Soma hii na ujifunze

Soma hii na ujifunze

madeinmusoma

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2014
Posts
326
Reaction score
391
Baba John katoka safari zake mbio mbio na kuingia ndani kwake,kamkuta mkewe kakaa mkewe akamuuliza vipi mbona leo mapema na upo na haraka hivyo.

Mume:Akajibu jiandae tuende kwenye msiba mama kafariki.

Mkee:Heeee! mimi siwezi kwenda kwenye msiba mpaka nitengeneze nywele siwezi kwenda na nywele chafu akaondoka kaenda saloon katengeza baadae karudi na kumuuliza mumewe.

Mke:Hivi mama mkwee kwani alikuwa anaumwa nini mpaka mauti inamkuta.

Mume:Mama hajafariki nimetoka kuongea nae sasaivi

Mke:Jamani wewe si umeniambia nijiandae twende kwenye msiba mama kafarikia au.

Mume:Ndio lakini aliefariki ni mama yako.

Mwanamke akaanza kulia na kupiga kelele na akamwambia mumewe baba fanya haraka twende niwai mazishi hawatanielewa nisipo onekana mwanamume nae akamjibu subili niende kunyoa nywele siwezi kwenda na nywele za hivi.
 
Ehee hapo zinga la funzo kwa huyo mwanamke aliyeonyesha ubinafsi ulopitiliza. Pia hili ni funzo kwa watu wengine wasiojitambua.
 
Hii inaonehsa jinsi ambavyo mafunzo ya ndoa huwa ni muhimu lakini watu wanaweka masikio kwenye kipengele kimoja tu cha Afya ya Uzazi. Upendo ukitawala haya hayatokei.
 
Aiseeee yani hadi kwenye msiba unataka kujionesha?Sasa watu wana machungu yao watakua na mda wakuangalia nywele zako????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom