Soma hapa shujaa anayejificha

GHULA

Member
Mar 3, 2013
77
66
IMENICHUKUA muda kuandika andiko hili gazetini kutokana na kutokuwa nimeamini kile anachodaiwa kufanya Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kaka na rafiki yangu, Samson Mwigamba, ambaye sasa amesimamishwa uongozi.

Si kwamba siamini kwa sababu Mwigamba ni malaika hawezi kufanya makosa, la hasha! Isipokuwa nilitaka kwanza kusikia kauli yake ya utetezi wa kile kilichomtokea ili nipime kama alikuwa sahihi, alisingiziwa ama aliteleza.

Nilipigiwa simu Jumamosi iliyopita na mwanahabari mwenzangu kutoka jijini Arusha, akinieleza kuwa Mwigamba ameibua taharuki ukumbini baada ya kubainika na kukiri mbele ya kikao kuwa aliandika na kusambaza ujumbe wa uongo wa kuwadhalilisha viongozi wa kitaifa wa chama chake kwenye mtandao wa kijamii wa Jamii Forum.

Kama Yesu Kristo alivyohamaki alipobaini kuwa msaliti wake ni miongoni mwa wanafunzi wake, Yuda, nami ndivyo nilivyostuka nilipopokea taarifa ile kutokana na nilivyomfahamu Mwigamba kwa uadilifu na mapenzi kwa chama chake, hivyo sikutegemea kabisa kama anaweza kuingizwa mtego wa kucheza mchazo kama huo.


Nilijaribu kumpigia simu, lakini kwa bahati mbaya wakati huo ilionyesha inatumika kwa muda mrefu, hivyo nikaendelea kutafakari mwenyewe ni kwanini Mwigamba ajifiche wakati ana taarifa nzito kwa chama chake?

Nikajiuliza huyu ni kiongozi anayeingia kwenye vikao vikuu vya chama, ni kwanini masuala hayo hakuyahoji huko? Pili nikawaza kuwa hata kama ni kuogopa kutazamwa vibaya na wenzake au kufukuzwa, ni kwanini asingejitokeza kwenye vyombo vya habari kuanika hayo anayodhani ni bomu ndani ya chama ili wanachama wachukue hatua?

Sikupata majibu ya maswali yangu, hata baada ya kuwa nimezungumza na viongozi kadhaa wa CHADEMA hadi Jumatatu baada ya Mwigamba kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kile alichokiita “siri iliyofichika”.

Baada ya kuwa nimemsikiliza kwa makini kaka yangu Mwigamba, nilibaini kuwa utetezi wake hauna mashiko hata chembe, isipokuwa angekwenda moja kwa moja kwa kuwaomba radhi wanachama wa CHADEMA na viongozi wao kuwa aliteleza kwa kile alichokifanya.

Mwigamba alisema kuwa alilazimika kutumia njia hiyo ya kujificha ili kufikisha ujumbe kwa wahusika hatua ziweze kuchukuliwa kwani angetumia njia ya vikao kuhoji angeonekana msaliti na asingepewa nafasi.

Kwa mujibu wa Mwigamba, ndani ya CHADEMA wenye ubavu wa kuhoji au kukosoa bila kunyooshewa kidole ni Dk. Kitila Mkumbo, Prof. Mwesiga Baregu na Mzee Shilungushela, kwamba wengine wanaonekana wasaliti.

Yawezekana kaka yangu Mwigamba alikuwa na hoja na tuhuma za kweli, lakini njia aliyotumia si sahihi. Neno moja ninaloweza kumshauri kaka yangu ni hili la kwamba; “Shujaa haogopi vita”, anakaa mstari wa mbele, yuko tayari kwa lolote hata kukosana na marafiki zake na hata kupoteza maisha, lakini historia inaandikwa kwake.

