Slaa ataja sababu za CCM kung’ang’ania madaraka

unatumia kichwa kufugia nywele, halafu unakunywa gongo kuliko kawaida ndio mana ubongo umeharibika. na utabaki hivyo hivyo nyamafu wewe.watakutumia kama ile mipira mpaka uje ushtuke una mvi kama za babu yako halafu huna kitu. mjinga wewe

Kwa taarifa yako mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa Tz kama unavyodhania,ila ni mpiga kura na nimuhanga wa utawala haramu wa chama tawala.
 
Hii PICHA NI YA MWAKA 2010 WAKATI wa uchaguzi mkuu.



changia mada ndg picha ci muhimu sana.changia kama alichosema ni kweli ama si kweli,picha inaweza kuwa ya maktaba lakn ujumbe uliolengwa ukafika.usitawaliwe na miemko ya upenzi wa mtu bali hoja ya msingi.
 
DR SLAA NDIYO TEGEMEO LA WATANZANIA ,tunakushukuru baba , mungu akulinde sana mkuu .
 
Hii PICHA NI YA MWAKA 2010 WAKATI wa uchaguzi mkuu. mleta mada anajaribu kuuhadaa umma

Tusiandikie mate na wino ungalipo! right click hapo kwenye image halafu click view image info halafu click general ,halafu uje uthibitishe kauli yako.
 
tuko makini sana mkuu na huu uongo wa hawa walevi wa gongo. wanatumia picha za matukio ya mwaka 2010 kumpamba slaa baada ya kuona anadoda katika mikutano yake.


Tusiandikie mate , kama unatumia computer right click hapo kwenye image halafu click view image info halafu click general halafu njoo mthibitishe kama image hii si ya mwaka 2013
 
tatizo lenu ni picha au ujumbe?mbona mandela alivyofariki amkutaka iwekwe picha ya wakati ana miaka 95?yaani ccm mpo kishabiki sana mpaka tuna hoji vichwa vyenu mnatumia kufikiri au kufugia nywele
we ulikuwa na nia gani kuweka picha hii? ulikuwa na maana ya kuuaminisha umma kuwa alijaza watu kiasi hicho. Kwanini usiweke picha ya siku hiyo? Sasa watu wakisema ukweli unasema watu wana ushabiki, kwani wewe kilichokusukuma kufanya hivyo si ushabiki huohuo? Kwanini wana chadema mkifanya jambo basi zuri ila akifanya mwingine basi ni mbaya? Acheni ubinafsi uliopita kiasi... ( sina chama mimi)
 
tatizo lenu ni picha au ujumbe?mbona mandela alivyofariki amkutaka iwekwe picha ya wakati ana miaka 95?yaani ccm mpo kishabiki sana mpaka tuna hoji vichwa vyenu mnatumia kufikiri au kufugia nywele

Hawa ni watu wa ajabu kabisa,wao ni kuchunga tu vitumbua vyao.,Wao badala ya kijadili kilichoongewa wao wapo mara Chadema,mara Mbowe,Ooh Slaa kimepanda kimeshuka.,Yaani wao ni kutoa mashuzi tu."wanachusha" na kushusha hadhi ya jamwvi.
 
Shule anayotoa Dr. Slaa italisaidia sana Taifa hili na vizazi vyake kwa miaka 100 ijayo.

Huyu ndiye kiongozi na mwanasiasa pekee kwa takriban miaka 30 iliyopita ambaye ana kipaji, uwezo, ushawishi na nia ya dhati ya kulitumikia hili Taifa na hasa kututoa hapa tulikozama.

Kwa vigezo vya utendaji, uwezo na ushawishi; Dr. Slaa yuko ktk kwenye mabano sawa pamoja (same bracket) na hayati Mwl. Nyerere na Edward M. Sokoine.

Nazidi kuijutia na kuomboleza kwa ajili ya nchi yangu Tanzania hasa ile nafasi Watanzania tuliypoteza 2010; laiti angekuwa yuko Magogoni muda huu tusingekuwa jamvi la wageni huko kwenye madini, gesi, utalii, kilimo, elimu nk
 
Sababu za CCM kung'ang'ania madaraka ndio hiyo hiyo anayoitumia Mbowe kung'ang'ania madaraka ya uenyekiti
 
Kwa kawaida chama cha siasa huibukia pabovu pa chama kingine. chama kikiharibu mahali fulani ni pointi ya kuondokea chama kinzani.
sasa chadema kinaibukia kwenye tatizo la ufisadi, wizi na udhaifu mwingine ambavyo vina athari kubwa kwa taifa. baadhi ya watu wanaibukia tabia binafsi za mtu hii ni weakness! maana ni rahisi tu kumwondoa mtu na malengo ya taasisi yakabaki palepale. mfano kushobokea jambo la kuhalalisha gongo au mtu kuwa na mpenzi mahali. Lets talk about national issues: poverty, ideology and vision, education, healthy, security and things like these. kama watu wanakunywa gongo yenye sumu kwa sasa inaonekana sawa lakini ikifikiriwa baadaye wanywe isiyo na sumu inakuwa issue ni tatizo! haya, watu wanaongelea mambo ya picha ambayo naamini haiathiri kile tunachokifahamu it becomes also a weakness!
 
Dokta amezungumzia jambo la chama kung'ang'ania madaraka kwa sababu ya kuhofia hatima yake. hili ni jambo la wazi kabisa kila mahali na hata katika taasisi zote. labda tungejadili kama hili lipo kweli. niliwahi sema humu kuwa wanaohofia ccm koundoka madarakani si vionguzi pekee bali wote wanaonufaika na kuwepo kwa ccm wote, wote kabisa! mfano kama kuna udhaifu watukapata fursa ya kufanya uhalifu unadhani hao wahalifu watapenda ccm itoke? wako wauzaji unga, wala rushwa, wala magendo, wanaopendeleana kwa vyeo, wezi n.k. wote hawa watatetea mfumo uliopo. wapo ambao hawana makosa lakini wamenufaika na ccm hao ni kama watoto wa vigogo, wake zao, jamaa na marafiki wa viongozi wa ccm. wote hao watapinga na hata kutukana vyama kama cdm. hawatapenda ccm itoke. wataogopa hatma yao! wapo viongozi walioshidwa kufanya mazuri ni lazima waogope hata dalili tu za kuja serikali mpya. huo ndio msingi wa hoja ya Slaa, Waliokosa hoja wanakuja na mambo ya gongo na picha shame!
 
CCM Wanag'ang'ania madarakani kwa kuwa wanajua iko sikuwa wananchi watahoji Almasi, Dhahabu, Nickel, Rubby, Tanzanite, Granite, Uranium zimewasaidia vipi? wananchi watahoji ardhi yao kwanini imeuzwa, wanajua kuwa iko siku wananchi watahoji Tembo, Twiga wameishia wapi? Wananchi watahoji yale Mabilioni kwa matrilioni zinamilikiwa na akina nani na zimetokana na nini?... Migodi ya Nyamongo, Geita, Kahama, Mwadui, Nzega, Kiwira zimetunufaisha vipi? Kwanin huduma ya afya, maji safi na salama hakuna wakati sisi ni matajiri? Kwanini watoto wetu hawapatiwi elimu bora? kwanini wafanyakazi wanahadaiwa? Kwanini wageni ndo hawalipi kodi ilhali wananchi wanakamuliwa kodi?... CCM wanajua kuwa wakiachia madaraka kamwe hawatakuwa salama...
 
Ccm ilishinda uchaguzi kwa asilimia kubwa kuanzia udiwani,ubunge mpaka uraisi hili la kung'ang'ania limetoka wapi? Slaa usitufanye watanzania wote ni mabozongo kama umefilisika kisiasa kaa pembeni unywe gongo na nduguzo
 
Back
Top Bottom