solar power business..

frangerry

Member
Mar 9, 2012
7
1
wanabodi,
nimekuwa nikifikiria juu ya kuanzisha biashara ya kuuza vifaa, ku-install systems na kufanya maintenance ya solar power systems kwa muda sasa.
naomba msaada wa kimawazo na taarifa juu ya upatikanaji wa vifaa,na taratibu za kisheria za kufuata
pia kama kuna watu walio kwenye biashara hii (wakubwa) tayari wanaweza kupata mteja,pia kwa walio nje wanaweza niunganisha na source za huko pia.

karibuni kwa ushauri
 
Kwanza jiulize:
  • Je, una ufahamu wa masuala hayo ya umeme-jua? Aina fulani ya utaalamu ni muhimu
  • Je, una mpango mkakati (strategic plan) wa nini unataka kufanya?
  • Umefanya utafiti kuhusu soko (market survey)? Hapa utasaidika katika kuamua unatarajia kuhusika na wateja wa aina gani (wakubwa, wa kati au wadogo) na pricing mechanism.
Kwa enzi hizi za utandawazi upatikanaji wa mali sio tatizo kubwa, inategema na namna gani wewe umejipanga kwani tofauti kati ya wazalishaji zipo katika ubora, bei n.k.

Senti zangu hamsini!
 
Kwanza jiulize:
  • Je, una ufahamu wa masuala hayo ya umeme-jua? Aina fulani ya utaalamu ni muhimu
  • Je, una mpango mkakati (strategic plan) wa nini unataka kufanya?
  • Umefanya utafiti kuhusu soko (market survey)? Hapa utasaidika katika kuamua unatarajia kuhusika na wateja wa aina gani (wakubwa, wa kati au wadogo) na pricing mechanism.
Kwa enzi hizi za utandawazi upatikanaji wa mali sio tatizo kubwa, inategema na namna gani wewe umejipanga kwani tofauti kati ya wazalishaji zipo katika ubora, bei n.k.

Senti zangu hamsini!

Thanks much mkuu,
Kwa ufupi ninaknowledge ya solar power kwa kiasi kinachofaa.
Market survey nimefanya kwa level ya wateja wadogo,namaanisha vijijini na wilayani,kwa watu binafsi pia kwa serikali za wilayani,covering zahanatiz ,schools na mengineyo.so target ni wateja wadogo kwa kuanzia.
Na linaridhisha kuingiza bidhaa sokoni.
Naamin tutasaidiana kwa ushauri zaidi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom