Soko la matikiti

Soko la matikiti

KAPURO

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2016
Posts
235
Reaction score
153
Natumaini wazima wa afya, Nilikuwa mkimya kitambo kidogo nilikuwa shambani kwenye field baada ya kusoma maandiko mengi na sasa nategemea kuvuna matikiti tarehe 5 mwezi wa Tisa.
Tafadhali kama kuna MTU anajua hali ya soko la Dar anijuze, Pia kama kuna MTU anamtandao na wasambazaji kwa njia ya tenda naomba pia anijuze Namba Yangu ni 0753359245. Niko Mlandizi Kibaha.
Asanteni sana.
 
Habari nzuri sana. Wanakuja wajuzi wakupe mchanganuo
 
Mkuu mimi nikushauri utafute mteja uuzie mzigo wako shambani. Unaweza kuuza kwa gari Kwa mfano Fuso single diff sh milioni 2.5 mpaka 3 kutegemeana na ukubwa wa tikiti zako. Canter may be kwa 2 milion nk, we nenda buguruni sokoni pale ongea na madalali wa tikiti wata kuunganisha na wateja.
Ukisema upeleke mzigo sokoni utaingia cost za usafirishaji, ushuru wa soko, gharama za wapakiaji, washushaji na bado unaweza kuta soko limejaa. Kama usipopata mteja na tikiti zinazidi kukomaa basi hapo vuna peleka sokoni kama hatua ya mwisho.
 
Back
Top Bottom