Napata shaka kuona kiongozi kama Mwigamba hawezi kuhoji ufisadi wa chama anachodai anakipenda ndani ya vikao, eti anaogopa kuitwa msaliti. Lakini shaka zaidi ni kuona alituma andiko hilo hilo kwenye mitandao baada ya kuwasilisha taarifa ya utendaji wa chama mkoa na kutoa sifa lukuki kwa wake anaogeuka sasa kutwambia ni maadui zake.

Mwanafalsafa wa Kijerumani na mtaalamu wa maadili, Emmanuel Kant, anaamini kuwa ‘The end does not justify the meas’, yaani matokeo hayahalalishi njia uliyotumia.

Kant anasema kuwa unaweza kufanya jambo kwa nia njema, lakini matokeo yake yakawa mabaya na yenye madhara.

Hivi ndivyo alivyofanya Mwigamba. Licha ya kupata nafasi ya kukutana na viongozi wakuu wa chama na hivyo kuwa na uwezo wa kueleza madukuduku yake, hakufanya hivyo bali alisubiri kutumia njia ya kujificha kufanya alivyofanya na baadaye alipogundulika ndipo akafichua kwamba ana uadui na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Kwa mtazamo wangu, kaka yangu Mwigamba, hakuitendea haki CHADEMA, viongozi wake wala wafuasi wake, kwani hata kama hayo aliyoyaandika yana ukweli asilimia 100, kama mwanachama mtiifu, alipaswa kutumia njia sahihi bila kujificha ili kueleza hatua zichukuliwe.

Hawa viongozi wa CHADEMA si malaika, wanaweza kufanya makosa, lakini mtoa tuhuma si shujaa, ana hofu ya kuitwa msaliti na kuonekana mbaya kwa viongozi. Lakini kama nilivyoeleza awali sifa za shujaa kuwa hapaswi kuhofia chochote ilmradi tu anasimamia na kutetea ukweli kwa maslahi ya wengi.
 
GHULA, unahangaika sana kukitetea chama kinachoongozwa na viongozi waongo, wanafiki na wazandiki. Mwigamba yupo sahihi na tuhuma alizotoa ni za kweli
 
Tumshukuru Mwigamba kwa kuibua hoja zile maana wengi tusingejua kuwa katiba ya CHADEMA imechakachuliwa au chama hakina akaunti yenye fedha hata moja
 
Mwigamba pia ametusaidia kujua kuwa Dr Slaa na Mnyika ni waongo na hawana uelewa juu ya Katiba yao
 
ujumbe mzuri sana kwenda kwa kamanda mwigamba,mwalimu mzoefu na mwadishi mzuri sana ila kupotoka kwake kumempa funzo na kujua kuwa kila mwanachama ndani ya cdm anamwangalia mwenzake,kuanzia anapoamka asbh,anaongea na nani nanakutana na nani,ndiyo maana kwenye cm yake pia kumekutwa msg alizokuwa anawasiliana na mamlaka ya juu ili kutimiza malengo yake,tuna vita kubwa sana ndani yetu,kikubwa tuwe makini tu mda wote.

kutenda kosa sio kosa ila kurudia kosa ndiyo kosa,mie kwa roho safi namsamehe bure,hukumu zetu ziko juu ya mbingu who am i to judge him?

mungu akuongozi utimize wajibu wako wa kila siku na kusudio lako ndani ya chama na nje ya chama
 
ndani ya CHADEMA wenye ubavu wa kuhoji au kukosoa bila kunyooshewa kidole ni Dk. Kitila Mkumbo, Prof. Mwesiga Baregu na Mzee Shilungushela, kwamba wengine wanaonekana wasaliti.
Kama aliona hoja yake ni ya msingi na yeye hatasikilizwa alishidwa vipi kuwaona hao unaowataja kwamba wanasikilizwa ili walifikishe jambo hili mbele ya vikao halali vya chama?.
 
ujumbe mzuri sana kwenda kwa kamanda mwigamba,mwalimu mzoefu na mwadishi mzuri sana ila kupotoka kwake kumempa funzo na kujua kuwa kila mwanachama ndani ya cdm anamwangalia mwenzake,kuanzia anapoamka asbh,anaongea na nani nanakutana na nani,ndiyo maana kwenye cm yake pia kumekutwa msg alizokuwa anawasiliana na mamlaka ya juu ili kutimiza malengo yake,tuna vita kubwa sana ndani yetu,kikubwa tuwe makini tu mda wote.

kutenda kosa sio kosa ila kurudia kosa ndiyo kosa,mie kwa roho safi namsamehe bure,hukumu zetu ziko juu ya mbingu who am i to judge him?

mungu akuongozi utimize wajibu wako wa kila siku na kusudio lako ndani ya chama na nje ya chama

Ulipaswa pia kumpongeza kwa yale aliyoeleza
 
Tumshukuru Mwigamba kwa kuibua hoja zile maana wengi tusingejua kuwa katiba ya CHADEMA imechakachuliwa au chama hakina akaunti yenye fedha hata moja

Wewe chaburma"
unatoa ushahidi kama nani ndani ya chadema?

Kama mleta thread alipoashiria kuwa mwigamba ni mkosaji asingetakiwa kuandika ile habari kwa siri,na baadae kwenye vyombo vya habari.
Hii sio sahihi maana yeye ni kiongozi chadema,Angewakilisha huko bila matatizo,
 
Mwigamba ni chui ndani ya ngozi ya kondoo. Kwa aliyoyafanya hastahili kuwa mwana CDM hata akiomba msamaha. Ni msaliti kama akina Mtela et al. Aende zake kwa mabwana wanaomtumia - ccm kwa maana kazi waliyomtuma ametekeleza.
Na bado, wako mamluki wengi ndani ya CDM
 
Kusimama mbele ya kundi la watoa roho na kuwaambia ukweli ni ushujaa wa hali ya juu.

Mwigamba ana roho saba kama paka, hafi mara moja.....
 
Hivi na wewe hili ndio jina lako halisi? Wacha uoga na wewe jitambulishe Mwigamba akutambuwe ajuwe ni rafiki yangu fulani ananipa makavu, otherwise tofauti ya wewe na Mwigamba ni ndogo sana.
Mkuu, hawa jamaa wanachekesha sana. Nilitegemea hoja kama hizi ziandikwe na mtu ambaye anatumia jina lake halisi. Isije ikawa huyu ndo Godbless Lema na anaandika haya kupindisha hoja za Mwigamba
 
Kusimama mbele ya kundi la watoa roho na kuwaambia ukweli ni ushujaa wa hali ya juu.

Mwigamba ana roho saba kama paka, hafi mara moja.....
Mkuu, unanikumbusha ya Zitto Kabwe alivyomwandikia personal letter Katibu Mkuu, Dr Slaa kuomba ufanyike uchunguzi wa ndani dhidi ya Lwakatare baada ya kukumbwa na kashfa ya kupanga njama za kumdhuru Mwandishi Dennis Msacky barua ambayo ilikuja kutundikwa humu JF na Ofisi ya Dr Slaa. Wengi tulijiuliza sana iweje Naibu Katibu Mkuu amwandikie Katibu Mkuu barua binafsi? Kuna waliomwandama Zitto na kumwona msaliti. Ila tukio la Mwigamba limetufumbua kuwa kuna tatizo la kimawasiliano ndani ya CHADEMA baina ya viongozi kwa viongozi au wanachama kwa viongozi
 
Mwigamba ni chui ndani ya ngozi ya kondoo. Kwa aliyoyafanya hastahili kuwa mwana CDM hata akiomba msamaha. Ni msaliti kama akina Mtela et al. Aende zake kwa mabwana wanaomtumia - ccm kwa maana kazi waliyomtuma ametekeleza.
Na bado, wako mamluki wengi ndani ya CDM
Wewe mwite tu kwa majina yote mabaya lakni hiyo haitasaidia kuondoa uongo wa Dr Slaa
 
IMENICHUKUA muda kuandika andiko hili gazetini kutokana na kutokuwa nimeamini kile anachodaiwa kufanya Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kaka na rafiki yangu, Samson Mwigamba, ambaye sasa amesimamishwa uongozi.

Si kwamba siamini kwa sababu Mwigamba ni malaika hawezi kufanya makosa, la hasha! Isipokuwa nilitaka kwanza kusikia kauli yake ya utetezi wa kile kilichomtokea ili nipime kama alikuwa sahihi, alisingiziwa ama aliteleza.
Nilipigiwa simu Jumamosi iliyopita na mwanahabari mwenzangu kutoka jijini Arusha, akinieleza kuwa Mwigamba ameibua taharuki ukumbini baada ya kubainika na kukiri mbele ya kikao kuwa aliandika na kusambaza ujumbe wa uongo wa kuwadhalilisha viongozi wa kitaifa wa chama chake kwenye mtandao wa kijamii wa Jamii Forum.

Kama Yesu Kristo alivyohamaki alipobaini kuwa msaliti wake ni miongoni mwa wanafunzi wake, Yuda, nami ndivyo nilivyostuka nilipopokea taarifa ile kutokana na nilivyomfahamu Mwigamba kwa uadilifu na mapenzi kwa chama chake, hivyo sikutegemea kabisa kama anaweza kuingizwa mtego wa kucheza mchazo kama huo.

Nilijaribu kumpigia simu, lakini kwa bahati mbaya wakati huo ilionyesha inatumika kwa muda mrefu, hivyo nikaendelea kutafakari mwenyewe ni kwanini Mwigamba ajifiche wakati ana taarifa nzito kwa chama chake?
Nikajiuliza huyu ni kiongozi anayeingia kwenye vikao vikuu vya chama, ni kwanini masuala hayo hakuyahoji huko? Pili nikawaza kuwa hata kama ni kuogopa kutazamwa vibaya na wenzake au kufukuzwa, ni kwanini asingejitokeza kwenye vyombo vya habari kuanika hayo anayodhani ni bomu ndani ya chama ili wanachama wachukue hatua?

Sikupata majibu ya maswali yangu, hata baada ya kuwa nimezungumza na viongozi kadhaa wa CHADEMA hadi Jumatatu baada ya Mwigamba kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza kile alichokiita “siri iliyofichika”.
Baada ya kuwa nimemsikiliza kwa makini kaka yangu Mwigamba, nilibaini kuwa utetezi wake hauna mashiko hata chembe, isipokuwa angekwenda moja kwa moja kwa kuwaomba radhi wanachama wa CHADEMA na viongozi wao kuwa aliteleza kwa kile alichokifanya.
Mwigamba alisema kuwa alilazimika kutumia njia hiyo ya kujificha ili kufikisha ujumbe kwa wahusika hatua ziweze kuchukuliwa kwani angetumia njia ya vikao kuhoji angeonekana msaliti na asingepewa nafasi.

Kwa mujibu wa Mwigamba, ndani ya CHADEMA wenye ubavu wa kuhoji au kukosoa bila kunyooshewa kidole ni Dk. Kitila Mkumbo, Prof. Mwesiga Baregu na Mzee Shilungushela, kwamba wengine wanaonekana wasaliti.
Yawezekana kaka yangu Mwigamba alikuwa na hoja na tuhuma za kweli, lakini njia aliyotumia si sahihi. Neno moja ninaloweza kumshauri kaka yangu ni hili la kwamba; “Shujaa haogopi vita”, anakaa mstari wa mbele, yuko tayari kwa lolote hata kukosana na marafiki zake na hata kupoteza maisha, lakini historia inaandikwa kwake.
Napata shaka kuona kiongozi kama Mwigamba hawezi kuhoji ufisadi wa chama anachodai anakipenda ndani ya vikao, eti anaogopa kuitwa msaliti. Lakini shaka zaidi ni kuona alituma andiko hilo hilo kwenye mitandao baada ya kuwasilisha taarifa ya utendaji wa chama mkoa na kutoa sifa lukuki kwa wake anaogeuka sasa kutwambia ni maadui zake.

Mwanafalsafa wa Kijerumani na mtaalamu wa maadili, Emmanuel Kant, anaamini kuwa ‘The end does not justify the meas’, yaani matokeo hayahalalishi njia uliyotumia.
Kant anasema kuwa unaweza kufanya jambo kwa nia njema, lakini matokeo yake yakawa mabaya na yenye madhara.
Hivi ndivyo alivyofanya Mwigamba. Licha ya kupata nafasi ya kukutana na viongozi wakuu wa chama na hivyo kuwa na uwezo wa kueleza madukuduku yake, hakufanya hivyo bali alisubiri kutumia njia ya kujificha kufanya alivyofanya na baadaye alipogundulika ndipo akafichua kwamba ana uadui na mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Kwa mtazamo wangu, kaka yangu Mwigamba, hakuitendea haki CHADEMA, viongozi wake wala wafuasi wake, kwani hata kama hayo aliyoyaandika yana ukweli asilimia 100, kama mwanachama mtiifu, alipaswa kutumia njia sahihi bila kujificha ili kueleza hatua zichukuliwe.
Hawa viongozi wa CHADEMA si malaika, wanaweza kufanya makosa, lakini mtoa tuhuma si shujaa, ana hofu ya kuitwa msaliti na kuonekana mbaya kwa viongozi. Lakini kama nilivyoeleza awali sifa za shujaa kuwa hapaswi kuhofia chochote ilmradi tu anasimamia na kutetea ukweli kwa maslahi ya wengi.


Nilieleza hili kwenye thread moja niliyojibu humu.Mwandishi wa makala hii nskubaliana na mtazamo na hoja yake hii.
 
Mkuu, unanikumbusha ya Zitto Kabwe alivyomwandikia personal letter Katibu Mkuu, Dr Slaa kuomba ufanyike uchunguzi wa ndani dhidi ya Lwakatare baada ya kukumbwa na kashfa ya kupanga njama za kumdhuru Mwandishi Dennis Msacky barua ambayo ilikuja kutundikwa humu JF na Ofisi ya Dr Slaa. Wengi tulijiuliza sana iweje Naibu Katibu Mkuu amwandikie Katibu Mkuu barua binafsi? Kuna waliomwandama Zitto na kumwona msaliti. Ila tukio la Mwigamba limetufumbua kuwa kuna tatizo la kimawasiliano ndani ya CHADEMA baina ya viongozi kwa viongozi au wanachama kwa viongozi

Thibitisha kama barua iliyovuja huku ilitoka kwenye ofisi ya katibu mkuu.Hili lilishajibiwa humu mkaambiwa mlete vielelezo kuwa barua hiyo ilitumwa kwa mkono au kwa njia ipi.Hamkuleta mnapiga majungu tu
 
Wewe chaburma"
unatoa ushahidi kama nani ndani ya chadema?

Kama mleta thread alipoashiria kuwa mwigamba ni mkosaji asingetakiwa kuandika ile habari kwa siri,na baadae kwenye vyombo vya habari.
Hii sio sahihi maana yeye ni kiongozi chadema,Angewakilisha huko bila matatizo,

Mleta mada naye ni mnafiki kama ulivyo wewe. Mbona na yeye anatumia ID Fake?
 
Mkuu, hawa jamaa wanachekesha sana. Nilitegemea hoja kama hizi ziandikwe na mtu ambaye anatumia jina lake halisi. Isije ikawa huyu ndo Godbless Lema na anaandika haya kupindisha hoja za Mwigamba

Mimi siamini katika Kuhisi, nimeambiwa, nimeambiwa, nimeambiwa, nimeambiwa, nimeambiwa! No I only base on fact.
 
Back
Top Bottom