Siuji kwanini iko hivi

Siuji kwanini iko hivi

Habari zenu wana jamvi,

Kwanini inakua ngumu hawa watu kukutana? Mr right kumpata miss right inaonekana ni kama ndoto vile. Kinachonishangaza hawa wote wako kwenye jamii lkn hawaonani.

Tujadili.
Mie nadhani Mr/Mrs Right ni wapenzi ambao wameunganishwa na mapenzi ya kweli! mapenzi ya kweli ni yale ambayo wawili hawa wamejua mapungufu ya kila mmoja wao na kujua jinsi ya kuishi nayo! Mr/Mrs Right wanavumiliana na wanaelewana.
Mr/Mrs Right hawakutani tu baa, disco, shopping malls au kwenye Cinema Mr
and Mrs Right wametengenezana kutokana na muda waliokuwa pamoja, Mr/Mrs Right ni zaidi ya wapenzi ni marafiki waaminifu na wanaojua maana ya kuwa na rafiki na urafiki wa kweli.
Ukiwaona Mr/Mrs Right Jua kuna mengi magumu wamepitia na kukwepa vizingiti vingi.
 
wenye mapenzi ya kweli wamekua adimu sana
wengi wanaigiza (i hate this)
wanangoja perfect timings za kuumiza wenzio wao kwa kisingizio cha ''ubinadamu''
ni kumuomba Mungu tu,akupe mtu sahihi
kwa juhudi za mtu binafsi mwisho ni kukata tamaa tu na kujiandaa kwa visasi hata kwa ambao hawakukukosea
 
Hawa wapo katika jamii na wanaweza kukutana tatizo ni moja kuchukuliana na kukubali kuwa unamapungufu na mwenzako ana mapungufu kwa hiyo ni lazima kukubali kuendana nayo ili kila mmoja afurahie kuwa na mwenzake,tatizo kila mu anataka aonekane yeye ndo zaidi ya mwenzake.
 
wenye mapenzi ya kweli wamekua adimu sana
wengi wanaigiza (i hate this)
wanangoja perfect timings za kuumiza wenzio wao kwa kisingizio cha ''ubinadamu''
ni kumuomba Mungu tu,akupe mtu sahihi
kwa juhudi za mtu binafsi mwisho ni kukata tamaa tu na kujiandaa kwa visasi hata kwa ambao hawakukukosea
Nimeupenda mchango wako, ni kweli kabisa hasa hapo kwenye red ndio jibu sahihi pasipo kumuomba Bwana inakua bahati nasibu kumpata mr/mrs right maana alishasema wazi kwamba fedha na dhahabu waweza pewa na mwanadamu lkn mwenza mwema ni kazi yake kukutafutia. Kumbe jambo la msingi ni kujenga personal relationship na Muumba.
 
Mie nadhani Mr/Mrs Right ni wapenzi ambao wameunganishwa na mapenzi ya kweli! mapenzi ya kweli ni yale ambayo wawili hawa wamejua mapungufu ya kila mmoja wao na kujua jinsi ya kuishi nayo! Mr/Mrs Right wanavumiliana na wanaelewana.
Mr/Mrs Right hawakutani tu baa, disco, shopping malls au kwenye Cinema Mr
and Mrs Right wametengenezana kutokana na muda waliokuwa pamoja, Mr/Mrs Right ni zaidi ya wapenzi ni marafiki waaminifu na wanaojua maana ya kuwa na rafiki na urafiki wa kweli.
Ukiwaona Mr/Mrs Right Jua kuna mengi magumu wamepitia na kukwepa vizingiti vingi.
Mkuu kuna ukweli ktk hili isipokua hapo kwenye blue sidhani kama kila wakati iko hivyo lkn bado inaapply kwa baadhi ya wahusika. Je unawaambiaje hawa ndugu au wahanga kwenye hili la kupishana na a right choice.

Heaven on Earth , BAK , Fixed Point , Kaizer , @Mrembo by nature Mentor na wengineo : Je mnasemaje ktk hili.
 
Mkuu kuna ukweli ktk hili isipokua hapo kwenye blue sidhani kama kila wakati iko hivyo lkn bado inaapply kwa baadhi ya wahusika. Je unawaambiaje hawa ndugu au wahanga kwenye hili la kupishana na a right choice.

Heaven on Earth , BAK , Fixed Point , Kaizer , @Mrembo by nature Mentor na wengineo : Je mnasemaje ktk hili.
mi mbona kama sijaielewa hii mada twin!
hao mr/mrs right wana characteristics gani?
siku zote huwa nafikiriaga nimekutana na wangu.....naye kwa ninavyomwona alivyo na furaha naona kama mimi ndo wake vile..... au mimi naliangalia hili swala kijuu juu tu?
 
^^
Chukua mikono yako miwili..
Kila mkono utanue vidole vyake..
Utazame nafasi za wazi kati ya kidole na kidole..
Kisha iunganishe mikono yote miwili.
Kuna furaha mikono inapoungana.
NDIVYO YALIVYO MAPENZI
Ktk mapenzi wanakutana watu wenye madhaifu ili wazibiane mapungufu.(Hiyo ndiyo sababu)
Ukikuta ndoa ya 'The Rights' ama haidumu au mmoja atakufa
^^
Thank you.
 
Mie kwa maoni yangu watu wanaweka vigezo vingi sana kiasi ambacho inakuwa vigumu kwa Mr Right/Miss Right kukutana na mwrnzie ambaye wanaweza kupendana na hatimaye kufunga ndoa. Miaka iliyopita kwa mfano hiki kigezo kinachotumiwa na wanaume wengi miaka hii kwamba bidada mpaka apate ujauzito ndiyo ndoa itangazwe kilikuwa hakipo kabisa. Watu wakipendana na kuridhiana kwamba kila mtu anaona anaweza kuishi na mwenzie basi wanatangaza ndoa na kisha kufunga pingu za maisha, lakini miaka hii ya karibuni Njemba inaweza kumkubali bidada kwamba ametimiza vigezo vyote vya kuwa mkewe lakini anaweka na kigezo hicho kingine cha, "Sitangazi ndoa mpaka upate ujauzito" sasa kama bi dada naye hayuko tayari kupata ujauzito nje ya ndoa basi mapenzi huingia dosari na watu hawa kutengana.

Pia kuna akina bidada wana vigezo vyao kwa mfano njemba lazima iwe na mshiko wa uhakika, vinginevyo hakutakuwa na ndoa. Miaka ya nyuma watu walipendana na kuanzia chini kabisa wanaanza maisha kwenye chumba kimoja na kujinyima ili kuweza kufanya mambo makubwa katima maisha yao kama vile kujiendeleza kielimu, kuweka akiba ili kuweza kujenga nyumba yao n.k. mpaka nao wakaweza kujiinua kimaisha na kuishi maisha ya juu ukilinganisha na pale walipoanzia. Leo akina bidada wanataka wamkute njemba ana kila kitu nyumba ya ghorofa, magari ya bei mbaya, bank account iliyoshiba moaka zinamwagika. Bidada wa hivi wengi wanaishiwa kuchezewa tu na wakija stuka biological clock ndiyo inakaribia kugota wanaanza kuhangaika huku na kule kutafuta sperm donor yeyote yule angalau naye aweze kuitwa mama. Wachache hubahatika kukutana na njembas mwenye kila kitu. Mahusiano ya miaka hii ni kizungumkuti kikubwa sana.
 
Bila shaka unaongelea love compatibility!!!!!
Mbona inawezekana kwa asilimia mia moja!
...
Unaposema Mr/Mrs right unamaana gani?
Ivi kweli kuna Mr/Mrs ambao sio right?
Kwa kigezo gani?
...
Naomba unijibu kwanza!
 
mi mbona kama sijaielewa hii mada twin!
hao mr/mrs right wana characteristics gani?
siku zote huwa nafikiriaga nimekutana na wangu.....naye kwa ninavyomwona alivyo na furaha naona kama mimi ndo wake vile..... au mimi naliangalia hili swala kijuu juu tu?
Hahahahaha twin wewe uko safi bwana . Unajua huwa inanishangaza kuona watu wengi wanalalamika hawapati watu wanaoendana nao na wakati mwingine unaweza kukutana na wadada wema na wanaofaa kuolewa lkn wanalalamika hawapati wenzi sahihi na pengine pia waweza kutana na wakaka wastarabu tu nao wanakwambia hawapati wenzi sahihi wa kuoa sasa huwa najiuliza inakuaje watu hawa hawakutani.

Nadhani twin umenielewa sasa. Huwa najiuliza je madai yao yako sahihi au wanatoo much expectations kiasi kwamba wanaona kila wamuonae hakolifai.
 
Bila shaka unaongelea love compatibility!!!!!
Mbona inawezekana kwa asilimia mia moja!
...
Unaposema Mr/Mrs right unamaana gani?
Ivi kweli kuna Mr/Mrs ambao sio right?
Kwa kigezo gani?
...
Naomba unijibu kwanza!
Mkuu hapo nilipobold sina maana hiyo kwani watu wanapoamua kuishi pamoja ina maana wamekubaliana . Kuna maswali mengi huwa yapo mitaani huenda na wewe ulishakutana nayo hasa unapozungumza na vijana baadhi yao ktk mazungumzo wanaweza kutoa malalamiko yao kuhusu relationship walizo nazo na hata kudiriki kukwambia walio nao sio watu sahihi. Na ukiwaangalia ni vijana wenye tabia njema kabisa sasa inakuaje hawakutani na wanaowafaa.
 
Mie kwa maoni yangu watu wanaweka vigezo vingi sana kiasi ambacho inakuwa vigumu kwa Mr Right/Miss Right kukutana na mwrnzie ambaye wanaweza kupendana na hatimaye kufunga ndoa. Miaka iliyopita kwa mfano hiki kigezo kinachotumiwa na wanaume wengi miaka hii kwamba bidada mpaka apate ujauzito ndiyo ndoa itangazwe kilikuwa hakipo kabisa. Watu wakipendana na kuridhiana kwamba kila mtu anaona anaweza kuishi na mwenzie basi wanatangaza ndoa na kisha kufunga pingu za maisha, lakini miaka hii ya karibuni Njemba inaweza kumkubali bidada kwamba ametimiza vigezo vyote vya kuwa mkewe lakini anaweka na kigezo hicho kingine cha, "Sitangazi ndoa mpaka upate ujauzito" sasa kama bi dada naye hayuko tayari kupata ujauzito nje ya ndoa basi mapenzi huingia dosari na watu hawa kutengana.

Pia kuna akina bidada wana vigezo vyao kwa mfano njemba lazima iwe na mshiko wa uhakika, vinginevyo hakutakuwa na ndoa. Miaka ya nyuma watu walipendana na kuanzia chini kabisa wanaanza maisha kwenye chumba kimoja na kujinyima ili kuweza kufanya mambo makubwa katima maisha yao kama vile kujiendeleza kielimu, kuweka akiba ili kuweza kujenga nyumba yao n.k. mpaka nao wakaweza kujiinua kimaisha na kuishi maisha ya juu ukilinganisha na pale walipoanzia. Leo akina bidada wanataka wamkute njemba ana kila kitu nyumba ya ghorofa, magari ya bei mbaya, bank account iliyoshiba moaka zinamwagika. Bidada wa hivi wengi wanaishiwa kuchezewa tu na wakija stuka biological clock ndiyo inakaribia kugota wanaanza kuhangaika huku na kule kutafuta sperm donor yeyote yule angalau naye aweze kuitwa mama. Wachache hubahatika kukutana na njembas mwenye kila kitu. Mahusiano ya miaka hii ni kizungumkuti kikubwa sana.
Rafiki asante sana sina cha kuongeza kwani umezungumzia hali halisi kabisa . Kwa hiyo jamii inapaswa kubadili mtazamo ili mambo yawe kama enzi za mwaka 47.
 
Hahahahaha twin wewe uko safi bwana . Unajua huwa inanishangaza kuona watu wengi wanalalamika hawapati watu wanaoendana nao na wakati mwingine unaweza kukutana na wadada wema na wanaofaa kuolewa lkn wanalalamika hawapati wenzi sahihi na pengine pia waweza kutana na wakaka wastarabu tu nao wanakwambia hawapati wenzi sahihi wa kuoa sasa huwa najiuliza inakuaje watu hawa hawakutani.

Nadhani twin umenielewa sasa. Huwa najiuliza je madai yao yako sahihi au wanatoo much expectations kiasi kwamba wanaona kila wamuonae hakolifai.
hapo nimekuelewa twin....
naona rafiki yako BAK kakujibu vizuri sana hapo juu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu hapo nilipobold sina maana hiyo kwani watu wanapoamua kuishi pamoja ina maana wamekubaliana . Kuna maswali mengi huwa yapo mitaani huenda na wewe ulishakutana nayo hasa unapozungumza na vijana baadhi yao ktk mazungumzo wanaweza kutoa malalamiko yao kuhusu relationship walizo nazo na hata kudiriki kukwambia walio nao sio watu sahihi. Na ukiwaangalia ni vijana wenye tabia njema kabisa sasa inakuaje hawakutani na wanaowafaa.

Kila mtu hujiona yuko sahihi, Sio kweli!
Sio kweli kutokana na utofauti wa interests!
Kila mtu anainterest zake!
...
Unaposema Mr/Mrs right bila shaka unaongelea GOOD MORAL! What is moral????
There is no universal definition of Moral!
What is moral to you is not moral to me!
...
Hao ambao huonekana na tabia njema then hawana mahusiano mazuri inawezekana 100%!
Na hawadumu kutokana na sababu 2 hapo juu!
...
Kwa Upande wa pili, ningependa ukubali kuna ndoa ziko vizuri sana, ingawa wengine huwashangaa kwa kuwepo na sifa mbaya kwa wanandoa hao na bado wenyewe wanalisongesha bariida!
...
KITU CHA MSINGI kwanza ni kujielewa mwenyewe!
Je wewe ni social or antisocial?
Mvumilivu or not?
Uko direct or indirect?Muongo au mkweli?
...
Then kabla ya kukurupuka unatakiwa umtambue mwenzio at least katika vipengele hivyo!
...
NB: kuna watu hubahatika kupata right wenza bila mzunguko huo!
Ndoa njema ni bahati!
Nadhani nimesoumeka hapo!
 
Kwangu hakuna kilichochemka mambo yangu yako safi sina shida ktk hili bali nataka tujadili ili tuweze kuwasaidia wengine kwani vilio vimekua vingi hapa jukwaani .
nilisema kilichochema....naamini si kila anaeleta hoja hapa imemgusa yeye moja kwa moja, yawezakuwa ya watu waliomzunguka ama nje ya jamii ila lengo likiwa kuwasaidia wana JF na jamii kwa ujumla
 
wenye mapenzi ya kweli wamekua adimu sana

wengi wanaigiza

Aisee utasubiri sana mpaka yes.u arudi na hutompat mr/ mrs Right. Maisha ya sasa ni bongo flava tu
 
Back
Top Bottom