Social Networking/Mitandao ya ki-Jamii...


...la la la,....πŸ™‚

...binafsi Facebook na hii mitandao ya kijamii imeniwezesha kunikutanisha tena na watu weeengi niliokuwa nimesoma nao, nimeishi nao na hata wale ex-gelo frendz niliojirusha nao miaka hiyooooo....

...kimbembe ni jinsi gani ya ku handle hizo rekindled flames bana japo tayari wengi wetu tushakuwa na minyama uzembe, lakini si unajua tena....mnaanza na "..hivi nimekumisije?" au "...hivi kwanini ulinichunia!?"...kisha mnaendelea "...bado nakumbukia maujuzi yako, bado upo vile vile....?! " ----kufumba na kufumbua mshabadilishana namba za simu na na ahadi za kupeana 'what you've been missing all those years!"

Balaaa!
 
Hizo options zinamisi 2 important ones, 'unstable' na 'unpredictable'
Hii mitandao hai-respond to clientele needs kabisa! Afadhali maxence hajaweka hii option ya marital status humu jf, kila mtu angekuwa single tena yenye bold,lol

...dahhh, umegusa patamu sana;

umegusia kama vile watu hawaelewi lengo, nia na madhumuni ya kujiunga kwenye hii mitandao ya kijamii ni tofauti na jinsi wanavyotumia uhuru wao wa maoni na uchangiaji, ndivyo sivyo?
...


....biashara matangazo, wewe huoni wengine wanavyopiga picha za mapozi ya mvuto wa kufa mtu japo ni mke/mume wa mtu?



...huu mfano kama kale katabia ka kudokoa nyama jikoni umenifurahisha sana.
 
Kulinda mahusiano yangu kuna mitandao nilishaachana nayo kabisa nisije nikaingia majaribuni. Lol.
Mbu, hii thread imenifanya nimfikirie mara mbili mbili rafiki yangu, ana mpenzi wake(ambae anamuita mume mtarajiwa) kila kukicha ana kazi ya kuweka picha mpya facebook tena nyingi akiwa kifua wazi. Wadada nao wanacomment kumwambia ana kifua kizuri. Rafiki yangu hapendi na kashamwambia jamaa ila hasikii.
Mdada naona anakufa na tai shingoni.
 
Reactions: Mbu
Duh, umeongea kwa hisia.
Hadi umenitisha hata kuwa hapa jf
ukiachia mbali fb ambapo napaogopa siku zote
sijui nilog off for good?!!

Mbona mi naona nimeongea kawaida tu!

Mimi naona niliyoyaongea ni mambo halisi yanayotokea katika dunia ya leo. Au wewe unaona ni mambo ya kufikirika zaidi?
 

...hahaha...ndipo tulipo na huko tunakoelekea sijui kutazuka balaa gani yarabi,
heri yao kina mzee DC miaka yao kulikuwa na Autograph tu za kusaini kisha unamrudishia

mwenyewe...
 
Analike akionesha amekusoma, amependa ulichoandika au anakufatilia.
 
watu wana-subscribe kwenye hii mitandao ya kijamii kwa malengo tofauti: kupashana habari, kujenga urafiki, kuinter-act na professionals wenzetu, kufuatilia watu na matukio etc; unfortunately, mitandao yenyewe iko so much open-ended kiasi kwamba huna au una control kidogo sana kuhusu yale unayo-upload; pia watu tuna-tend kujisahau sana na kujiachia as if nobody else is watching - nadhani ni muhimu kujiwekea mipaka on how far we can go with the flow hasa kwenye mambo ya mapenzi, flirting etc kabla wengi wetu hatujaumbuka
 
Reactions: Mbu
Facebook noma kule,unaweza ukafa na presha tena kama couples,ndo mambo ya kulazimishana 2andike married to...au in a relationship with...,2pige picha kila mtu ajue wewe wangu.Kifupi facebuk ina disadvantages nyingi sana.
 
Reactions: Mbu
Facebook noma kule,unaweza ukafa na presha tena kama couples,ndo mambo ya kulazimishana 2andike married to...au in a relationship with...,2pige picha kila mtu ajue wewe wangu.Kifupi facebuk ina disadvantages nyingi sana.

...hahahaha, wengine wanataka kumjua mwenza wajue jinsi ya kujipanga likilipuka.

Tukiangalia upande wa faida twaweza jikuta unausoma na kuujua udhaifu wa mwenzako pitia facebook...
picha anazoweka, comments zake kutokana na moods, marafiki zake wapya na wazamani,....nk
 

Labda inabidi watu wawekeane sheri kabisa kuhusiana na hii mitandao.
1. Hamna kuweka picha zinazoreaveal sana.
2. Hamna kuupdate ulimwengu kuhusu mahusiano yalipo/yanapoelekea (leo complicated, kesho vile, status za leo "he/she is the best, kesho kaniboa".
3. Hamna kuadd Xs (kama mmoja anaona italeta matatizo).
4. Hamna kiandika status zinahusiana na mambo ya ndani (sex, financia issues, mipango n.k)
5. Kila mmoja anakua rafiki wa mwenzie.
6. . . . . . . . .
 
Reactions: Mbu

aaaaarrrggghh? Lizzy masharti gani hayo sasa? hahahaha....
hivi kuna ubaya gani kumu add ex kwa facebook au hizi social networks?
au utajuaje huyu ni ex wake, au huyu ana fling & flirt kwa sana?

...yaani relationship na mtu ndio mnakabana kabana namna hii? hahahaha
 
facebook

1.vijimama na serengeti
2.vizee na visichana
3.vijana kwa vijana
4.wote mnachanganyana.
vigezo picha ziwe photoshop au umepiga maeneo ya ukweli,au umezipiga kule majuu,mbona kitaeleweka tu kirahisi
 
...Halafu Lizzy umenikumbusha kitu, kuna watu kila siku wanaweka updates zao tangu wanaamka, wanachokula, wanapokwenda,
na mapicha yao ya kila siku, .....akipotea siku moja, siku ya pili anahadithia alipopotelea jana....!

...hivi tafsiri ya siri ya mambo ya ndani ni nini vile?
 
facebook

1.vijimama na serengeti
2.vizee na visichana
3.vijana kwa vijana
4.wote mnachanganyana.
vigezo picha ziwe photoshop au umepiga maeneo ya ukweli,au umezipiga kule majuu,mbona kitaeleweka tu kirahisi

...hahaha, jina halijengwi kwa ubao kaka,
linajengwa kwa pesa, ujiko au maskendeli!

watu wamegundua facebook, kama njia nyepesi ya kujijengea jina
ndio maana
Twitter bado ina washabiki wachache...
 
ni ukweli
na inatisha
ndo maana natamani kulof off fo good!

Mbona mi naona nimeongea kawaida tu!

Mimi naona niliyoyaongea ni mambo halisi yanayotokea katika dunia ya leo. Au wewe unaona ni mambo ya kufikirika zaidi?
 
...Mkuu Mbu kama humjui ex basi imekula kwako hahahahah lol! mawasiliano ya karibu kabisa kwa raha zao πŸ™‚πŸ™‚...Kama unamfahamu basi hastahili kabisa kuwepo katika page ya mke/mume vinginevyo ndio mwanzo wa varangati ndani ya nyumba.

 
Last edited by a moderator:
...Mkuu Mbu kama humjui ex basi imekula kwako hahahahah lol! mawasiliano ya karibu kabisa kwa raha zao πŸ™‚πŸ™‚...Kama unamfahamu basi hastahili kabisa kuwepo katika page ya mke/mume vinginevyo ndio mwanzo wa varangati ndani ya nyumba.

..hah? kiongozi hivi kuna umuhimu kumjua sijui kumfahamu ex wa mke/mume?
sasa wale one night stand utawa block vipi nao? nao wamo hao...
 

...hahaha, jina halijengwi kwa ubao kaka,
linajengwa kwa pesa, ujiko au maskendeli!

watu wamegundua facebook, kama njia nyepesi ya kujijengea jina
ndio maana
Twitter bado ina washabiki wachache...
twitter hata matumizi yake magumu.
facebook unakuwa na friends 5000 na zingine pendings yaani unafans sawa na msanii mwenye jina tz
 
Reactions: Mbu
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…