha kunishitua mimi Doreen, hapa duniani nimeona kila kitu kabla yake, kwanza nina wasiwasi na umri wake, yasije yakawa yale yale mambo ya Adrienne ya Pupils. MUNGU wangu, ivi hili jini umelileta kwangu la nini labda? ! Yani mimi nimekuomba mkate wewe umenipa jiwe?! What the hell?!
Kwenye Gari James alikuwa mwenye furaha sana, James Akajisemea moyoni kweli Mungu yupo, chuma kama hiki ningekipata wapi kudadeki?! Motto mwake, na hivi nimemuwekea mapigo ya mamtoni anafurahije sasa!? Akamuangalia Doreen akaona kama hayupo comfortable anajifinya vidole amegeukia pembeni, anang’ata mdomo, kama amekasirika anataka kulia, akapunguza sauti ya redio, akamwuliza, "Doreen, uko sawa? Doreen akajibu, sawa. Leo umependeza sana, inaelekea kupendeza ni kawaida yako maana hata jana ulikuwa zaidi. Ulipoingia tu pale hotelini na macho yangu yalipokuona moyo ulienda mbio Sana". Doreen akasmile akaendelea kukaa kimya, ila moyoni akajibu shenzi zako, mavi wee. Wakafika Sheraton hotel Muda wa saa 7 kasoro mchana, waiter akatokea, akawapa menu. Doreen akamwambia hapana mimi nahitaji 1 muffin and hot chocolate. Waiter akamwuliza James na wewe kaka? James akajibu bado nachagua kaka nivulie kidogo. Akaendelea kuchagua ndani ya dk 15, Doreen akajisemea moyoni, He is soo classless, yani hapa Mungu anamuumbua hatari, Doreen akawa ameshaletewa muffin na hot chocolate anakaribia kumaliza kula.
Waiter akaja, enhe kaka naamini mambo tayari sasa, ndio James akaagiza anavyotaka.
James akaanza maswali, nambie mrembo, unafanya shughuli gani hapa mjini?
Doreen akamjibu sifanyi shughuli yeyote. James akamwuliza inawezekana kweli, au unaishi na wazazi? Doreen akamwambia hapana wazazi wangu wapo mkoa, mimi naishi pekeyangu.
Ohoo! Sasa unaishije bila kazi au unafanya biashara? Akauliza James. Doreen akamjibu sina kazi, natafuta wala biashara sifanyi.
James akamwuliza, umesomea elimu gani? Akamjibu Degree ya finance and economy. James akamwambia basi nitumie cv yako na kila kitu kwenye email yangu, akatoa business card akampa, nitakuangalizia kwa marafiki zangu ajira, tuombe Mungu. Au ulikuwa unapenda kufanya kazi sehemu gani? Doreen akajibu, sehemu yoyote inayolipa vizuri nitashukuru, asante.
Huku nyuma, Chanel, Adrienne na Carrie wakawa wanamvutia picha Doreen, wakaanza kuwaza sasa hivi atakuwa analaani sio kitoto, utadhani hajatoka kanisani. Adrienne akasema I hope that guy is nice maana mimi namashaka nae, Doreen has been through a lot katika maisha yake, wala sitataka ateseke tena in future.
May be we should text her, it’s been hours hatujamsikia, huenda kawa kidnapped, akasema chanel. Carrie akamjibu, mtu mzima anakuwaje kidnapped samahani kweupe hivi, acheni utoto, mwacheni atarudi mwenyewe. Enhe sasa usiku tunaenda kujirusha wapi? Naona tupo wa 3 am sure Doreen atarudi na kusema amechoooka anataka kulala, na hivi kesho sikukuu mimi bado nataka kutoka. Leo wapi wapendwa? Akasema carrie.
Hata sijui, akajibu Adrienne, kwanini tusikae tu ndani au leo kuna bendi inapigwa? Twanga pepeta or something!?
Yah, twendeni kwenye bendi leo, akadakia Chanel, wakakubaliana wanaenda kwenye bandi ya twanga pepeta.
Huku nyuma stori kati ya Doreen na James zimenoga, walipotoka Sheraton wakaenda cocobeach kupunga upepo wakamalizia na slipway for ice cream. Doreen Kuangalia saa mkononi mwake akakuta saa 1 usiku, akakumbuka saa 2 usiku wanatakiwa kutoka na marafiki zake, akaangalia simu akakuta missed call 20 za Adrienne. Akaomba arudishwe nyumbani na James haraka, akadanganya kuna dharura nyumbani kwangu, unaona missed calls 20 nahisi kuna tatizo nyumbani.
Kufika nyumbani, Doreen akashuka haraka huku anakimbia kutoka kwenye gari, akamwambia James asanteeeeeeeeeeeeeeeee, usiku mwemaaaaaaaaa, byeeeeeee, akamuacha James ameduwaa hata kuzima gari akashindwa. James alitegemea good night kiss and hugs, akaambulia kelele za mrembo.
ITAENDELEA