Greenwhich
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 1,337
- 968
Hizo zote ni chuki na aibu za kuumbuliwa nyie vibaraka msio jua kufikiria uwezo wenu wakufikiri ni sawa na akili za kuku tu. Mmechakachua rasimu ya katiba sababu ya pesa mmesahau kuwa hiyo katiba itakuja kuwahukumu mbeleni CCM haitotawala milele karne hii sio ile ya zama za ujima hii ni karne nyingine, Watanzania wa leo wameelewa mchezo wote mlioufanya CCM mmezoea kufoji hadi kura za marehemu mmefoji amuone haya. SHAME ON YOU
Huyu Mzee ashachanganyikiwa kabisa, laana ya viongozi wa dini ishaanza kumvuruga
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.
Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.
Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.